< Jeremiah 36 >

1 And it came to pass, in the fourth year of Jehoiakim son of Josiah, king of Judah, that this word came unto Jeremiah from Yahweh, saying:
Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema:
2 Take thee a scroll, and write therein all the words which I have spoken unto thee concerning Israel and concerning Judah and concerning all the nations, —from the day I began to speak unto thee from the days of Josiah, even until this day:
“Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
3 Peradventure, the house of Judah will hearken unto all the calamity, which I am devising to execute against them, —to the end they may return every man from his wicked way, whereupon I will forgive their iniquity, and their sin.
Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
4 So Jeremiah called Baruch, son of Neriah, —and Baruch wrote, from the mouth of Jeremiah, all the words of Yahweh which he had spoken unto him upon a scroll.
Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu.
5 Then did Jeremiah command Baruch, saying, —I, am hindered, I cannot enter the house of Yahweh;
Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana.
6 Thou, therefore shalt enter and read in the roll which thou hast written from my mouth the words of Yahweh in the ears of the people in the house of Yahweh on the day of a fast, —moreover also, in the ears of all Judah who are coming in out of their cities, shalt thou read them:
Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao.
7 Peradventure, their supplication, will fall prostrate, before Yahweh, and they return every man from his wicked way, —For, great, are the anger and the indignation which Yahweh hath spoken against this people.
Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”
8 So then Baruch son of Neriah did according to all which Jeremiah the prophet commanded him, reading in the book the words of Yahweh in the house of Yahweh.
Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu.
9 And it came to pass in the fifth year of Jehoiakim son of Josiah king of Judah in the ninth month, that all the people of Jerusalem, and all the people who were coming in out of the cities of Judah into Jerusalem, had proclaimed a fast before Yahweh;
Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
10 Baruch, therefore, read in the book the words of Jeremiah, in the house of Yahweh, —in the chamber of Gemariah son of Shaphan—the scribe, in the upper court, at the opening of the new gate of the house of Yahweh, in the ears of all the people.
Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
11 When Micaiah, son of Gemariah son of Shaphan, heard all the words of Yahweh out of the book,
Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu,
12 then went he down unto the house of the king up to the chamber of the scribe, and lo! there, all the princes sitting, —Elishama the scribe, and Delaiah son of Shemaiah, and Elnathan son of Achbor, and Gemariah son of Shaphan and Zedekiah son of Hananiah, and all the princes,
alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote.
13 So Micaiah told them all the words which he heard, —when Baruch read in the book in the ears of the people.
Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
14 All the princes, therefore sent unto Baruch, Jehudi, son of Nethaniah son of Shelemiah son of Cushi saying, The roll wherein thou didst read in the ears of the people, take it in thy hand, and come, So Baruch son of Neriah took the roll in his hand, and came in unto them.
maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
15 Then said they unto him, Sit down we pray thee and read it in our ears, So Baruch read it in their ears.
Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu.
16 And it came to pass when they heard all the words, that they turned with fear one to another, —and said unto Baruch, We must, surely tell, the king, all these words!
Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
17 Then unto Baruch, put they questions saying, —Tell us, we pray thee, How, didst thou write all these words at his mouth?
Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
18 So Baruch said unto them, With his own mouth, used he to proclaim unto me all these words, —and I kept on writing in the book, with ink.
Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
19 Then said the princes unto Baruch, Go hide thee, thou and Jeremiah, and let no man, know where ye, are!
Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”
20 Then went they in unto the king, into the court, but the roll, had they put in charge, in the chamber of Elishama the scribe, —so they declared in the ears of the king all the words.
Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
21 The king, therefore sent, Jehudi, to fetch the roll, and he fetched it out of the chamber of Elishama the scribe, —and Jehudi read it in the ears of the king, and in the ears of all the princes who were standing near the king.
Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
22 Now, the king, was sitting in the winter house in the ninth month, —with the fire-stove before him burning.
Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
23 So then it came to pass when Jehudi had read three or four columns that he cut it up into fragments with a scribe’s knife, and cast them into the fire that was in the stove, —until, all the roll, was consumed on the fire that was on the stove.
Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea.
24 Yet were they not in dread, neither rent they their garments, —the king, nor any of his servants that were hearing all these words.
Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao.
25 Nevertheless Elnathan and Delaiah and Gemariah, interceded with the king, not to burn the roll, —but he hearkened not unto them.
Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza.
26 Then did the king command Jerahmeel son of the king, and Seraiah son of Azriel, and Shelemiah son of Abdeel, to fetch Baruch the scribe, and Jeremiah the prophet, —but Yahweh had hid them.
Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.
27 Then came the word of Yahweh unto Jeremiah, after the king had burned the roll, and the words which Baruch had written from the mouth of Jeremiah saying:
Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema:
28 Again take thee another roll, and write thereon, all the former words which were on the first roll, which Jehoiakim king of Judah hath burned.
“Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
29 But unto Jehoiakim king of Judah, shalt thou say, Thus, saith Yahweh, —Thou, hast burned this roll saying, Why hast thou written thereon—saying, The king of Babylon shall, certainly, come and lay waste this land, and cause to cease therefrom man and beast?
Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
30 Therefore, Thus, saith Yahweh, Concerning Jehoiakim king of Judah, —He shall have none to sit upon the throne of David, —And, his dead body, shall be cast out—to the heat by day, and to the frost by night;
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
31 And I will visit upon him and upon his seed and upon his servants the punishment of their iniquity, —and will bring upon them and upon the inhabitants of Jerusalem and against, the men of Judah, all the calamity, which I have spoken against them but they have not hearkened.
Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’”
32 So, Jeremiah, took another roll and gave it unto Baruch son of Neriah the scribe, who wrote thereon, from the mouth of Jeremiah all the words of the book, which Jehoiakim king of Judah had burned, in the fire, —and further were added thereunto many words like unto them
Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.

< Jeremiah 36 >