< Isaiah 2 >

1 That which Isaiah, son of Amoz saw in vision, —concerning Judah and Jerusalem.
Hili ndilo aliloliona Isaya mwana wa Amozi kuhusu Yuda na Yerusalemu:
2 But it shall come to pass, in the afterpart of the days, That the mountain of the house of Yahweh Shall be, set up, as the head of the mountains, And be exalted above the hills, —And all the nations, shall stream thereunto;
Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote, utainuliwa juu ya vilima, na mataifa yote yatamiminika huko.
3 And many peoples shall go and say—Come ye, and let us ascend Unto the mountain of Yahweh Unto the house of the God of Jacob, That he may teach us of his ways, And we may walk in his paths, —For, out of Zion, shall go forth a law, And the word of Yahweh out of Jerusalem;
Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
4 And he will judge between the nations, And be umpire to many peoples, —And they will beat their swords into ploughshares and their spears into pruning-hooks, Nation—against nation, shall not lift up sword, Neither shall they learn any more to make war,
Atahukumu kati ya mataifa na ataamua migogoro ya mataifa mengi. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
5 O house of Jacob! come ye and let us walk in the light of Yahweh.
Njooni, enyi nyumba ya Yakobo, tutembeeni katika nuru ya Bwana.
6 Therefore hast thou abandoned thy people the house of Jacob, Because they have become full of the East, And use hidden arts like the Philistines, —And with the children of foreigners, strike hands; —
Umewatelekeza watu wako, nyumba ya Yakobo. Wamejaa ushirikina utokao Mashariki, wanapiga ramli kama Wafilisti na wanashikana mikono na wapagani.
7 So that filled is their land with silver and gold, And there is no end to their treasures, —And filled is their land with horses, And there is no end to their chariots;
Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hakuna mwisho wa hazina zao. Nchi yao imejaa farasi, hakuna mwisho wa magari yao.
8 And filled is their land with idols, —To the work of their own hands, do they bow themselves down, To that which they made with their own fingers.
Nchi yao imejaa sanamu, wanasujudia kazi za mikono yao, vitu vile vidole vyao vimevitengeneza.
9 So the mean man boweth down And the great man stoopeth low, —Therefore do not thou forgive them!
Kwa hiyo mwanadamu atashushwa na binadamu atanyenyekezwa: usiwasamehe.
10 Enter into the rock, Or hide thee in the dust, —Because of the terribleness of Yahweh, And for his majestic splendour.
Ingieni kwenye miamba, jificheni ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake!
11 The lofty looks of mean men, shall be humbled, And, the haughtiness of great men, shall be bowed down, —And Yahweh alone shall be exalted in that day.
Macho ya mtu mwenye majivuno yatanyenyekezwa na kiburi cha wanadamu kitashushwa, Bwana peke yake ndiye atakayetukuzwa siku hiyo.
12 For, a day of Yahweh of hosts, [shall be] —Upon every one who is high and lofty, —And upon every one who is lifted up, And he shall be brought low;
Bwana Mwenye Nguvu Zote anayo siku aliyoiweka akiba kwa wote wenye kujivuna na wenye kiburi, kwa wote wanaojikweza (nao watanyenyekezwa),
13 And upon all cedars of Lebanon, that are high and lifted up, —And upon all the oaks of Bashan;
kwa mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu sana, na mialoni yote ya Bashani,
14 And upon all the lofty mountains, —And upon all the uplifted hills;
kwa milima yote mirefu na vilima vyote vilivyoinuka,
15 And upon every high tower, —And upon every fortress wall;
kwa kila mnara ulio mrefu sana na kila ukuta wenye ngome,
16 And upon all the ships of Tarshish, —And upon all desirable banners.
kwa kila meli ya biashara, na kila chombo cha baharini cha fahari.
17 And the haughtiness of mean men, shall be humbled, —And the loftiness of great men, shall be laid low, —And Yahweh alone shall be exalted in that day.
Majivuno ya mwanadamu yatashushwa, na kiburi cha wanadamu kitanyenyekezwa, Bwana peke yake ndiye atatukuzwa siku hiyo,
18 And, the idols, shall wholly pass away;
nazo sanamu zitatoweka kabisa.
19 And they shall enter into the holes of the rocks, and into the caves of clay, —Because of the terribleness of Yahweh, And for his majestic splendour, When he ariseth to shake terribly the earth.
Watu watakimbilia kwenye mapango ndani ya miamba, na kwenye mahandaki ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
20 In that day shall the son of earth cast his idols of silver, and his idols of gold, —which had been made for him to worship, into the hole of the mice, and to the bats;
Siku ile, watu watawatupia panya na popo sanamu zao za fedha na za dhahabu, walizozitengeneza ili waziabudu.
21 That he may enter into the clefts of the rocks, and into the fissures of the crags, —Because of the terribleness of Yahweh, And for his majestic splendour, When he ariseth to shake terribly the earth.
Watakimbilia kwenye mapango miambani na kwenye nyufa za miamba kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
22 Cease ye from the son of earth, In whose nostrils is but a breath, —For wherein to be reckoned upon, is he?
Acheni kumtumainia mwanadamu, ambaye hana kitu ila pumzi katika pua zake. Yeye ana thamani gani?

< Isaiah 2 >