< Jeremiah 38 >

1 And, when Shephatiah son of Mattan and Gedaliah son of Pashhur and Jucal son of Shelemiah, and Pashhur son of Malchiah, heard the words which Jeremiah was speaking unto all the people saying:
Shefatia mwana wa Matani, na Gedalia mwana wa Pashuri, na Yehukali mwana wa Shelemia, na Pashuri mwana wa Malkiya wakasikia kile Yeremia alichokuwa akiwaambia watu wote wakati aliposema,
2 Thus saith Yahweh, He that remaineth in this city shall die, by sword by famine, or by pestilence, —whereas, he that goeth forth unto the Chaldeans, shall live, so shall he have his life for a spoil, and shall live.
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Yeyote akaaye ndani ya mji huu atakufa kwa upanga, njaa au tauni, lakini yeyote atakayejisalimisha kwa Wakaldayo ataishi. Atakayeyatoa maisha yake kama nyara, ataishi.’
3 Thus, saith Yahweh, —This city shall surely be given, into the hand of the force of the king of Babylon, and he shall capture it.
Tena hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mji huu kwa hakika utatiwa mikononi mwa jeshi la mfalme wa Babeli, ambaye atauteka.’”
4 Then said the princes unto the king, —Let this man we pray thee, be put to death, for in this way, is he weakening the hands of the men of war who are left in this, city, and the hands of all the people, by speaking unto them such words as these; for, this man, is not seeking prosperity for this people but misfortune.
Ndipo maafisa wakamwambia mfalme, “Mtu huyu imempasa kuuawa. Anawakatisha tamaa askari waliobaki katika mji huu, vivyo hivyo na watu wote pia, kwa ajili ya mambo anayowaambia. Mtu huyu hawatakii mema watu hawa, bali maangamizi yao.”
5 Then said King Zedekiah, —Lo! he is in your hand; for the king is not one who is able to do anything against you.
Mfalme Sedekia akajibu, “Yeye yuko mikononi mwenu! Mfalme hawezi kufanya lolote kuwapinga ninyi.”
6 Then took they Jeremiah and cast him into the dungeon of Malchiah son of the king, which was in the guard-court, and they let Jeremiah down with ropes, —now, in the dungeon, was no water only mire, so Jeremiah sank in the mire.
Basi wakamchukua Yeremia na kumtia kwenye kisima cha Malkiya, mwana wa mfalme, kilichokuwa katika ua wa walinzi. Wakamteremsha Yeremia kwa kamba ndani ya kisima. Hakikuwa na maji ndani yake, ila tope tu, naye Yeremia akazama ndani ya matope.
7 When Ebed-melech the Ethiopian one of the eunuchs, he being in the house of the king, heard that they had delivered Jeremiah into the dungeon, —the king being seated in the gate of Benjamin,
Lakini Ebed-Meleki Mkushi, aliyekuwa afisa katika jumba la kifalme, akasikia kuwa walikuwa wamemtia Yeremia ndani ya kisima. Wakati mfalme alipokuwa ameketi katika Lango la Benyamini,
8 then went forth Ebed-melech out of the house of the king, and spake unto the king, saying:
Ebed-Meleki akatoka nje ya jumba la kifalme na kumwambia,
9 My lord, O King! wickedly, have these men done all that they have done to Jeremiah the prophet, whom indeed they have cast into the dungeon, —since he would have died where he was because of the famine, for there is no bread any longer, in the city.
“Mfalme bwana wangu, watu hawa wamefanya uovu kwa yote waliomtendea nabii Yeremia. Wamemtupa ndani ya kisima, mahali ambapo atakufa kwa njaa wakati ambapo hakuna chakula popote katika mji.”
10 Then the king commanded Ebed-melech the Ethiopian saying, —Take with thee from hence thirty men, and lift Jeremiah the prophet out of the dungeon before he die.
Basi mfalme akamwamuru Ebed-Meleki Mkushi, akisema, “Chukua watu thelathini kutoka hapa pamoja nawe, mkamtoe nabii Yeremia huko kwenye kisima kabla hajafa.”
11 So Ebed-melech took the men with him, and went into the house of the king under the treasury, and took thence pieces of cast-off clothes, and old rags, —and let them down unto Jeremiah in the dungeon with the ropes.
Basi Ebed-Meleki akawachukua watu pamoja naye, wakaenda mpaka kwenye chumba kilichoko chini ya hazina ndani ya jumba la kifalme. Akachukua matambaa makuukuu pamoja na nguo zilizochakaa kutoka huko, na kumshushia Yeremia kwa kamba ndani ya kisima.
12 Then said Ebed-melech the Ethiopian unto Jeremiah, —Put, I pray thee the pieces of cast-off clothes and the old rags under thine arm-joints, under the ropes, And Jeremiah did so,
Ebed-Meleki Mkushi akamwambia Yeremia, “Weka haya matambaa makuukuu na hizo nguo zilizochakaa makwapani ili kuzuia kamba.” Yeremia akafanya hivyo,
13 Then drew they Jeremiah with the ropes, and lifted him up out of the dungeon, —and Jeremiah remained in the guard-court.
nao wakamvuta juu kwa kamba na kumtoa katika kisima. Yeremia akakaa katika ua wa walinzi.
14 Then King Zedekiah sent and fetched Jeremiah the prophet unto him, in the third entrance, which is in the house of Yahweh, —and the king said unto Jeremiah—I am going to ask thee a thing, do not hide anything from me.
