< Jeremiah 29 >

1 Now these, are the, words of the letter which Jeremiah the prophet sent from Jerusalem, —unto the residue of the elders of the captivity, and unto the priests and unto the prophets and unto all the people, whom Nebuchadnezzar had carried away captive from Jerusalem to Babylon;
Haya ndiyo maneno ya ile barua ambayo nabii Yeremia aliituma kutoka Yerusalemu kwenda kwa wazee waliobaki miongoni mwa wale waliohamishwa, na kwa makuhani, manabii na watu wengine wote ambao Nebukadneza alikuwa amewachukua kwenda uhamishoni Babeli kutoka Yerusalemu.
2 after that Jeconiah the king and the queen-mother and the eunuchs the princes of Judah and Jerusalem and the craftsmen and the smiths, had gone forth from Jerusalem; —
(Hii ilikuwa ni baada ya Mfalme Yekonia na malkia mamaye, maafisa wa mahakama, viongozi wa Yuda na wa Yerusalemu, mafundi na wahunzi kwenda uhamishoni kutoka Yerusalemu.)
3 by the hand of Elasah son of Shaphan and Gemariah son of Hilkiah, whom Zedekiah king of Judah sent unto Babylon to Nebuchadnezzar king of Babylon, saying: —
Barua ilikabidhiwa kwa Elasa mwana wa Shafani, na kwa Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Sedekia mfalme wa Yuda aliwatuma kwa Mfalme Nebukadneza huko Babeli. Barua yenyewe ilisema:
4 Thus, saith Yahweh of hosts, God of Israel, Unto all the captivity whom I have suffered to be carried away captive from Jerusalem to Babylon:
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, awaambialo wale wote niliowapeleka kutoka Yerusalemu kwenda uhamishoni Babeli:
5 Build ye houses and dwell in them, —And plant ye gardens and eat the fruit thereof;
“Jengeni nyumba na mstarehe, pandeni bustani na mle mazao yake.
6 Take ye wives and beget sons and daughters, And take wives, for your sons, and, your daughters, give ye to husbands, That they may bear sons and daughters, —And so become ye many there and do not become few;
Oeni wake na mzae wana na binti, waozeni wana wenu wake, nanyi watoeni binti zenu waolewe, ili nao pia wazae wana na binti. Ongezekeni idadi yenu huko, wala msipungue.
7 And seek the welfare of the city whither I have caused you to be carried away captives, and pray for her unto Yahweh, —For in her welfare, shall ye have welfare.
Pia tafuteni amani na mafanikio ya mji ambamo nimewapeleka uhamishoni. Mwombeni Bwana kwa ajili ya mji huo, kwa sababu ukistawi, ninyi pia mtastawi.”
8 For Thus, saith Yahweh of hosts God of Israel, Let not your prophets that are in your midst nor your diviners beguile you, —Neither hearken ye unto your dreams which ye are dreaming;
Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Msikubali manabii na wabashiri walioko miongoni mwenu wawadanganye. Msisikilize ndoto ambazo mmewatia moyo kuota.
9 For falsely, are they prophesying unto you in my name, —I have not sent them, Declareth Yahweh.
Wanawatabiria ninyi uongo kwa jina langu. Sikuwatuma,” asema Bwana.
10 For, thus, saith Yahweh, —That as soon as there are fulfilled to Babylon seventy years, I will visit you, —and establish for you my good word, by causing you to return unto this place.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Miaka sabini itakapotimia kwa ajili ya Babeli, nitakuja kwenu na kutimiza ahadi yangu ya rehema ya kuwarudisha mahali hapa.
11 For, I, know the plans which I am planning for you Declareth Yahweh, —Plans of welfare and not of calamity, To give you a future and a hope.
Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,” asema Bwana, “ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru, ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo.
12 So shall ye call upon me, —And go and pray unto me, —And I will hearken unto you;
Kisha mtaniita, na mtakuja na kuniomba, nami nitawasikiliza.
13 So shall ye seek me and find, For ye will enquire after me with all your heart;
Mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
14 And I will be found of you, Declareth Yahweh, And will turn back your captivity, And will gather you out of all the nations and out of all the places whither I have driven you, Declareth Yahweh, And will bring you back into the place whence I had caused you to be carried away captive:
Nitaonekana kwenu,” asema Bwana, “nami nitawarudisha watu wenu waliotekwa. Nitawakusanya kutoka mataifa yote na mahali pote nilipokuwa nimewafukuzia, nami nitawarudisha mahali ambapo nilikuwa nimewatoa walipochukuliwa uhamishoni,” asema Bwana.
15 Because ye have said, —Yahweh hath raised us up prophets in Babylon.
Mnaweza mkasema, “Bwana ameinua manabii kwa ajili yetu huku Babeli,”
16 For, thus, saith Yahweh Against the king who is sitting on the throne of David, and Against all the people who are remaining in this city, —your brethren who have not gone forth with you into captivity:
lakini hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme aketiaye kiti cha enzi cha Daudi, na watu wa kwenu wote wanaobaki katika mji huu, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni.
17 Thus, saith Yahweh of hosts, Behold me! sending upon them sword famine, and pestilence, —So will I make them like the horrid figs, that cannot be eaten for badness;
Naam, hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Nitatuma upanga, njaa na tauni dhidi yao, nami nitawafanya kuwa kama tini dhaifu zile ambazo ni mbovu sana zisizofaa kuliwa.
