< Hebrews 11 >

1 But faith is, of things hoped for, a confidence, of facts, a conviction, when they are not seen;
Kuwa na imani ni kuwa na hakika ya mambo tunayotumainia; kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona.
2 For, thereby, well-attested were the ancients.
Maana wazee wa kale walipata kibali cha Mungu kwa sababu ya imani yao.
3 By faith, we understand the ages to have been fitted together, by declaration of God, —to the end that, not out of things appearing, should that which is seen, have come into existence. (aiōn g165)
Kwa imani sisi tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu; vitu vinavyoonekana kutoka vitu visivyoonekana. (aiōn g165)
4 By faith, a fuller sacrifice, did Abel, offer unto God, than Cain, —through which, he received witness that he was righteous, there being a witnessing upon his gifts, by God; and, through it, though he died, he yet is speaking.
Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu iliyokuwa bora zaidi kuliko ile ya Kaini. Kwa imani yake alikubaliwa na Mungu kuwa mwadilifu; Mungu mwenyewe alizikubali sadaka zake. Kwa imani yake ingawa amekufa, bado ananena.
5 By faith, Enoch was translated, so as not to see death, and was not found, because that, God, had translated him; for, before the translation, he had received witness that he had become well-pleasing unto God; —
Kwa imani Henoki alichukuliwa na Mungu, asipate kufa. Hakuonekana tena kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Maandiko yasema kwamba kabla ya kuchukuliwa kwake, yeye alikuwa amempendeza Mungu.
6 But, apart from faith, it is impossible to be well-pleasing; for he that approacheth unto God—must needs have faith, that he is, and that, to them who seek him out, a rewarder he becometh.
Basi, pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Kwa maana kila mtu anayemwendea Mungu ni lazima aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba huwatuza wale wanaomtafuta.
7 By faith, Noah, having received intimation concerning the things not yet seen, filled with reverence, prepared an ark to the saving of his house—through which he condemned the world, and, of the righteousness by way of faith, became heir.
Kwa imani Noa alionywa na Mungu juu ya mambo ya baadaye ambayo hakuweza kuyaona bado. Alimtii Mungu, akajenga ile safina ambamo aliokolewa yeye pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo ulimwengu ulihukumiwa, naye Noa akapokea uadilifu unaotokana na imani.
8 By faith, being called, Abraham obeyed—to come forth into a place he was destined to receive for an inheritance; and he came forth, not well knowing whither he was coming.
Kwa imani Abrahamu alimtii Mungu alipoitwa aende katika nchi ambayo Mungu angempa iwe yake. Ingawa hakujua alikokuwa anakwenda, Abrahamu alihama.
9 By faith, he sojourned in the land of promise, as a foreign land, in tents, dwelling, along with Isaac and Jacob, the joint-heirs of the same promise;
Kwa imani aliishi kama mgeni katika nchi aliyoahidiwa na Mungu. Aliishi huko katika hema kama walivyoishi Isaka na Yakobo, ambao pia walishiriki ahadi ileile.
10 For he was awaiting the city having foundations, whose architect and builder is, God.
Maana Abrahamu alikuwa akingojea mji wenye misingi imara, mji ambao Mungu mwenyewe ndiye fundi aliyeubuni na kuujenga.
11 By faith, even Sarah herself, received power for founding a seed, even beyond the season of life’s prime, —seeing that, faithful, she reckoned, him that had promised;
Kwa imani hata Sara aliamini kwamba Mungu hutimiza ahadi zake, kwa hiyo akajaliwa kuchukua mimba ingawaje alikuwa amepita umri.
12 Wherefore, even from one, were born, and, as to these things, one who had become dead, —like the stars of the heaven, for multitude, and as the sand that is by the lip of the sea, that cannot be numbered.
Kwa hiyo, kutoka katika mtu huyo mmoja, Abrahamu, ambaye alikuwa kama amekufa, walitokea watu wengi wasiohesabika kama vile nyota za mbinguni na mchanga wa pwani.
