< Isaiah 6 >

1 In the year that King Uzziah died, I saw My Lord, sitting upon a throne high and lifted up, and, his skirts, did fill the temple,
Katika mwaka ule Mfalme Uzia alikufa, nilimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu na kilichotukuzwa sana, nalo pindo la joho lake likajaza Hekalu.
2 Seraphim, were standing above him; six wings severally, had each one, —With twain, he covered his face And with twain, he covered his feet And with twain, he did fly.
Juu yake walikuwepo maserafi, kila mmoja alikuwa na mabawa sita: Kwa mabawa mawili walifunika nyuso zao, kwa mengine mawili walifunika miguu yao, na kwa mawili walikuwa wakiruka.
3 And they continued crying out one to another, and said, Holy—holy—holy, is Yahweh of hosts, —the fulness of the whole earth, is his glory.
Nao walikuwa wakiitana kila mmoja na mwenzake: “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu ni Bwana Mwenye Nguvu Zote; dunia yote imejaa utukufu wake.”
4 And the foundations of the porch, were moved at the voice of him that cried, —and the house, was filled with smoke.
Kwa sauti zao, miimo ya milango na vizingiti vilitikisika, nalo Hekalu likajaa moshi.
5 Then said I—Woe to me!—for I am undone, Because a man of unclean lips, am, I, And in the midst of a people of unclean lips, do I dwell, —For the King. Yahweh of hosts, have mine eyes seen!
Ndipo nikalia, “Ole wangu! Nimeangamia! Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninaishi katikati ya watu wenye midomo michafu, nayo macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
6 Then flew unto me one of the seraphim, And in his hand, a live coal, —With tongs, had he taken it from off the altar.
Ndipo mmoja wa wale maserafi akaruka kunijia akiwa na kaa la moto linalowaka mkononi mwake, ambalo alikuwa amelichukua kwa koleo kutoka madhabahuni.
7 Then touched he my mouth, and said—Lo! this hath touched thy lips, —Thus shall be taken away, thine iniquity, And, thy sin, by propitiation be covered.
Akanigusa nalo kinywa changu na kusema, “Tazama, hili limegusa midomo yako, uovu wako umeondolewa, nayo dhambi yako imesamehewa.”
8 Then heard I the voice of My Lord, saying, Whom shall I send? And who will go for us? And I said—Here am I—send me.
Kisha nikasikia sauti ya Bwana ikisema, “Nimtume nani? Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?” Nami nikasema, “Mimi hapa. Nitume mimi!”
9 Then said he—Go and say unto this people, —Hear on but do not discern, See on but do not perceive:
Akasema, “Nenda ukawaambie watu hawa: “‘Mtaendelea daima kusikiliza, lakini kamwe hamtaelewa; mtaendelea daima kutazama, lakini kamwe hamtatambua.’
10 Stupefy thou the heart of this people, And their ears, make thou heavy, And their eyes, overspread, —Lest they see with their eyes And with their ears, should hear, And their heart should discern and come back. And they be healed.
Fanya mioyo ya watu hawa kuwa migumu, fanya masikio yao yasisikie, na upofushe macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, nao wakageuka, nikawaponywa.”
11 Then said I—How long, My Lord? And he said—Until the time that Cities be wasted through having no inhabitant And houses—through having no men, And, the ground, be laid waste unto desolation;
Ndipo nikasema, “Hadi lini, Ee Bwana?” Naye akanijibu: “Hadi miji iwe imeachwa magofu na bila wakazi, hadi nyumba zitakapobaki bila watu, na mashamba yatakapoharibiwa na kuangamizwa,
12 And Yahweh have far removed men, —And great! be the abandonment in the midst of the land.
hadi Bwana atakapokuwa amekwisha kumpeleka kila mmoja mbali sana, na nchi itakapokuwa imeachwa kabisa.
13 Yet still shall there be in it a tenth, Though it again be consumed, —Like an oak and like a terebinth Which when felled, have a stock in them, A holy seed, shall be the stock thereof.
Hata kama sehemu ya kumi ya watu watabaki katika nchi, itaharibiwa tena. Lakini kama vile mvinje na mwaloni ibakizavyo visiki inapokatwa, ndivyo mbegu takatifu itakavyokuwa kisiki katika nchi.”

< Isaiah 6 >