< Jeremiah 29 >

1 Now these, are the, words of the letter which Jeremiah the prophet sent from Jerusalem, —unto the residue of the elders of the captivity, and unto the priests and unto the prophets and unto all the people, whom Nebuchadnezzar had carried away captive from Jerusalem to Babylon;
Haya ni maneno katika waraka ambao Yeremia nabii alituma kutoka Yerusalemu kwa wazee waliosalia miongoni mwa mateka na makuhuni, manabii, na watu wote ambao Nebukadreza aliwapeleka utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli.
2 after that Jeconiah the king and the queen-mother and the eunuchs the princes of Judah and Jerusalem and the craftsmen and the smiths, had gone forth from Jerusalem; —
Hii ilikuwa baada ya Yekonia mfalme, mama yake mfalme, na watumishi wakuu, viongozi wa Yuda na Yerusalemu, na wahunzi walikuwa wamepelekwa mbali na Yerusalemu.
3 by the hand of Elasah son of Shaphan and Gemariah son of Hilkiah, whom Zedekiah king of Judah sent unto Babylon to Nebuchadnezzar king of Babylon, saying: —
Aliutuma waraka huu kwa mkono wa Elasa mwana wa Shafani, Gemaria, mwana wa Hilkia, ambaye Sedekia, mfalme wa Yuda, alikuwa amemtuma kwa Nebukadreza mfalme wa Babeli
4 Thus, saith Yahweh of hosts, God of Israel, Unto all the captivity whom I have suffered to be carried away captive from Jerusalem to Babylon:
Waraka ulisema, Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi kwa mateka ambao niliwasababisha kuwa mateka kutoka Yerusalemu hadi Babeli,
5 Build ye houses and dwell in them, —And plant ye gardens and eat the fruit thereof;
'Jengeni nyumba na muishi ndani yake. Pandeni bustani na mle matunda yake.
6 Take ye wives and beget sons and daughters, And take wives, for your sons, and, your daughters, give ye to husbands, That they may bear sons and daughters, —And so become ye many there and do not become few;
Chukueni wake na mzae wana na mabinti. Kisha Kisha chukueni wake kwa ajili ya wana wenu, na wapatieni waume binti zenu. Wazae wana na mabinti na waongezeke ili msiwe wachache sana.
7 And seek the welfare of the city whither I have caused you to be carried away captives, and pray for her unto Yahweh, —For in her welfare, shall ye have welfare.
Itafuteni amani ya mji ambako nimewafanya kuwa watumwa, na mkauombee kwangu kwa niaba yake kwa kuwa kutakuwa na amani kwenu kama mji uko katika amani.'
8 For Thus, saith Yahweh of hosts God of Israel, Let not your prophets that are in your midst nor your diviners beguile you, —Neither hearken ye unto your dreams which ye are dreaming;
Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi, 'Msiwaache manabii ambao wako katikati yenu na wabashiri wenu kuwadanganya, na msizisikilize ndoto ambazo ninyi wenyewe mnaota.
9 For falsely, are they prophesying unto you in my name, —I have not sent them, Declareth Yahweh.
Kwa maana wanatabiri uongo kwenu katika jina langu. Mimi sikuwatuma—hili ni tangazo la Yahwe.'
10 For, thus, saith Yahweh, —That as soon as there are fulfilled to Babylon seventy years, I will visit you, —and establish for you my good word, by causing you to return unto this place.
Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Babeli atakapokuwa amewatawala kwa muda wa mika sabini, nitawasaidia ninyi na kulitimiza neno langu jema kwa ajili yenu ili kuwarudisha ninyi katika sehemu hii.
11 For, I, know the plans which I am planning for you Declareth Yahweh, —Plans of welfare and not of calamity, To give you a future and a hope.
Kwa maana mimi mwenyewe naijua mipangao niliyonayo kwa ajili yenu—hili ni tangazo la Yahwe—mipango kwa ajili ya amani na siyo kwa ajili ya mabaya, ili kuwapa ninyi tumaini na siku zenu za mwisho.