18 Therefore will I pursue them with sword with famine and with pestilence, —And will make them a terror to all the kingdoms of the earth A curse and an astonishment and a hissing and a reproach, among all the nations whither I have driven them:
Nitawafukuza kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni, nami nitawafanya kitu cha kuchukiza sana kwa falme zote za dunia, na kuwa kitu cha laana na cha kuogofya, cha dharau na kukemewa, miongoni mwa mataifa yote nitakakowafukuzia.
19 Because they hearkened not unto my words Declareth Yahweh, —which I sent unto them by my servants the prophets, betimes, sending them yet hearkened they not Declareth Yahweh.
Kwa kuwa hawakuyasikiliza maneno yangu,” asema Bwana, “maneno ambayo niliwatumia tena na tena kupitia watumishi wangu manabii. Wala ninyi watu wa uhamisho hamkusikiliza pia,” asema Bwana.
20 Ye, therefore, hear ye the word of Yahweh, all ye of the captivity, whom I have sent from Jerusalem to Babylon:
Kwa hiyo, sikieni neno la Bwana, enyi nyote mlio uhamishoni, niliowapeleka Babeli kutoka Yerusalemu.
21 Thus, saith Yahweh of hosts, God of Israel Concerning Ahab son of Kolaiah, and concerning Zedekiah son of Maaseiah, who are prophesying to you in my name, a falsehood, Behold me! delivering them into the hand of Nebuchadrezzar king of Babylon, and he will smite them before your eyes:
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya, na Sedekia mwana wa Maaseya, wanaowatabiria uongo kwa jina langu: “Nitawatia mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atawaua mbele ya macho yenu hasa.
22 So shall there be taken up—from them—a curse, by all of the captivity of Judah who are in Babylon saying, —Yahweh make thee like Zedekiah and like Ahab, Whom the king of Babylon roasted in the fire!
Kwa ajili yao, watu wote wa uhamisho kutoka Yuda walioko Babeli watatumia laana hii: ‘Bwana na akutendee kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwachoma kwa moto.’
23 Because they have committed vileness in Israel And have committed adultery with the wives of their neighbours, And have spoken as a word in my name a falsehood, which I commanded them not, —And, I, am one who knoweth—and a witness Declareth Yahweh.
Kwa kuwa wamefanya mambo maovu kabisa katika Israeli, wamezini na wake za majirani zao, tena kwa Jina langu wamesema uongo, mambo ambayo sikuwaambia kuyafanya. Nami nayajua haya, na ni shahidi wa jambo hilo,” asema Bwana.
24 Also unto Shemaiah the Nehelamite, shalt thou speak, saying:
Mwambie Shemaya Mnehelami,
25 Thus, speaketh Yahweh of hosts, God of Israel, saying, —Because, thou, hast sent in, thine own name, letters, unto all the people who are in Jerusalem, and unto Zephaniah son, of Maaseiah the priest, and unto all the priests saying:
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ulituma barua kwa jina lako mwenyewe kwa watu wote wa Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa kuhani Maaseya na kwa makuhani wengine wote. Ulimwambia Sefania,
26 Yahweh, hath made thee priest instead of Jehoiada the priest, that ye should be deputies in the house of Yahweh, to any man who is raving and prophesying, so shalt thou put him into the stocks and into the pillory:
‘Bwana amekuweka wewe uwe kuhani badala ya Yehoyada ili uwe msimamizi wa nyumba ya Bwana. Unapaswa kufunga kwa mikatale na mnyororo wa shingoni mwendawazimu yeyote anayejifanya nabii.
27 Now, therefore, why, hast thou not rebuked Jeremiah of Anathoth, who is prophesying unto you?
Kwa nini basi hukumkemea Yeremia Mwanathothi, aliyejifanya kama nabii miongoni mwenu?
28 For, on this account, hath he sent unto us in Babylon, saying, —’Tis, long! Build ye houses and dwell in them, And plant gardens and eat the fruit thereof.
Ametutumia ujumbe huu huku Babeli: Mtakuwako huko muda mrefu. Kwa hiyo jengeni nyumba mkakae; pandeni mashamba na mle mazao yake.’”
29 And Zephaniah the priest hath read this letter in the ears of Jeremiah the prophet,
Kuhani Sefania, hata hivyo, akamsomea nabii Yeremia ile barua.
30 Therefore hath the word of Yahweh come unto Jeremiah, saying:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
31 Send thou unto all them of the captivity, saying, Thus, saith Yahweh, Concerning Shemaiah the Nehelamite, —Because Shemaiah, hath prophesied to you, when, I, had not sent him, And hath caused you to trust in falsehood,
“Tuma ujumbe huu kwa watu wote walio uhamishoni: ‘Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi, hata ingawa sikumtuma, naye amewafanya kuamini uongo,
32 Therefore Thus, saith Yahweh, —Behold me! bringing punishment upon Shemaiah the Nehelamite, and upon his seed, He shall have no man to dwell in the midst of this people, Nor shall he see the good that I am about to do for my people, Declareth Yahweh; Because revolt, hath he spoken against Yahweh.
hili ndilo Bwana asemalo: Hakika nitamwadhibu Shemaya Mnehelami pamoja na uzao wake. Hapatakuwa na yeyote atakayebaki miongoni mwa watu hawa, wala hataona mema nitakayowatendea watu wangu, asema Bwana, kwa sababu ametangaza uasi dhidi yangu.’”

< Jeremiah 29 >