< Job 16 >

1 Then responded Job, and said: —
Kisha Ayubu akajibu:
2 I have heard many such things, Wearisome comforters, are ye all!
“Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
3 Is there to be an end to windy words? Or what so strongly exciteth thee, that thou must respond?
Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
4 I also, like you, could speak, —If your soul were in the place of my soul, I could string together words against you, and could therewith shake over you my head.
Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
5 I could make you determined, by my mouth, and then my lip-solace should restrain you.
Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
6 Though I do speak, unassuaged is my stinging pain, —And, if I forbear, of what am I relieved?
“Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
7 But, now, hath he wearied me, thou hast destroyed all my family;
Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
8 And, having captured me, it hath served, as a witness; and so my wasting away hath risen up against me, in my face, it answereth.
Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
9 His anger, hath torn and persecuted me, He hath gnashed upon me with his teeth, Mine adversary, hath sharpened his eyes for me.
Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
10 They have gaped upon me with their mouth, With reproach, have they smitten my cheek, Together, against me, have they closed their ranks.
Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
11 GOD doth abandon me to him that is perverse, and, into the hands of the lawless, he throweth me headlong.
Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
12 At ease, was I when he shattered me, Yea he seized me by my neck, and dashed me in pieces, then set me up for himself as a mark:
Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
13 His archers came round against me, He clave asunder my reins, and spared not, He poured out, on the earth, my gall:
wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
14 He made a breach in me, breach upon breach, He ran upon me, like a mighty man.
Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
15 Sackcloth, sewed I on my skin, and rolled—in the dust—my horn:
“Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
16 My face, is reddened from weeping, and, upon mine eyelashes, is the death-shade: —
Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
17 Though no violence was in my hands, and, my prayer, was pure.
Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
18 O earth! do not cover my blood, and let there be no place for mine outcry.
“Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
19 Even now, lo! in the heavens, is my witness,
Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
20 And, he that voucheth for me is on high. My friends are, they who scorn me, Unto GOD, hath mine eye shed tears: —
Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
21 That one might plead, for a man, with GOD, —Even a son of man, for his friend!
kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
22 When, a few years, come, then, by a path by which I shall not return, shall I depart.
“Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.

< Job 16 >