< Hosea 7 >

1 When I would have brought healing to Israel, then was disclosed the iniquity of Ephraim, and the wicked doings of Samaria, for they have wrought falsehood, —when, a thief, would enter, a band roamed about, outside,
kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wevi huvunja nyumba, maharamia hunyangʼanya barabarani,
2 And they say not to their own hearts, that, all their wickedness, I remember, now, have their doings, beset them about, right before my face, have they been done.
lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.
3 By their wickedness, they gladden a king, and, by their flatteries, —rulers.
“Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.
4 They all, are adulterers, like an oven too hot for the baker, —who leaveth off stoking, after kneading the dough, till the whole be leavened.
Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.
5 In the day of our king, the rulers, have made themselves ill, with the heat of wine, —he hath extended his hand with scoffers.
Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.
6 For they have made ready, like an oven, their heart, by their lying in wait, —all the night, their baker sleepeth, in the morning, he, kindleth up as it were a blazing fire.
Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.
7 They all, become hot as an oven, and devour their judges, —all their kings, have fallen, there hath been none among them crying unto me.
Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
8 As for Ephraim! with the peoples, hath he been mingling himself, —Ephraim, is a cake not turned.
“Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
9 Foreigners have, eaten up, his strength, and, he, knoweth it not, —even gray hairs, are sprinkled upon him, and, he, knoweth it not.
Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.
10 Therefore doth the Excellency of Israel, answer, to his face; yet have they not returned unto Yahweh their God, nor have they sought him, in spite of all this!
Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Bwana Mungu wake wala kumtafuta.
11 So then, Ephraim, hath become, like a simple dove, having no understanding, on Egypt, have they called, to Assyria, have they gone,
“Efraimu ni kama hua, hudanganywa kwa urahisi na hana akili: mara anaita Misri, mara anageukia Ashuru.
12 Whithersoever they go, I will spread over them my net, like a bird of the heavens, will I bring them down, I will chastise them, by the time the report can reach the flock of them.
Wakati watakapokwenda, nitatupa wavu wangu juu yao; nitawavuta chini waanguke kama ndege wa angani. Nitakaposikia wakikusanyika pamoja, nitawanasa.
13 Woe to them! for they have taken flight from me, destruction to them! for they have transgressed against me, —when, I, would have ransomed them, then, they, spake—concerning me—falsehoods.
Ole wao, kwa sababu wamepotoka kutoka kwangu! Maangamizi ni yao kwa sababu wameniasi! Ninatamani kuwakomboa, lakini wanasema uongo dhidi yangu.
14 Neither made they outcry unto me, in their heart, although they kept on howling upon their beds, over corn and new wine, they gathered themselves together, they rebelled against me.
Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao, bali wanaomboleza vitandani mwao. Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya, lakini hugeukia mbali nami.
15 When, I, had warned them, I strengthened their arm, —yet, against me, kept they on devising wickedness.
Niliwafundisha na kuwatia nguvu, lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
16 They would return—not to him who is on high! They have become like a deceitful bow, their rulers, shall fall by the sword, for the rage of their tongue, this, [shall be] their derision in the land of Egypt.
Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana, wako kama upinde wenye kasoro. Viongozi wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya maneno yao ya jeuri. Kwa ajili ya hili watadhihakiwa katika nchi ya Misri.

< Hosea 7 >