< Isaiah 15 >

1 The oracle on Moab: Because, in a night, was laid waste Ar of Moab—destroyed! Because, in a night, was laid waste Kir of Moab—destroyed,
Neno kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!
2 He hath gone up to Bayith and Dibon, to the high places, to weep, —On Nebo and on Medeba, Moab is howling, On all their heads, a baldness, Every beard, clipped.
Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake, mpaka mahali pake pa juu ili walie, Moabu anaombolezea Nebo na Medeba. Kila kichwa kimenyolewa na kila ndevu limeondolewa.
3 In their streets, have they girded them with sackcloth, —On their housetops, and in their broadways, every one is howling—melting in tears;
Wamevaa nguo za magunia barabarani, juu ya mapaa na kwenye viwanja wote wanaomboleza, wamelala kifudifudi kwa kulia.
4 And Heshbon, hath made outcry, and Elealeh, Unto Jahaz, hath been heard their voice, —For this cause, do the armed men of Moab roar, Every man’s soul, quivereth to him.
Heshboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikika hadi Yahazi. Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele, nayo mioyo yao imezimia.
5 Mine own heart, for Moab continueth to make outcry, Her fugitive, as far as Zoar, is like a heifer of three years; For the accent of Luhith, with weeping, they ascend, For by the way of Horonaim—an outcry of destruction, they excite;
Moyo wangu unamlilia Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Soari, hadi Eglath-Shelishiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhithi, wanakwenda huku wanalia; barabarani iendayo Horonaimu wanaombolezea maangamizi yao.
6 For, the waters of Nimrim, shall become desolation, —For grass, hath dried up, Herbage hath failed, Green thing, hath not sprung up!
Maji ya Nimrimu yamekauka na majani yamenyauka; mimea imekauka wala hakuna kitu chochote kibichi kilichobaki.
7 For this cause, the savings they had made and that which they had stored, Over the torrent-bed of the willows, shall they bear them.
Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.
8 For the outcry hath gone round the boundary of Moab, —As far as Eglaim, the howling thereof, And to Beer-elim, the howling thereof.
Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu, kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu, maombolezo yao hadi Beer-Elimu.
9 For the waters of Dimon, are full of blood, For I will lay upon Dimon new troubles, —To the escaped of Moab, the lions, Even to the survivors on the soil.
Maji ya Dimoni yamejaa damu, lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni: simba juu ya wakimbizi wa Moabu na juu ya wale wanaobaki katika nchi.

< Isaiah 15 >