< Exodus 37 >

1 And Bezaleel made the ark, of acacia wood, two cubits and a half, the length thereof and, a cubit and a half, the breadth thereof, and, a cubit and a half, the height thereof;
Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
2 and he overlaid it with pure gold within and without, -and made for it a rim of gold, round about;
Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
3 and he cast for it four rings of gold, upon the four feet thereof, —even, two rings, on the one side thereof and, two rings, on the other side thereof;
Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
4 and he made staves of acacia wood, and overlaid them with gold;
Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
5 and he brought the staves into the rings, upon the sides of the ark, for lifting the ark.
Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
6 And he made a propitiatory of pure gold, —two cubits and a half, the length thereof, and, a cubit and a half, the breadth thereof:
Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
7 and he made two cherubim, of gold, of beaten work, did he make them, out of the two ends of the propitiatory:
Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
8 one cherub, out of this end, and, one cherub, out of that end, out of the propitiatory itself, made he the cherubim, out of the two ends thereof:
Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
9 and the cherubim were spreading out their wings on high making a shelter with their wings over the propitiatory, with, their faces, one towards the other, towards the propitiatory, were the faces of the cherubim,
Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
10 And he made the table of acacia wood, two cubits, the length thereof and, a cubit, the breadth thereof, and a cubit and a half the height thereof,
Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
11 And he overlaid it with pure gold, —and he made thereto a rim of gold round about:
Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
12 and he mane thereto a border of a handbreadth, round about, and he made a rim of gold to the border thereof round about:
Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
13 and he cast for it, four rings of gold, and placed the rings upon the four corners, which pertained to the four feet thereof:
Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
14 near to the border, were the rings, as receptacles for the staves, for lifting the table;
Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
15 and he made the staves of acacia wood, and overlaid them with gold, —for lifting the table;
Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
16 and he made the utensils which were to be upon the table, its dishes and its pans and its bowls, and its basins for pouring out therewith, of pure gold.
Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
17 And he made the lampstand, of pure gold, of beaten work, made he the lampstand, its base and its shafts, its cups, its apples and its blossoms were, of the same;
Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
18 with, six branches coming out of its sides, —three branches of the lampstand out of its one side and three branches of the lampstand out of its other side:
Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
19 three cups like almond-flowers in the one branch—apple and blossom, and, three cups like almond-flowers, in the next branch, apple and blossom, so for the six branches coming out of the lampstand;
Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
20 and in the lampstand itself, four cups, like almond-flowers, its apples and its blossoms:
Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
21 with, an apple, under the two branches of the same, and, an apple, under the next two branches of the same, and, an apple, under the next two branches of the same, for the six branches coming out of the same:
Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
22 their apples and their brunches were of the same, all of it one beaten work, of pure gold.
Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
23 And he made the lamps thereof seven, —with its snuffers and its snuff-trays, of pure gold.
Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
24 Of a talent of pure gold, made he it, —and all the utensils thereof.
Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
25 And he made the incense altar, of acacia wood, —a cubit, the length thereof, and, a cubit, the breadth thereof, foursquare, and two cubits the height thereof, of the same, were the horns thereof.
Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
26 And he overlaid it with pure gold—the top thereof and the sides thereof round about, and the horns thereof, -and he made thereto a rim of gold, round about.
Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
27 And two rings of gold, made he thereto—beneath the rim thereof, upon the two corners thereof, upon the two sides thereof, —as receptacles for the staves, to lift it therewith.
Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
28 And he made the staves of acacia wood, —and overlaid them with gold.
Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
29 And he made the holy anointing oil, and the pure fragrant incense, —the work of a perfumer.
Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.

< Exodus 37 >