< Genesis 11 >

1 So it came to pass that, all the earth, was of one manner of speech, —and of one stock of words.
Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
2 And it came to pass as they brake away onwards, that they found a plain in the land of Shinar, and dwelt there.
Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
3 Then said they, each man to his friend, Come on! let us make bricks, and burn them thoroughly, —So the bricks, served them for stone, and bitumen, served them for mortar,
Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
4 And they said Come on! let us build for ourselves a city, and a tower with its head in the heavens, so let us make for ourselves a name, —lest we be scattered abroad over the face of all the earth.
Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
5 And Yahweh came down, to behold the city, and the tower, —which the sons of men had built.
Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
6 Then said Yahweh: Lo! one people and one manner of speech, have they all, this, then is what they have begun to do, —now, therefore, nothing will be withholden from them which they may plan to do.
Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
7 Come on! let us go down, and there confuse their speech, —that they may not understand, each man the speech of his friend.
Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
8 So Yahweh scattered them from thence over the face of all the earth, —and so they left off building the city.
Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
9 For this cause, was the name thereof called Babel ["Confusion"]; because there, did Yahweh confuse the speech of all the earth, —and, from thence, did Yahweh scatter them abroad, over the face of all the earth.
Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
10 These, are the genealogies of Shem, Shem was a hundred years old when he begat Arpachshad, two years after the flood
Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
11 and Shem lived after he begat Arpachshad, five hundred years, —and begat sons and daughters.
Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
12 And, Arpachshad, lived thirty-five years, —and begat Shelah;
Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
13 and Arpachshad lived after he begat Shelah, four hundred and three years, —and begat sons and daughters.
Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 And, Shelah, lived thirty years, —and begat Eber;
Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 and Shelah lived, after he begat Eber, four hundred and three years, —and begat sons and daughters.
Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
16 And Eber lived thirty-four years, —and begat Peleg;
Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 and Eber lived after he begat Peleg, four hundred and thirty years, —and begat sons and daughters.
Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
18 And Peleg lived thirty years, and begat Reu:
Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 and Peleg lived after he begat Reu, two hundred and nine years, —and begat sons and daughters.
Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 And Reu lived thirty-two years—and begat Serug;
Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
21 and Reu lived after he begat Serug, two hundred and seven years, —and begat sons and daughters.
Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
22 And Serug lived thirty years, —and begat Nahor;
Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 and Serug lived after he begat Nahor, two hundred years, —and begat sons and daughters.
Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
24 And Nahor lived twenty-nine years, —and begat Terah;
Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 and Nahor lived, after he begat Terah, a hundred and nineteen years, —and begat sons and daughters.
Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
26 And Terah lived seventy years, —and begat Abram, Nahor, and Haran.
Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
27 These, then are the generations of Terah, Terah begat Abram, Nahor, and Haran, —and, Haran, begat Lot;
Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
28 and Haran died, in the presence of Terah his father, —in the land of his birth, in Ur of the Chaldees.
Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
29 And Abram and Nahor took to themselves wives; the name of Abram’s wife, was Sarai; and, the name of Nahor’s wife, Milcah, daughter of Haran father of Milcah, and father of Iscah.
Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
30 And, Sarai, remained barren, —she had no child,
Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
31 And Terah took Abram his son and Lot son of Haran his son’s son, and Sarai his daughter-in-law, wife of Abram his son, —and came forth with them out of Ur of the Chaldees, that they might go their way towards the land of Canaan, and they came in as far as Haran and dwelt there.
Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
32 And the days of Terah were two hundred and five years, —and Terah died in Haran.
Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.

< Genesis 11 >