12 So shall ye call upon me, —And go and pray unto me, —And I will hearken unto you;
Kisha mtaniita, na kwenda na kuniomba mimi, na nitawasikiliza.
13 So shall ye seek me and find, For ye will enquire after me with all your heart;
Kwa maana mtanitafuta na kunipata, kwa kuwa mtanitafuta kwa moyo wenu wote.
14 And I will be found of you, Declareth Yahweh, And will turn back your captivity, And will gather you out of all the nations and out of all the places whither I have driven you, Declareth Yahweh, And will bring you back into the place whence I had caused you to be carried away captive:
Kisha nitapatikana kwenu—hili ni tangazo la Yahwe—na nitawarudisha watu wenu waliofungwa; nitawakusanya kutoka mataifa yote na sehehemu zote ambako nimewatawanya—hili ni tangazo la Yahwe—kwa maana nitawarudisha kutoka sehemu ambako niliwasababisha kuwa mateka.
15 Because ye have said, —Yahweh hath raised us up prophets in Babylon.
Tangu mliposema kwamba Yahwe ameinua manabii kwa ajili yetu katika Babeli,
16 For, thus, saith Yahweh Against the king who is sitting on the throne of David, and Against all the people who are remaining in this city, —your brethren who have not gone forth with you into captivity:
Yahwe anasema hivi kwa mfalme aliyeketi katika kiti cha enzi cha Daudi na watu wote wakaao katika mji huo, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi utumwani—
17 Thus, saith Yahweh of hosts, Behold me! sending upon them sword famine, and pestilence, —So will I make them like the horrid figs, that cannot be eaten for badness;
Yahwe wa majeshi anasema hivi, ''Ona, niko karibu kutuma upanga, njaa, na ugonjwa juu yao. Kwa maana nitawafanya kuwa kama tini mbovu ambazo ni mbaya sana hazifai kuliwa.
18 Therefore will I pursue them with sword with famine and with pestilence, —And will make them a terror to all the kingdoms of the earth A curse and an astonishment and a hissing and a reproach, among all the nations whither I have driven them:
Kisha nitawafuata kwa upanga, njaa, na tauni na kuwafanya kuwa kitu cha kushangaza kwa falme zote juu ya dunia—kitu cha kuogofya, kitu cha kulaaniwa na kuzomewa, na kitu cha aibu miongoni mwa mataifa yote ambako nilimtawanya.
19 Because they hearkened not unto my words Declareth Yahweh, —which I sent unto them by my servants the prophets, betimes, sending them yet hearkened they not Declareth Yahweh.
Hii ni kwa sababu hawakulisikiliza neno langu—hili ni tangazo la Yahwe—ambalo nililituma kwao kupitia watumishi wangu manabii. Niliwatuma tena na tena, lakini hamkusikiliza—hili ni tangazo la Yahwe. '
20 Ye, therefore, hear ye the word of Yahweh, all ye of the captivity, whom I have sent from Jerusalem to Babylon:
Kwa hiyo ninyi wenyewe sikilizeni neno la Yahwe, ninyi mateka wote ambao amewatuma kutoka Yerusalemu hadi Babeli,
21 Thus, saith Yahweh of hosts, God of Israel Concerning Ahab son of Kolaiah, and concerning Zedekiah son of Maaseiah, who are prophesying to you in my name, a falsehood, Behold me! delivering them into the hand of Nebuchadrezzar king of Babylon, and he will smite them before your eyes:
'Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya na Sedekia mwana wa Maaseya, watabirio uongo kwenu katika jina langu: Ona, niko karibu kuwaweka katika mkono wa Nebukadreza mfalme wa Babeli. Atawaua mbele ya macho yenu.
22 So shall there be taken up—from them—a curse, by all of the captivity of Judah who are in Babylon saying, —Yahweh make thee like Zedekiah and like Ahab, Whom the king of Babylon roasted in the fire!
