< Job 42 >

1 Then Job responded to Yahweh, and said: —
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
2 I know that, all things, thou canst do, and that no purpose can be withholden from thee.
“Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote, wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.
3 Who is it that hideth counsel without knowledge? Therefore, have I declared, but not understood, things too wonderful for me, which I could not know.
Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’ Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi, mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.
4 Hear thou, I pray thee, and, I, will speak, I will ask thee, and inform thou me.
“Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena; nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’
5 By the hearing of the ear, had I heard thee, but, now, mine own eye, hath seen thee.
Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako, lakini sasa macho yangu yamekuona.
6 For this cause, I tremble and repent, on dust and ashes.
Kwa hiyo najidharau mwenyewe, na kutubu katika mavumbi na majivu.”
7 And it came to pass, after Yahweh had spoken these words unto Job, that Yahweh, said unto Eliphaz the Temanite, Kindled is mine anger against thee and against thy two friends, for ye have not spoken concerning me the thing that is right, like my servant Job.
Baada ya Bwana kusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira juu yako na juu ya rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.
8 Now, therefore, take unto you seven bullocks and seven rams, and go unto my servant Job, and ye shall offer up an ascending-sacrifice in your own behalf, and, Job my servant, shall pray over you, —for, him, will I accept, that I may not deal out to you disgrace, because ye have not spoken concerning me the thing that is right, like my servant Job.
Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu ataomba kwa ajili yenu, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.”
9 So Eliphaz the Temanite and Bildad the Shuhite [and] Zophar the Naamathite went, and did according to that which Yahweh had spoken unto them, —and Yahweh accepted Job.
Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kama Bwana alivyowaambia; naye Bwana akayakubali maombi ya Ayubu.
10 And, Yahweh himself, turned the captivity of Job, when he prayed in behalf of his friends, —and Yahweh increased all that Job had possessed, unto twice as much.
Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Bwana akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni.
11 Then came unto him all his brethren and all his sisters, and all his former acquaintances, and they did eat bread with him in his house, —and shewed sympathy with him and comforted him, over all the calamity which Yahweh had brought upon him, —and they gave him, every one a weight of money, and every one, a ring of gold.
Ndipo ndugu zake wote waume kwa wake na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni, wakaja wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yote Bwana aliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
12 And, Yahweh, blessed the latter end of Job, more than his beginning, —and so he came to have fourteen thousand sheep, and six thousand camels, and a thousand yoke of oxen, and a thousand she-asses.
Bwana akaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda wa kike elfu moja.
13 And he came to have seven sons, and three daughters;
Tena alikuwa na wana saba na binti watatu.
14 and he called the name of the first Jemima, and the name of the second Kezia, —and the name of the third, Keren-happuch.
Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia na wa tatu Keren-Hapuki.
15 And there were found no women so fair as the daughters of Job, in all the land, —and their father gave them an inheritance, in the midst of their brethren.
Hapakuwepo mahali popote katika nchi ile yote palipopatikana wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.
16 And Job lived, after this, a hundred and forty years, —and saw his sons and his sons’ sons, four generations.
Baada ya hili Ayubu akaishi miaka 140; akawaona wanawe na wana wa wanawe hata kizazi cha nne.
17 So Job died, old and satisfied with days.
Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyekuwa ameshiba siku.

< Job 42 >