13 In faith, all these died—not bearing away the promises, but, from afar, beholding and saluting them, and confessing that, strangers and sojourners, were they upon the land.
Watu hawa wote walikufa wakiwa na imani. Walikufa kabla ya kupokea mambo ambayo Mungu alikuwa ameahidi, lakini kwa mbali waliyaona, wakashangilia, na kukiri wazi kwamba wao walikuwa wageni na wakimbizi duniani.
14 For, they who such things as these are saying, make it clear that, of a paternal home they are in quest;
Watu wanaosema mambo kama hayo, huonyesha wazi kwamba wanaitafuta nchi yao wenyewe.
15 And, if indeed of that they had been mindful, from which they had come out, they might, in that case, have had an opportunity, to return;
Kama wangalikuwa wanaifikiria nchi walikotoka zamani, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
16 But, now, after a better one, are they reaching, that is, a heavenly; wherefore God is not ashamed of them, to be invoked as, their God, —for he hath prepared for them, a city.
Lakini sasa wanataka nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Ndiyo maana Mungu haoni haya wakimwita yeye Mungu wao, kwa sababu yeye mwenyewe amekwisha watayarishia mji.
17 By faith, Abraham, when tested, offered up Isaac, and, the only-begotten, would he have offered up, who the promises had accepted, —
Kwa imani, Abrahamu alimtoa mwanae Isaka sadaka wakati Mungu alipomjaribu. Huyo Abrahamu ndiye aliyekuwa amepokea ahadi ya Mungu, lakini, hata hivyo, alikubali kumtoa dhabihu mwanae wa pekee,
18 Even him of whom it had been said—In Isaac, shall there be called to thee, a seed:
ingawa Mungu alikuwa amemwambia: “Wazawa wako watatokana na Isaka.”
19 Accounting that, even from among the dead, God, was able, to raise [him], —whence, even in similitude, he bare him away.
Abrahamu aliamini kwamba Mungu anaweza kuwafufua wafu: na kwa namna fulani kweli Abrahamu alimpata tena mwanae kutoka wafu.
20 By faith, even concerning things to come, did Isaac bless Jacob and Esau.
Kwa imani Isaka aliwabariki Yakobo na Esau, wapate baraka zitakazokuja baadaye.
21 By faith, Jacob, when about to die, blessed each of the sons of Joseph; and bowed in worship on the top of his staff.
Kwa imani Yakobo alipokuwa karibu kufa, aliwabariki kila mmoja wa wana wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiegemea ile fimbo yake.
22 By faith, Joseph, when drawing to his end—concerning the exodus of the sons of Israel, called to remembrance, and, concerning his bones, gave commandment.
Kwa imani Yosefu alipokuwa karibu kufa, alinena juu ya kutoka kwa Waisraeli katika nchi ya Misri, na pia akawaachia maagizo kuhusu mifupa yake.
23 By faith, Moses, when born—was hid three months by his parents, because, they saw, that, goodly, was, the child, and were not affrighted, at the decree of the king.
Kwa imani wazazi wa Mose walimficha huyo mtoto kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuzaliwa kwake. Walimwona kuwa ni mtoto mzuri, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
24 By faith, Moses, when grown up—refused to be called the son of a daughter of a Pharaoh,
Kwa imani Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
25 Rather choosing—to be jointly suffering ill-treatment with the people of God, than, for a season, to be having, sins enjoyment;
Aliona ni afadhali kuteseka pamoja na watu wa Mungu kuliko kufurahia raha ya dhambi kwa kitambo kidogo.
26 Accounting—as greater riches than Egypt’s treasures, the reproach of the Anointed One; for he was looking away unto the recompense.
Alitambua kwamba kuteseka kwa ajili ya Masiha kuna faida kubwa zaidi kuliko utajiri wote wa nchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia tuzo la baadaye.
