< Genesis 39 >

1 Now, Joseph, was taken down to Egypt, —and Potiphar, courtier of Pharaoh, chief of the royal executioners, an Egyptian bought him, at the hand of the Ishmaelites, who had brought him down thither.
Yusufu akaletwa Misri. Potifa, aliyekuwa afisa wa Farao mkuu wa walinzi na Mmisri, akamnunua kutoka kwa Waishmaeli, waliokuwa wamempeleka pale.
2 And it came to pass that Yahweh, was with Joseph, so that he became a prosperous man, —and was in the house of his lord the Egyptian.
Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu na akawa mtu aliyefanikiwa. Aliishi katika nyumba ya Mmisri bwana wake.
3 And his lord saw, that, Yahweh, was with him—and that whatsoever, he was doing, Yahweh, was causing to prosper in his hand.
Bwana wake akaona kwamba Yahwe alikuwa pamoja naye na kwamba Yahwe alifanikisha kila kitu alichokifanya.
4 So Joseph found favour in his eyes and waited upon him, —and he made him overseer over his house, and all that he had, gave he into his hand.
Yusufu akapata kibali mbele zake. Akamtumikia Potifa. Potifa akamfanya msimamizi juu ya nyumba yake, na kila alichokimiliki, akakiweka chini ya uangalizi wake.
5 And it came to pass from the time that he made him overseer in his house and over all that he had, that Yahweh blessed the house of the Egyptian, for Joseph’s sake, —yea it came to pass, that the blessing of Yahweh, was with all that he had, in the house and in the field;
Ikawa alipomfanya msimamizi juu ya nyumba yake na juu ya kila kitu alichomiliki, Yahwe akaibariki nyumba ya Mmisri kwa sababu ya Yusufu. Baraka za Yahwe zilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa nyumbani na shambani.
6 so that he left all that he had in the hand of Joseph, and took note with him of nothing, save only the bread which, he himself, was eating. And so it was that Joseph was comely in form and comely in countenance.
Potifa akaweka kila alichokuwa nacho chini ya uangalizi wa Yusufu. Hakuwa na haja ya kufikiri juu ya lolote isipokuwa chakula alichokula tu. Basi Yusufu alikuwa kijana mzuri na wa kuvutia.
7 And it came to pass after these things, that his lord’s wife lifted up her eyes unto Joseph, —and she said—Come! lie with me.
Ikawa baada ya hayo mke wa bwana wake akamtamani Yusufu. Akamwambia, “Lala nami.”
8 And he refused and said unto his lord’s wife, Lo! my lord, taketh no note with me as to what is in the house, —but, all that pertaineth to him, hath he delivered into my hand:
Lakini yeye alikataa na kumwambia mke wa bwana wake, “Tazama, bwana wangu haangalii chochote nikifanyacho nyumbani, na ameweka kila kitu anachokimiliki chini ya uangalizi wangu.
9 There is no one greater in this house than I, neither hath he withheld from me anything, save only thyself in that thou, art his wife, —how, then could I do this great wickedness, and sin against God?
Hakuna mtu aliye mkuu katika nyumba hii kuliko mimi. Hajanidhuiria chochote isipokuwa wewe, kwa sababu wewe ni mkewe. Ni kwa namna gani basi naweza kufanya uovu mkuu namna hii na kumtenda dhambi Mungu?
10 And it came to pass, that although she Spake unto Joseph day after day, yet hearkened he not unto her to lie beside her to be with her.
Akamwambia Yusufu siku baada ya siku, lakini yeye akakataa kulala naye wala kuwa naye.
11 And it came to pass, when, on a certain day, he went into the house to attend to his business, —and there was no man of the household, there in the house,
Ikawa siku moja aliingia ndani kufanya kazi yake. Hakuna mtu yeyote wa nyumbani aliyekuwepo pale ndani.
12 that she caught him by his garment, saying—Come! lie with me. Then left he his garment in her hand, and fled and gat forth outside,
Akashika nguo zake na kusema, “Lala nami.” Akaacha nguo zake mikononi mwake, akakimbia, na kutoka nje.
13 And it came to pass when she saw that he had left his garment in her hand, —and fled forth outside,
Ikawa, alipoona kwamba ameziacha nguo zake mikononi mwake na kwamba amekimbia nje,
14 that she cried out to the men of her house and spake to them, saying, Look ye! he hath brought in to us a Hebrew man to insult us, —He came in unto me, to lie with me, so I cried out with a loud voice.
akawaita watu wa nyumbani mwake na kuwambia, “Tazama, Potifa ameleta Mwebrania huyu kutudhihaki. Aliingia kulala nami, na nikapiga kelele.
15 And it came to pass, when he heard that I lifted high my voice, and cried out, then left he his garment beside me, and fled and gat forth outside.
Ikawa aliponisikia nikipiga kelele, akaniacha na nguo yake, akakimbia, na kutoka nje.”
16 So she laid by his garment beside her, —until his lord should come into his house,
Akaweka nguo zake karibu naye hata bwana yake alipokuja nyumbani.
17 Then spake she unto him, according to these words, saying, —He hath been in unto me—the Hebrew servant whom thou didst bring in to us—to insult me.
Akamwambia maelelezo haya, “Yule mtumishi Mwebrania uliyemleta kwetu, aliingia kunidhihaki.
18 And it came to pass when I lifted high my voice and cried out, then left he his garment beside me, and fled outside.
Ikawa nilipopiga kelele, akaacha nguo yake kwangu akakimbia nje.”
19 And it came to pass, when his lord heard the words of his wife which she spake unto him saying, According to these words, hath thy servant done to me, Then was kindled his anger.
Ikawa, bwana wake aliposikia maelezo aliyoambiwa na mkewe, “Hivi ndivyo mtumishi wako alivyonitenda,” alikasirika sana.
20 So Joseph’s lord took him and delivered him up to the prison: the place where, the prisoners of the king, were imprisoned, —so he was there, in the prison.
Bwana wa Yusufu akamchukua na kumweka gerezani, mahali walipowekwa wafungwa wa mfalme. Akawa pale kifungoni.
21 And it came to pass that, Yahweh, was with Joseph, and extended unto him lovingkindness, —and gave him his favour in the eyes of the chief of the prison.
Lakini Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu na kumwonyesha uaminifu wa agano. Akampa kibali mbele ya mlinzi wa gereza.
22 So the chief of the prison delivered up, into Joseph’s hand all the prisoners who were in the prison, —and of all that was doing there, he, was the doer.
Mlinzi wa gereza akawaweka mikononi mwa Yusufu wafungwa wote waliokuwa gerezani. Chochote walichokifanya, kilikuwa chini ya uangalizi wa Yusufu.
23 After nothing, was the chief of the prison looking, of whatever was in his hand, —in that Yahweh, was with him, and whatsoever, he was doing, Yahweh, was causing to prosper.
Mlinzi wa gereza hakuwa na wasiwasi juu ya chochote kilichokuwa mkononi mwake, kwa sababu Yahwe alikuwa pamoja naye. Yahwe akafanikisha kila alichokifanya.

< Genesis 39 >