< Hebrews 1 >

1 Whereas, in many parts and in many ways of old, God spake unto the fathers, in the prophets,
Hapo zamani, Mungu alisema na babu zetu mara nyingi kwa namna nyingi kwa njia ya manabii,
2 At the end of these days, He hath spoken unto us in his Son, —whom he hath appointed heir of all things, through whom also he hath made the ages; (aiōn g165)
lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu na akamteua avimiliki vitu vyote. (aiōn g165)
3 Who, being an eradiated brightness of his glory, and an exact representation of his very being, also bearing up all things by the utterance of his power, purification of sins, having achieved, sat down on the right hand of the majesty in high places:
Yeye ni mng'ao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe, akiutegemeza ulimwengu kwa neno lake lenye nguvu. Baada ya kuwapatia binadamu msamaha wa dhambi zao, aliketi huko juu mbinguni, upande wa kulia wa Mungu Mkuu.
4 By so much becoming superior to the messengers, by as much as, going beyond them, he hath inherited a more distinguished name.
Mwana ni mkuu zaidi kuliko malaika, kama vile jina alilopewa na Mungu ni kuu zaidi kuliko jina lao.
5 For unto which of the messengers said he at any time—My Son, art, thou, I, this day have begotten thee? and again—I, will become, his father, and, he, shall become my Son?
Maana Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Wewe ni Mwanangu; Mimi leo nimekuwa Baba yako.” Wala hakusema juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu.”
6 But, whensoever he again introduceth the first-begotten into the habitable earth, he saith—And let all God’s messengers worship him!
Lakini Mungu alipokuwa anamtuma Mwanae mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, alisema: “Malaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu.”
7 Even as to the messengers, indeed, he saith—Who maketh his messengers, winds, and his ministers of state, a fiery flame;
Lakini kuhusu malaika, Mungu alisema: “Mungu awafanya malaika wake kuwa pepo, na watumishi wake kuwa ndimi za moto.”
8 but, as to the Son, —Thy throne, O God, is unto times age-abiding, and—A sceptre of equity, is the sceptre of his kingdom, (aiōn g165)
Lakini kumhusu Mwana, Mungu alisema: “Utawala wako ee Mungu, wadumu milele na milele! Wewe wawatawala watu wako kwa haki. (aiōn g165)
9 Thou hast loved righteousness, and hated lawlessness, —For this cause, hath God, thy God, anointed thee with the oil of exultation, beyond thy partners;
Wewe wapenda uadilifu na kuchukia uovu. Ndiyo maana Mungu, Mungu wako amekuweka wakfu na kukumiminia furaha kubwa zaidi kuliko wenzako.”
10 and—Thou, by way of beginning, Lord, the earth, didst found, and, the works of thy hands, are the heavens, —
Pia alisema: “Bwana, wewe uliumba dunia hapo mwanzo, mbingu ni kazi ya mikono yako.
11 They, shall perish, but, thou, abidest still, and, all, as a mantle, shall be worn out,
Hizo zitatoweka, lakini wewe wabaki daima, zote zitachakaa kama vazi.
12 And, as if a robe, wilt thou fold them up, —as a mantle, and they shall be changed; but, thou, art the same, and thy years shall not fail.
Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilishwa kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule daima, na maisha yako hayatakoma.”
13 But, to which of the messengers, hath he said, at any time—Sit thou at my right hand, until I make thy foes thy footstool?
Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako.”
14 Are they not, all, spirits, doing public service, —for ministry, sent forth, for the sake of them who are about to inherit salvation?
Malaika ni roho tu wanaomtumikia Mungu, na Mungu huwatuma wawasaidie wale watakaopokea wokovu.

< Hebrews 1 >