< Isaiah 10 >

1 Alas! for them who ordain iniquitous decrees, —And, busy writers, who make a business of writing mischief:
Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
2 Turning aside from judgment, the poor, And robbing, of justice, the oppressed of my people, —So that, widows, become, their spoil, And of the fatherless, they make prey.
kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
3 What, then, will ye do for the day of visitation, And for the devastation, which from afar, shall come? Unto whom, will ye flee for help? And where will ye leave your gory?
Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
4 Without me, one hath bowed under a prisoner Yea under the slain, do they fall! For all this, hath his anger, not turned back, But still, is his hand outstretched.
Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
5 Alas! for Assyria, the rod of mine anger, —Yea, the very staff in their hand, is, my displeasure:
“Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
6 Against an irreligious nation, will I send him, Yea against the people with whom I am wroth, will I command him, —To capture spoil And lay hold on prey, And cause them to be trodden down as the mire of the lanes.
Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
7 But as for him, not so, doth he deem, And in his heart, not so, doth he think, —For, to destroy, is in his heart, And to cut off nations, not a few;
Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
8 For he saith: —Are not, my generals, all alike, kings?
Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
9 Is not, Calno, like Carchemish? Is not, Hamath, like Arpad? Is not, Samaria, like Damascus?
Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
10 As my hand hath reached unto the kingdoms of idols, —whose images did excel them of Jerusalem and Samaria,
Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
11 Shall I not as I have done to Samaria and her idols, so, do to Jerusalem and her images?
je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
12 Wherefore it shall come to pass—When My Lord shall finish his whole work upon Mount Zion and upon Jerusalem, I will bring punishment—Upon the fruit of the greatness of heart of the king of Assyria. And upon the vainglory of his uplifted eyes,
Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
13 For he hath said—By the strength of mine own hand, have I effectually wrought, And by my wisdom—for I have discernment, —That I might remove the bounds of peoples, Yea their treasures, have I plundered That I might lay prostrate as a mighty one the inhabitants;
Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
14 And my hand hath found as a nest the wealth of the peoples, And as the gathering of eggs that are forsaken, all the earth, have, I, gathered, —And there was none to flap a wing, or open a mouth or chirp.
Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
15 Shall the axe boast itself against him that heweth therewith? Or, the saw, magnify itself, against him that wieldeth it? As if a rod, could wield, them who lift it up! As if a staff, could raise, what is, not wood!
Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
16 Therefore, shall the Lord, Yahweh of hosts, Send, among his fat ones, leanness, And under his glory, shall he kindle a kindling, like the kindling of fire;
Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
17 So shall, the Light of Israel, become, a fire, And his Holy One, a flame, Which shall burn and consume his thorns and his briars, in one day;
Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
18 And the glory of his forest and of his garden land, both soul and body, shall it bring to an end, —And it shall be like the wasting away of a consumptive.
Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
19 And, the remnant of his forest-trees, few in number, shall become, —yea, a child, might describe them!
Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
20 And it shall come to pass in that day, That the remnant of Israel. And the escaped of the house of Jacob Shall, no more again, lean upon him that smote them, —But shall lean upon Yahweh the Holy One of Israel, in truth.
Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
21 A remnant, shall return, The remnant of Jacob, —unto the mighty GOD;
Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
22 For though thy people, O Israel shall be as the sand of the sea, A [mere] remnant, shall return of them, —A full end decreed, bringeth in, justice, like a flood;
Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
23 For, a full end and that a decreed one, is My Lord Yahweh of hosts executing in the midst of all the earth.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
24 Therefore, thus, saith My Lord, Yahweh of hosts, Do not fear O my people dwelling in Zion, because of Assyria, —When with his rod, he would smite thee, And when his staff, he would lift up against thee in the manner of Egypt;
Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
25 For, yet a very little while, and displeasure shall end, Yea, mine anger, over their destruction.
Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
26 And Yahweh of hosts, will brandish over him, a scourge—Like the smiting of Midian at the rock Oreb, —And his staff being over the sea, He will lift it up in the manner of Egypt;
Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
27 And it shall come to pass, in that day, That his burden shall remove from off thy shoulder, And his yoke from off thy neck, —Yea, the yoke shall be broken because of fatness.
Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
28 He hath come in unto Ayyath, Hath passed through Migron, —At Michmash, storeth his baggage:
Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
29 They have passed over the pass, Geba is his halting-place, —Terror-stricken is Ramah, Gibeah of Saul, hath fled!
Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
30 Make shrill thy voice, O daughter of Gallim! Hearken, O Laishah, Answer, O Anathoth!
Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
31 Madmenah, hath fled, —The inhabitants of Gebim, have gone into safety:
Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
32 While yet to-day, in Nob, he tarrieth, He brandisheth his hand toward The mount of the daughter of Zion, The hill of Jerusalem.
Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
33 Behold! the Lord, Yahweh of hosts, is about to lop off a tree-crown, with a crash, —Then shall, they who are lifted on high, be hewn down, And, the lofty, be laid low;
Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
34 Then will he fell the thickets of the forest with iron, —And, Lebanon by a majestic one shall fall.
Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.

< Isaiah 10 >