27 By faith, he forsook Egypt—not put in fear of the wrath of the king; for, as seeing him who cannot be seen, he persevered.
Kwa imani Mose alihama kutoka nchi ya Misri bila kuogopa hasira ya mfalme; na wala hakurudi nyuma, kwani alikuwa kama mtu aliyemwona yule Mungu asiyeonekana.
28 By faith, he hath kept the passover and the besmearing of the blood, lest, he that was destroying the first-born, should be touching them.
Kwa imani aliadhimisha siku ya Pasaka, akaamuru damu inyunyizwe juu ya milango, ili yule Malaika Mwangamizi asiwaue wazaliwa wa kwanza wa Israeli.
29 By faith, they passed through the Red Sea, as over dry land, —which the Egyptians, seizing an attempt to do, were swallowed up.
Kwa imani watu wa Israeli walivuka bahari ya Shamu, kana kwamba ilikuwa nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo walikufa maji.
30 By faith, the walls of Jericho, fell, having been surrounded for seven days.
Kwa imani kuta za mji wa Yeriko zilianguka watu wa Israeli walipokwisha zunguka kwa muda wa siku saba.
31 By faith, Rahab the harlot perished not with them who refused to yield, she having welcomed the spies with peace.
Kwa imani Rahabu aliyekuwa malaya hakuangamia pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa sababu aliwakaribisha wale wapelelezi.
32 And what more can I say? For, time, will fail me while I go on telling—concerning Gideon, Barak, Sampson, Jephthah, David also, and Samuel, and the prophets, —
Basi, niseme nini zaidi? Wakati hauniruhusu kueleza juu ya Gedeoni, Baraki, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii.
33 Who, through faith—prevailed in contest over kingdoms, wrought righteousness, attained unto promises, shut the mouths of lions,
Kwa imani hawa wote walipigana vita na wafalme, wakashinda. Walitenda mambo adili, wakapokea yale aliyoahidi Mungu. Walifunga vinywa vya simba,
34 Quenched the power of fire, escaped the mouths of the sword, were made powerful from weakness, became mighty in battle, overturned, camps of aliens;
Walizima mioto mikali, waliepuka kuuawa kwa upanga. Walikuwa dhaifu lakini walipata nguvu. Walikuwa hodari katika vita wakashinda majeshi ya kigeni.
35 Women received, by resurrection, their dead; but, others, were put to the rack, not accepting redemption, that, unto a better resurrection, they might attain:
Na, wanawake walioamini walirudishiwa wafu wao wakiwa wamefufuliwa. Baadhi yao walikataa kufunguliwa, wakateswa mpaka kufa ili wapate kufufuliwa na kuingia katika maisha bora zaidi.
36 Others, again, of mockings and scourgings, received trial, nay! further, of bonds and imprisonments:
Wengine walidhihakiwa na kupigwa mijeledi, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa gerezani.
37 They were stoned, were pierced through, were sawn asunder, by murder, with a sword, died, went about in sheep-skins, in goat-hides, —being in want, suffering tribulation, enduring ill-treatment:
Walipigwa mawe, walipasuliwa vipandevipande, waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi, walikuwa watu maskini, walioteswa na kudhulumiwa.
38 Of whom the world, was not worthy—upon deserts, wandering, and mountains, and in caves, —and in the caverns of the earth.
Ulimwengu haukustahili kuwa na watu hao. Walitangatanga jangwani na mlimani, wakaishi katika mashimo na mapango ya ardhi.
39 And, these all, though they obtained witness through their faith, yet bare not away, the promise:
Watu hawa wote walionekana kuwa mashujaa kwa sababu ya imani yao. Hata hivyo, hawakupokea yale ambayo Mungu aliwaahidia,
40 God, for us, something better providing, —that, not apart from us, should they be made, perfect.
maana Mungu alikuwa ameazimia mpango ulio bora zaidi kwa ajili yetu; yaani wao wangeufikia ukamilifu wakiwa pamoja nasi.

< Hebrews 11 >