< Genesis 45 >

1 And Joseph could not restrain himself before all who were stationed near him, so he cried out—Have forth every man from me! And there stood no man with him, when Joseph made himself known unto his brethren,
Hapo Yosefu hakuweza kujizuia zaidi mbele ya wote waliokuwa wamesimama karibu naye, akapaza sauti, akasema, “Mwondoeni kila mtu mbele yangu!” Kwa hiyo hapakuwepo mtu yeyote pamoja na Yosefu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
2 Then gave he forth his voice in weeping, —and the Egyptians heard, and the house of Pharaoh heard.
Naye akalia kwa sauti kubwa kiasi kwamba Wamisri walimsikia, hata watu wa nyumbani mwa Farao wakapata hizo habari.
3 Then said Joseph unto his brethren: I, am Joseph, is my father yet alive? But his brethren could not answer him, for they were terrified because of him.
Yosefu akawaambia ndugu zake, “Mimi ni Yosefu! Je, baba yangu angali hai bado?” Lakini ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwa sababu walipatwa na hofu kuu mbele yake.
4 Then said Joseph unto his brethren—Draw near I pray you, unto me. And they drew near. And he said—I, am Joseph your brother, whom ye sold into Egypt.
Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake, “Sogeeni karibu nami.” Waliposogea, akasema, “Mimi ni ndugu yenu Yosefu, yule ambaye mlimuuza Misri!
5 But, now, do not grieve, neither let it be vexing in your eyes, that ye sold me hither, —for, to save life, did God send me before you.
Sasa, msihuzunike wala msijichukie wenyewe kwa kuniuza huku, kwa sababu ilikuwa ni ili kuokoa maisha ya watu ndiyo sababu Mungu alinituma niwatangulie ninyi.
6 For these two years, hath the famine been in the midst of the land, —and, yet five years, are there, in which there shall be neither ploughing, nor harvest.
Kwa miaka miwili sasa imekuwepo njaa katika nchi, pia kwa miaka mitano ijayo hapatakuwepo kulima wala kuvuna.
7 So then God sent me before you, to plant for you a remainder in the earth, —and to save you alive, by a great deliverance,
Lakini Mungu alinitanguliza mbele yenu ili kuhifadhi mabaki kwa ajili yenu katika nchi, na kuokoa maisha yenu kwa wokovu mkuu.
8 Now, therefore it was not ye, who sent me hither, but, God, himself, —who also appointed me to be a father to Pharaoh, and a lord to all his house, and a ruler over all the land of Egypt.
“Kwa hiyo basi, si ninyi mlionileta huku, bali ni Mungu. Alinifanya kuwa baba kwa Farao, bwana wa watu wa nyumbani mwake wote, na mtawala wa Misri yote.
9 Haste ye and go up unto my father, then shall ye say unto him—Thus saith thy son Joseph, God hath appointed me lord to all Egypt, —come down unto me do not delay;
Sasa rudini haraka kwa baba yangu na mwambieni, ‘Hili ndilo mwanao Yosefu asemalo: Mungu amenifanya mimi kuwa bwana wa Misri yote. Shuka uje kwangu, wala usikawie.
10 so shalt thou dwell in the land of Goshen, and shalt be near unto me, thou, and thy sons, and thy sons’ sons, —and thy flocks and thy herds and all that is thine;
Nawe utaishi katika nchi ya Gosheni na kuwa karibu nami, wewe, watoto wako na wajukuu wako, makundi yako ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na vyote ulivyo navyo.
11 so will I sustain thee, there, for there are yet five years of famine, —lest thou come to poverty—thou and thy house and all who are thine.
Nitawatunza huko, kwa sababu bado iko miaka mingine mitano inayokuja ya njaa. La sivyo, wewe na nyumba yako na wote ulio nao mtakuwa fukara.’
12 Now lo! your own eyes do see, and the eyes of my brother Benjamin, —that it is my own mouth, that doth speak unto you.
“Mnaweza kujionea wenyewe, hata ndugu yangu Benyamini, kwamba hakika ni mimi ninayezungumza nanyi.
13 As soon as ye have told my father all my honour in Egypt, and all that ye have seen, so soon shall ye hasten and bring down my father hither.
Mwambieni baba yangu juu ya heshima yote niliyopewa huku Misri, na kuhusu kila kitu mlichokiona. Mleteni baba yangu huku haraka.”