Ndipo Mfalme Sedekia akatuma watu wamwitie nabii Yeremia wamlete kwake kwenye ingilio la tatu la Hekalu la Bwana. Mfalme akamwambia Yeremia, “Ninataka kukuuliza jambo fulani, usinifiche kitu chochote.”
15 Then said Jeremiah unto Zedekiah, When I tell thee, wilt thou not, surely put me to death? And when I counsel thee, thou wilt not hearken unto me.
Yeremia akamwambia Sedekia, “Nikikupa jibu, je, hutaniua? Hata kama nikikupa shauri, wewe hutanisikiliza.”
16 So King Zedekiah aware unto Jeremiah secretly saying, —By the life of Yahweh who made for us, this soul, I will in no wise put thee to death, Neither will I deliver thee into the hand of these men who are seeking thy life.
Lakini Mfalme Sedekia akamwapia Yeremia kiapo hiki kwa siri, akisema, “Hakika kama aishivyo Bwana, ambaye ametupa pumzi, sitakuua wala sitakutia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wako.”
17 Then said Jeremiah unto Zedekiah—Thus, saith Yahweh God of hosts, God of Israel—If thou wilt, indeed go forth, unto the princes of the king of Babylon, then shall thine own soul live, and, this city, shall not be burned with fire, —but thou shalt live, thou and thy house.
Kisha Yeremia akamwambia Sedekia, “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Ikiwa utajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, maisha yako yatasalimika, na mji huu hautateketezwa kwa moto. Pia wewe na jamaa yako mtaishi.
18 But, if thou wilt not go forth unto the princes of the king of Babylon, then shall this city be delivered into the hand of the Chaldeans, and they shall burn it with fire, and, thou, shalt not escape out of their hand.
Lakini ikiwa hutajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, mji huu utatiwa mikononi mwa Wakaldayo na watauteketeza kwa moto, nawe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao.’”
19 Then said King Zedekiah unto Jeremiah: I am afraid of the Jews who have fallen away unto the Chaldeans, lest they deliver me, into their hand, and they maltreat me.
Mfalme Sedekia akamwambia Yeremia, “Ninawaogopa Wayahudi ambao wamekimbilia kwa Wakaldayo, kwa kuwa Wakaldayo wanaweza kunitia mikononi mwao, nao wakanitenda vibaya.”
20 But Jeremiah said, They shall not deliver!—Hearken I pray thee unto the voice of Yahweh in what I am speaking unto thee, that it may be well with thee and thy soul live.
Yeremia akajibu, “Hawatakutia mikononi mwao. Mtii Bwana kwa kufanya kile ninachokuambia. Kisha utafanikiwa na maisha yako yatakuwa salama.
21 But if thou art refusing to go forth, this, is the thing which Yahweh hath shewed me: —
Lakini ukikataa kujisalimisha, hili ndilo Bwana alilonifunulia:
22 behold, then, all the women that are left in the house of the king of Judah, brought forth unto the princes of the king of Babylon, —and, those very women, saying, The men thou wast wont to salute, have goaded thee on and prevailed upon thee, —Thy foot having sunk in the mire, they have turned away back.
Wanawake wote walioachwa katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda wataletwa mbele ya maafisa wa mfalme wa Babeli. Wanawake hao watakuambia: “‘Walikupotosha na kukushinda, wale rafiki zako uliowaamini. Miguu yako imezama matopeni; rafiki zako wamekuacha.’
23 Yea thou shalt behold all thy wives and thy children brought forth unto the Chaldeans, and thou, shalt not escape out of their hand, —but by the hand of the king of Babylon, shalt thou be taken, and, this city, shall be burned with fire.
“Wake zako wote na watoto wataletwa na kutiwa mikononi mwa Wakaldayo. Wewe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao. Lakini utatekwa na mfalme wa Babeli, na mji huu utateketezwa kwa moto.”
24 Then said Zedekiah unto Jeremiah—Do not let, any man, know of these words, and thou shalt not die.
Kisha Sedekia akamwambia Yeremia, “Usiruhusu mtu yeyote ajue kuhusu haya mazungumzo, la sivyo utakufa.
25 But, when the princes hear that I have spoken with thee and they come in unto thee and say unto thee—Do tell us we pray thee what thou didst speak unto the king, do not hide it from us so will we not put thee to death, —and what spake the king unto, thee?
Maafisa wakisikia kwamba nimezungumza nawe, nao wakakujia na kusema, ‘Tuambie kile ulichozungumza na mfalme na kile mfalme alichokuambia, usitufiche au sivyo tutakuua,’
26 Then shalt thou say unto them, —I was causing my supplication to fall prostrate before the king, —that he would not cause me to return to the house of Jonathan, to die there.
basi waambie, ‘Nilikuwa ninamsihi mfalme asinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani nisije nikafia humo.’”
27 Then came in all the princes unto Jeremiah and asked him, and he told them according to all these words which the king, had commanded, —so they turned in silence from him, for the matter, had not been reported.
Maafisa wote wakamjia Yeremia na kumuuliza, naye Yeremia akawaambia kila kitu mfalme alichomwagiza kusema. Kisha hawakusema lolote zaidi na Yeremia kwa sababu hakuna yeyote aliyesikia mazungumzo yake na mfalme.
28 So Jeremiah remained in the guard-court, until the day when Jerusalem, was captured; thus it fell out when Jerusalem, was captured.
Naye Yeremia akabaki katika ua wa walinzi hadi siku Yerusalemu ilipotekwa.

< Jeremiah 38 >