< Haggai 1 >

1 In the second year of Darius the king, in the sixth month, on the first of the month, came the word of Yahweh, by the hand of Haggai the prophet, unto Zerubbabel son of Shealtiel, pasha of Judah, and unto Jehoshua son of Jehozadak the high priest, saying:
Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:
2 Thus, speaketh Yahweh of hosts, saying, —This people, have said, Not yet hath come the time for the house of Yahweh to be built.
Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’”
3 Therefore hath come the word of Yahweh by the hand of Haggai the prophet, saying:
Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai:
4 Is it a time that, ye yourselves, should be dwelling in your own paneled houses? and, this house, be in ruins?
“Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”
5 Now, therefore, Thus, saith Yahweh of hosts, —Apply your heart unto your own experience—
Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
6 Ye have sown much, but have brought in little, have eaten, and not been filled, have drunk, and not been satisfied with drink, have clothed you, and none hath been warm, —and, he that hath hired himself out, hath put his wages into a bag with holes.
Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”
7 Thus, saith Yahweh of hosts, —Apply your heart to your own experience:
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
8 Ascend the mountain—and bring in wood and build the house, —that I may be pleased therewith and get myself glory, saith Yahweh.
Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana.
9 When ye looked for much, then lo! it came to little, when ye brought it home, then I did blow into it, — Because of what? Demandeth Yahweh of hosts, Because of my house, the which is in ruins, while ye keep running every man to his own house.
“Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.
10 Wherefore—on your account, have the heavens, held back, dew, — and, the earth, held back her fruit;
Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.
11 And I have called for drought, upon the land and upon the mountains, and upon the corn and upon the new wine and upon the oil, and upon that which the ground, bringeth forth, —and upon man, and upon beast, and upon all the labour of the hands.
Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”
12 Then hearkened Zerubbabel son of Shealtiel, and Jehoshua son of Jehozadak the high priest, and all the remnant of the people, unto the voice of Yahweh their God, and unto the words of Haggai the prophet, as Yahweh their God, had sent him, —and the people, stood in awe, before Yahweh.
Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.
13 Then spake Haggai the messenger of Yahweh, in the message of Yahweh, to the people saying, —I, am with you, Declareth Yahweh.
Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana.
14 Thus did Yahweh, stir up—the spirit of Zerubbabel son of Shealtiel, pasha of Judah, and the spirit of Jehoshua son of Jehozadak the high priest, and the spirit of all the remnant of the people, —and they came in and did service in the house of Yahweh of hosts their God:
Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao,
15 on the twenty-fourth day of the month, in the sixth month, —in the second year of Darius the king.
katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.

< Haggai 1 >