Kisha laana itatamkwa na wafungwa wote wa Yuda katika Babeli kuhusu watu hawa. Laana itasema: Yahwe awafanye kuwa kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwaoka kwenye moto.
23 Because they have committed vileness in Israel And have committed adultery with the wives of their neighbours, And have spoken as a word in my name a falsehood, which I commanded them not, —And, I, am one who knoweth—and a witness Declareth Yahweh.
Hili litatokea kwa sababu ya mambo ya aibu waliyofanya katika Israeli walipofanya uzinzi na wake za majarani zao na kutangaza maneno ya uongo katika jina langu, mambo ambayo sikuwaamuru wayaseme. Kwa maana mimi ndiye nijuaye; mimi ni shahidi—hili ni tangazo la Yahwe.”'
24 Also unto Shemaiah the Nehelamite, shalt thou speak, saying:
Kuhusu Shemaya Mnehelami, sema hivi:
25 Thus, speaketh Yahweh of hosts, God of Israel, saying, —Because, thou, hast sent in, thine own name, letters, unto all the people who are in Jerusalem, and unto Zephaniah son, of Maaseiah the priest, and unto all the priests saying:
'Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwa sababu ulituma barua kwa jina lako kwa watu wote katika Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa Maaseya kuhani, na kwa makuhani wote, na ulisema,
26 Yahweh, hath made thee priest instead of Jehoiada the priest, that ye should be deputies in the house of Yahweh, to any man who is raving and prophesying, so shalt thou put him into the stocks and into the pillory:
“Yahwe aliwafanya ninyi kuwa makuhani badala ya Yehoyada kuhani, ili muwe wasimamizi wa nyumba ya Yahwe. Ninyi ni viongozi wa watu wote wajitiao wazimu na kujifanya wenyewe manabii. Mtawaweka katika mkatale na minyororo.
27 Now, therefore, why, hast thou not rebuked Jeremiah of Anathoth, who is prophesying unto you?
Kwa hiyo sasa, kwa nini hamkumkemea Yeremia wa Anathothi, ambaye hujifanya mwenyewe nabii juu yenu?
28 For, on this account, hath he sent unto us in Babylon, saying, —’Tis, long! Build ye houses and dwell in them, And plant gardens and eat the fruit thereof.
Kwa maana ametutumia sisi katika Babeli, 'Itakuwa muda mrefu. Jengeni nyumba na muishi ndani yake, na pandeni busitani na mule matunda yake.””
29 And Zephaniah the priest hath read this letter in the ears of Jeremiah the prophet,
Sefania kuhani akaisoma barua hii mbele ya Yeremia nabii.
30 Therefore hath the word of Yahweh come unto Jeremiah, saying:
Kisha neno la Yahwe likaja kwa Yeremia, likisema,
31 Send thou unto all them of the captivity, saying, Thus, saith Yahweh, Concerning Shemaiah the Nehelamite, —Because Shemaiah, hath prophesied to you, when, I, had not sent him, And hath caused you to trust in falsehood,
“tuma neno kwa mateka wote na sema, 'Yahwe anasema hivi kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi wakati mimi sikumtuma, na amewaongoza kuamini uongo,
32 Therefore Thus, saith Yahweh, —Behold me! bringing punishment upon Shemaiah the Nehelamite, and upon his seed, He shall have no man to dwell in the midst of this people, Nor shall he see the good that I am about to do for my people, Declareth Yahweh; Because revolt, hath he spoken against Yahweh.
kwa hiyo Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kumwadhibu Shemaya Mnehelami na uzao wake. Hapatakuwa na mtu wa kukaa miongoni mwa watu hawa kwa ajili yake. Hataona mema nitakayofanya kwa ajili ya watu wangu—hili ni tangazo la Yahwe—kwa maana ametangaza uasi dhidi ya Yahwe.””

< Jeremiah 29 >