< Ezekiel 24 >

1 And the word of Yahweh came unto me. in the ninth year in the tenth month, on the tenth of the month, saying:
Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Son of man. Write thee the name of the day, this selfsame day, —the king of Babylon cast himself against Jerusalem, on this selfsame day.
“Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo.
3 Put thou forth therefore, against the perverse house a parable, and say unto them Thus saith My Lord, Yahweh: Set on the caldron set it on, Moreover also pour into it water:
Iambie nyumba hii ya kuasi fumbo, na uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Teleka sufuria jikoni; iteleke na umimine maji ndani yake,
4 Gather the pieces thereof into it, Every good piece thigh and shoulder, With the choice of the bones, fill it:
Weka vipande vya nyama ndani yake, vipande vyote vizuri, vya paja na vya bega. Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri;
5 Take of the choice of the rock, Moreover also pile of bones place under it, - Boil the pieces thereof, Yea let the bones of it seethe in the midst thereof.
chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo. Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa; chochea mpaka ichemke na uitokose hiyo mifupa ndani yake.
6 Wherefore, Thus saith My Lord Yahweh, Woe! city of bloodshed. The caldron whose scum is in it, and whose scum, hath not gone out of it: Piece by piece, bring it out, There hath fallen thereon no lot.
“‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu, ole wa sufuria ambayo sasa ina ukoko ndani yake, ambayo ukoko wake hautoki. Kipakue kipande baada ya kipande, bila kuvipigia kura.
7 For, her own blood, hath come to be in her midst, Upon the smooth face of the cliff, hath she set it, - She hath not poured it out on the earth, that she might cover it with dust.
“‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake: huyo mwanamke aliimwaga juu ya mwamba ulio wazi; hakuimwaga kwenye ardhi, ambako vumbi lingeifunika.
8 To bring up indignation to execute an avenging, have I set her blood upon the smooth face of the cliff, —that it may not be covered.
Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi, nimemwaga damu yake juu ya mwamba ulio wazi, ili isifunikwe.
9 Wherefore Thus, saith My Lord Yahweh, Woe! city of bloodshed, —Even I myself, will make large the pile.
“‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu! Mimi nami nitalundikia kuni nyingi.
10 Heap on the wood Kindle the fire, Consume the flesh, Yea season with spice, And let the bones be scorched.
Kwa hiyo lundika kuni na uwashe moto. Pika hiyo nyama vizuri, changanya viungo ndani yake, na uiache mifupa iungue kwenye moto.
11 Then set it upon the live coals thereof empty, —that the copper of it may be scorched and burn. So that the impurity thereof may be annihilated within it The scum thereof be consumed,
Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaa mpaka iwe na moto sana na shaba yake ingʼae, ili uchafu wake upate kuyeyuka na ukoko wake upate kuungua na kuondoka.
12 With toils, hath she wearied herself, —Since her abundant scum will not go out of her, into the fire, with her scum!
Imezuia juhudi zote, ukoko wake mwingi haujaondoka, hata ikiwa ni kwa moto.
13 In thine uncleanness, is lewdness; be- cause I purified thee and thou wast not purified, from thine uncleanness, thou shalt not be purified any more, until I have let mine indignation rest upon thee.
“‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutoka kwenye huo uchafu wako, hutatakasika tena mpaka ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua.
14 I Yahweh, have spoken It cometh and I will perform I will not let alone, neither will I shield, Nor will I repent, - According to thy ways and according to thy doings, have they judged thee, Declareth My Lord Yahweh.
“‘Mimi Bwana nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu, Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema Bwana Mwenyezi.’”
15 And the word of Yahweh came unto me saying:
Neno la Bwana likanijia kusema:
16 Son of Man Behold me! taking away from thee the delight of thine eyes, with a stroke, - But thou shall not lament Neither shalt thou weep, Neither shall come—thy tears:
“Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote.
17 To groan, forbear, Over the dead—no mourning, shalt thou make Thy chaplet, bind thou on thee And thy sandals: , put thou on thy feet, And thou shalt not cover thy beard, And the bread of other men, shalt thou not eat.
Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya kawaida vya wakati wa matanga.”
18 So I spake unto the people in the morning, and my wife died in the evening, —and I did in the morning, as I had been commanded.
Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Asubuhi yake nilifanya kama nilivyoamriwa.
19 Then said the people unto me: Wilt thou not tell us what these things are to us, that thou shouldst be acting thus?
Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?”
20 So I said unto them: The word of Yahweh hath come unto me, saying:
Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
21 Say to the house of Israel thus, saith My Lord. Yahweh, Behold me! profaning my sanctuary. The pride of your strength, The delight of your eyes And the object of the tender regard of your soul, - And your sons and your daughters whom ye have left behind, by the sword, shall fall.
‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu na binti zenu mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga.
22 Then shall ye do, as I have done.— The beard, shall ye not cover, And the bread of other men: , shall ye not eat;
Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji.
23 And your chaplets shall be on your heads. And your sandals on your feet, Ye shall neither lament, nor weep, - Yet shall ye pine away in your iniquities, and shall groan one to another.
Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake.
24 So shall Ezekiel become to you a wonder, According to all that he hath done, shall ye do: When it cometh, then shall ye know that I am The Lord, Yahweh.
Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Wakati jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’
25 Thou, therefore Son of man, Shall it not be— In the day when I take away from them Their strength, The joy of their adorning, — The delight of their eyes And the desire of their soul, Their sons and their daughters
“Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao na binti zao vilevile,
26 That in that day, one that hath escaped shall come in unto thee, —to cause thee to hear it with thine own ears?
siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari.
27 That in that day, thy mouth shall be opened unto him that hath escaped, And thou shalt speak and not be dumb any longer? So shalt thou become to them a wonder, And they shall know that, I, am Yahweh.
Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”

< Ezekiel 24 >