< Jeremiah 17 >

1 The sin of Judah, is written With a stylus of iron, With the point of a diamond: It is engraved Upon the tablet of their heart, And upon the horns of your altars;
“Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma, imeandikwa kwa ncha ya almasi, kwenye vibao vya mioyo yao na kwenye pembe za madhabahu zao.
2 So long as their sons remember their altars, and their Sacred Stems, By the green tree, —Upon the high hills,
Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao na nguzo za Ashera, kandokando ya miti iliyotanda na juu ya vilima virefu.
3 O my mountain in the field Thy substance all thy treasures, for a prey, will I give: Thy high places for sin, within all thy bounds.
Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri na hazina zako zote nitazitoa ziwe nyara, pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.
4 So shalt thou even of thyself, suffer to rest the inheritance which I gave thee, Seeing that I will cause thee to serve thine enemies, in the land which thou knowest not; For, a fire, have ye kindled in mine anger, Unto times age-abiding, shall it burn.
Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza urithi niliokupa. Nitakufanya mtumwa wa adui zako katika nchi usiyoijua, kwa kuwa umeiwasha hasira yangu, nayo itawaka milele.”
5 Thus, saith Yahweh Accursed is the man—Who trusteth in a son of earth, And hath made flesh his arm, —And whose heart from Yahweh, turneth aside:
Hili ndilo asemalo Bwana: “Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu, ategemeaye mwenye mwili kwa ajili ya nguvu zake, ambaye moyo wake umemwacha Bwana.
6 Therefore shall he become as a shrub in the waste plain, Neither shall he perceive when good cometh, But shall inhabit Parched places in a wilderness, A land of salt that cannot be dwelt in.
Atakuwa kama kichaka cha jangwani; hataona mafanikio yatakapokuja. Ataishi katika sehemu zisizo na maji, katika nchi ya chumvi ambapo hakuna yeyote aishiye humo.
7 Blessed is the man Who trusteth in Yahweh, To whom Yahweh is his ground of confidence;
“Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana, ambaye matumaini yake ni katika Bwana.
8 For he shall become like a tree planted by waters, And, by a stream, shall he send out his roots, Neither shall he perceive when heat cometh, But, his leaf shall continue green: Even in a year of dearth, shall he not be anxious, Neither shall he cease from bearing fruit.
Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji. Hauogopi wakati wa joto ujapo; majani yake ni mabichi daima. Hauna hofu katika mwaka wa ukame na hautaacha kuzaa matunda.”
9 Deceitful is the heart above all things And, dangerously wayward, —Who can know it?
Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote, ni mwovu kupita kiasi. Ni nani awezaye kuujua?
10 I—Yahweh, Searching the heart, Testing the affections; And giving to every man According to his way, According to the fruit of his doings.
“Mimi Bwana huchunguza moyo na kuzijaribu nia, ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake, kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”
11 As a partridge gathereth eggs she did not lay, [So] is he that maketh riches but not with justice, —In the midst of his days, shall he leave them, And in his latter end, prove to have been base.
Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga, ndivyo alivyo mtu apataye mali kwa njia zisizo za haki. Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha, na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.
12 A throne of glory, exalted from the beginning, hath been the place of our sanctuary.
Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo, ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.
13 Thou hope of Israel Yahweh, All who forsake thee, shall turn pale, —Yea, all who depart from me, in the ground, shall be written, For they have forsaken a fountain of living water, even Yahweh.
Ee Bwana, uliye tumaini la Israeli, wote wakuachao wataaibika. Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini kwa sababu wamemwacha Bwana, chemchemi ya maji yaliyo hai.
14 Heal thou me O Yahweh, that I may be healed, Save me that I may be saved, —For, my praise, thou art!
Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe nami nitaokoka, kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.
15 Lo! they, are saying unto me, —Where is the word of Yahweh? Pray thee let it come to pass!
Wao huendelea kuniambia, “Liko wapi neno la Bwana? Sasa na litimie!”
16 But as for me, I have neither forced myself away from tending the flock after thee, Nor yet for the woeful day, have I longed—thou, knowest, —That which came out of my lips, before thy face, was uttered.
Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako; unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa. Kile kipitacho midomoni mwangu ki wazi mbele yako.
17 Do not thou become to me a terror, —My refuge, art thou, in the day of calamity.
Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu; wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.
18 Let my persecutors, turn pale, but let not me, turn pale, Let, them, be terrified, but let not, me, be terrified, —Bring thou upon them a day of calamity, And with a double fracture, destroy them.
Watesi wangu na waaibishwe, lakini nilinde mimi nisiaibike; wao na watiwe hofu kuu, lakini unilinde mimi na hofu kuu. Waletee siku ya maafa; waangamize kwa maangamizi maradufu.
19 Thus, said Yahweh unto me—Go and stand in the gate of the sons of the people, through which the kings of Judah enter in, and through which they come out, —also in all the gates of Jerusalem.
Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu.
20 Then shalt thou say unto them—Hear ye the word of Yahweh Ye kings of Judah and all Judah, And all ye inhabitants of Jerusalem, —who enter in through these gates:
Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wote wa Yuda, na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya.
21 Thus, saith Yahweh, Take heed unto your souls, —And do not bear any burden on the sabbath day, Nor bring it in through the gates of Jerusalem, —
Hili ndilo asemalo Bwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu.
22 Neither shall ye take forth any burden out of your houses on the sabbath day, Nor any manner of work, shall ye do, —But ye shall hallow the sabbath day, As I commanded your fathers.
Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yoyote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu.
23 Howbeit they hearkened not, neither inclined their ear, —but stiffened their neck, that they might not hearken, neither receive correction.
Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao, na hawakutaka kusikia wala kukubali adhabu.
24 And it shall come to pass, —If ye will, indeed hearken, unto me Declareth Yahweh, To bring in no burden through the gates of this city, on the sabbath day, —But to hallow the sabbath day, by not doing thereon any manner of work,
Lakini mkiwa waangalifu kunitii, asema Bwana, nanyi msipoleta mzigo wowote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo,
25 Then shall enter in through the gates of this city, Kings and princes Sitting on the throne of David, Riding in chariots and on horses They, and their princes, The men of Judah and the inhabitants of Jerusalem, And this city shall remain unto times age-abiding.
ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi wataingia kupitia malango ya mji huu, pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima.
26 And they shall come in—Out of the cities of Judah and Out of the places round about Jerusalem, and Out of the land of Benjamin, and Out of the lowlands, and out of the hill country, and Out of the South, Bringing in ascending-offering, and peace-offering, and meal-offering, and frankincense, —Even they who bring in a thank-offering into the house of Yahweh,
Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana.
27 But, if ye will not hearken unto me—To hallow the sabbath day, And to bear no burden and bring in through the gates of Jerusalem, on the sabbath day, Then will I kindle a fire within her gates, And it shall devour the palaces of Jerusalem, And shall not be quenched.
Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wowote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’”

< Jeremiah 17 >