14 Then fell he upon the neck of Benjamin his brother, and wept, —and Benjamin wept on his neck.
Ndipo akamkumbatia Benyamini ndugu yake na kulia, naye Benyamini akamkumbatia akilia.
15 Then kissed he all his brethren, and wept upon them, —and, thereafter, his brethren spake with him.
Pia akawabusu ndugu zake wote, huku akilia. Baada ya hayo ndugu zake wakazungumza naye.
16 Now, the report, was heard by the house of Pharaoh, saying, The brethren of Joseph have come in, And it was good in the eyes of Pharaoh, and in the eyes of all his servants.
Habari zilipofika kwenye jumba la Farao kwamba ndugu zake Yosefu wamefika, Farao na maafisa wake wote wakafurahi.
17 So then Pharaoh said unto Joseph—Say unto thy brethren This, do, —lade your asses, and go enter into the land of Canaan;
Farao akamwambia Yosefu, “Waambie ndugu zako, ‘Fanyeni hivi: Pakieni wanyama wenu mrudi mpaka nchi ya Kanaani,
18 and fetch your father and your households and come in unto me, —that I may give you the best of the land of Egypt, and eat ye the fat of the land.
mkamlete baba yenu na jamaa zenu kwangu. Nitawapa sehemu nzuri sana ya nchi ya Misri nanyi mtafurahia unono wa nchi.’
19 Thou, therefore command them, This, do ye, —Take you out of the land of Egypt, waggons for your little ones and for your wives, so shall ye bring your father and come in.
“Mnaagizwa pia kuwaambia, ‘Fanyeni hivi: Chukueni magari ya kukokotwa kutoka Misri, kwa ajili ya watoto wenu na wake zenu, mkamchukue baba yenu mje.
20 Your eye, moreover, let it not look with pity upon your goods, —for, the best of all the land of Egypt, is, yours.
Msijali kamwe kuhusu mali zenu, kwa sababu mema yote ya Misri yatakuwa yenu.’”
21 And the sons of Israel did so, and Joseph gave them waggons, at the bidding of Pharaoh, —and gave them provisions for the way:
Hivyo wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yosefu akawapa magari ya kukokotwa, kama Farao alivyoagiza, pia akawapa mahitaji kwa ajili ya safari yao.
22 to all of them, gave he to each man changes of raiment, —but, to Benjamin, he gave three hundred pieces of silver, and five changes of raiment.
Kila mmoja mavazi mapya, lakini Benyamini akampa shekeli 300 za fedha, na jozi tano za nguo.
23 Moreover, to his father, sent he as followeth—ten he-asses, laden from the best of Egypt, —and ten she-asses laden with corn and bread and nourishing food for his father for the way.
Hivi ndivyo vitu alivyotuma kwa baba yake: punda kumi waliochukua vitu vizuri vya Misri, punda wake kumi waliobeba nafaka, mikate na mahitaji mengine ya safari.
24 Thus sent he forth his brethren and they departed, —and he said unto them, Do not fall out by the way.
Akaagana na ndugu zake walipokuwa wakiondoka, akawaambia, “Msigombane njiani!”
25 And they went up out of Egypt, —and came into the land of Canaan, unto Jacob their father.
Basi wakatoka Misri na kufika kwa baba yao Yakobo katika nchi ya Kanaani.
26 And they told him saying—Joseph: is, yet alive, yea, indeed, he, is ruler in all the land of Egypt. And his heart became faint, for he believed them not.
Wakamwambia baba yao, “Yosefu angali hai! Ukweli ni kwamba yeye ndiye mtawala wa Misri yote.” Yakobo akapigwa na bumbuazi; hakuwasadiki.
27 So they spake unto him all the words of Joseph which he had spoken unto them h then saw he the waggons, which Joseph had sent to carry him, —and the spirit of Jacob their father revived.
Lakini walipokwisha kumweleza kila kitu ambacho Yosefu alikuwa amewaambia, na alipoona magari ya kukokotwa Yosefu aliyokuwa amempelekea ya kumchukua aende Misri, roho ya baba yao Yakobo ikahuishwa.
28 And Israel said, Enough! Joseph my son is, yet alive, I must go and see him before I die!
Ndipo Israeli akasema, “Nimesadiki! Mwanangu Yosefu bado yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”

< Genesis 45 >