< Exodus 11 >

1 Then said Yahweh unto Moses—Yet one plague, will I bring in upon Pharaoh and upon Egypt, after that, he will let you go from hence, —when he doth let you go, he will, altogether drive, you out from hence.
Basi Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Nitaleta pigo moja zaidi kwa Farao na katika nchi ya Misri. Baada ya hilo, atawaacha mwondoke hapa na atakapofanya hivyo, atawafukuza mtoke kabisa.
2 Speak, I pray you, in the ears of the people, —and let them ask—every man of his neighbour, and every woman of her neighbour, articles of silver and articles of gold.
Waambie watu wote waume kwa wake wawaombe majirani zao vitu vya fedha na vya dhahabu.”
3 And Yahweh gave the people favour, in the eyes of the Egyptians, —even the man Moses himself, was exceeding great in the land of Egypt, —in the eyes of Pharaoh’s servants and in the eyes of the people.
(Bwana akawafanya Wamisri wawe na moyo wa ukarimu kwa Waisraeli, naye Mose mwenyewe akaheshimiwa sana na maafisa wa Farao na watu wote katika nchi ya Misri.)
4 And Moses said, Thus saith Yahweh, —About midnight, am, I, going forth in the midst of Egypt;
Kwa hiyo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Panapo usiku wa manane Mimi nitapita katika nchi yote ya Misri.
5 then shall every firstborn in the land of Egypt die, from the firstborn of Pharaoh who is sitting on his throne, unto the firstborn of the handmaid who is behind the two millstones, —and every firstborn of beasts;
Kila mwanaume kifungua mimba katika Misri atakufa, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Farao, aketiye penye kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mtumwa wa kike, anayesaga nafaka kwa jiwe, pamoja na kila mzaliwa wa kwanza wa mifugo.
6 then shall there be a great outcry, in all the land of Egypt, —such, as never was and, such, as shall not be again.
Patakuwepo kilio kikubwa katika nchi yote ya Misri, kilio kibaya ambacho hakijakuwepo wala kamwe hakitakuwepo tena.
7 But against none of the sons of Israel, shall a dog sharpen his tongue, neither against man nor beast, —that ye may know that Yahweh maketh a difference between Egypt and Israel.
Lakini miongoni mwa Waisraeli hakuna hata mbwa atakayembwekea mwanadamu wala mnyama yeyote.’ Ndipo mtakapojua kuwa Bwana huweka tofauti kati ya Misri na Israeli.
8 So shall all these thy servants come down unto me and bow themselves down to me saying—Go forth, thou and all the people who are in thy footsteps, and after that, will I go forth. And he went forth from Pharaoh, in a heat of anger.
Maafisa hawa wako wote watanijia, wakisujudu mbele yangu, wakisema, ‘Ondoka, wewe pamoja na watu wako wote wanaokufuata!’ Baada ya haya nitaondoka.” Kisha Mose, huku akiwa amewaka hasira, akamwacha Farao.
9 And Yahweh had said unto Moses, Pharaoh will not hearken unto you, —that my wonders may be multiplied in the land of Egypt.
Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Farao atakataa kukusikiliza, ili maajabu yangu yapate kuongezeka katika nchi ya Misri.”
10 So then, Moses and Aaron, did all these wonders before Pharaoh, —but Yahweh let Pharaoh’s heart wax bold, and he did not let the sons of Israel go out of his land.
Mose na Aroni wakafanya maajabu haya yote mbele ya Farao, lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke katika nchi yake.

< Exodus 11 >