< Ephesians 1 >

1 Paul, an apostle of Christ Jesus, through God’s will, unto the saints who are [in Ephesus] and faithful in Christ Jesus, —
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, nawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Efeso, mlio waaminifu katika kuungana na Kristo Yesu.
2 Favour unto you, and peace, from God our Father, and Lord Jesus Christ.
Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3 Blessed, be the God and Father of our Lord Jesus Christ, who hath blessed us with every spiritual blessing, in the heavenlies, in Christ,
Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Maana, katika kuungana na Kristo ametubariki kwa kutujalia zawadi zote za kiroho mbinguni.
4 According as he made choice of us, in him, before the founding of a world, that we might be holy and blameless in his presence; in love,
Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituteua tuwe wake katika kuungana na Kristo ili tuwe watakatifu na bila hitilafu mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
5 marking us out beforehand unto sonship, through Jesus Christ, for himself, according to the good pleasure of his will,
Mungu alikuwa ameazimia tangu zamani kutuleta kwake kama watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Ndivyo alivyopenda na kunuia.
6 Unto the praise of the glory of his favour wherewith he favoured us in the Beloved One, —
Basi, tumsifu Mungu kwa sababu ya neema yake tukufu katika Mwanae mpenzi!
7 In whom we have the redemption through his blood, the remission of our offences, according to the riches of his favour,
Maana kwa damu yake Kristo sisi tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa. Ndivyo ulivyo ukuu wa neema yake
8 which he made to superabound towards us; in all wisdom and prudence,
aliotukirimia bila kipimo! Kwa hekima na ujuzi wake wote
9 making known to us the sacred secret of his will, according to his good pleasure which he purposed in him, —
Mungu alitekeleza kile alichonuia, akatujulisha mpango wake uliofichika, ambao alikuwa ameazimia kuutekeleza kwa njia ya Kristo.
10 For an administration of the fulness of the seasons, to reunite for himself (under one head) the all things in the Christ, the things upon the heavens, and the things upon the earth, in him:
Mpango huo ambao angeutimiza wakati utimiapo ni kukusanya pamoja viumbe vyote, kila kitu mbinguni na duniani, chini ya Kristo.
11 In whom also we were taken as an inheritance, according to the purpose of him who energiseth all things according to the counsel of his will,
Kila kitu hufanywa kufuatana na mpango na uamuzi wa Mungu; naye Mungu ametuteua sisi tuwe watu wake kwa mapenzi yake katika kuungana na Kristo, kufuatana na azimio alilofanya tangu mwanzo.
12 That we should be for the praise of his glory—we who had hoped beforehand in the Christ, —
Basi, sisi tuliotangulia kumtumainia Kristo tunapaswa kuusifu utukufu wa Mungu!
13 In whom, ye also—hearing the word of the truth, the glad-message of your salvation, —in whom also believing, —were sealed with the Spirit of the promise, the Holy [Spirit],
Nanyi pia watu wa mataifa mengine, mliusikia ujumbe wa kweli yaani Habari Njema iliyowaletea wokovu, mkamwamini Kristo; naye Mungu, ili kuonyesha kuwa ninyi ni wake, akawapiga mhuri kwa kuwapeni yule Roho Mtakatifu aliyetuahidia.
14 Which is an earnest of our inheritance, unto the redemption of the acquisition; —unto his glorious praise.
Huyu Roho ni dhamana ya kurithi yote yale Mungu aliyowaahidia watu wake, na jambo hili latuhakikishia kwamba Mungu atawakomboa kabisa wote walio wake. Tuusifu utukufu wake!
15 For this cause, I also, —having heard of the faith on your part in the Lord Jesus, and that towards all the saints,
Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia juu ya imani yenu kwa Bwana Yesu na mapendo yenu kwa watu wa Mungu,
16 Cease not giving thanks in your behalf, making mention in my prayers,
sijaacha kamwe kumshukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika sala zangu
17 That, the God of our Lord Jesus Christ, the Father of glory, would give you a Spirit of wisdom and understanding in gaining a personal knowledge of him, —
ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo Baba mtukufu, awajalieni Roho wake atakayewapa hekima na kuwafunulieni Mungu mpate kumjua.
18 The eyes of your heart having been enlightened, that ye may know—what is the hope of his calling, what the riches of the glory of his inheritance in the saints,
Namwomba Mungu aifunue mioyo yenu iweze kuuona mwanga wake, mpate kutambua lile tumaini alilowaitieni na utukufu mkuu wa zawadi alizowawekea watu wake,
19 And what the surpassing greatness of his power unto us who believe, —according to the energy of the grasp of his might
mpate kutambua jinsi uwezo wake ulivyo mkuu mno kwa ajili yetu sisi tunaoamini. Uwezo huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na nguvu ile kuu mno
20 which he energised in the Christ, when he raised him from among the dead, and seated him at his right hand in the heavenlies,
aliyomfufua nayo Kristo kutoka wafu, akamketisha kulia kwake mbinguni.
21 Over-above all principality, authority, and power, and lordship, and every name that is named, not only in this age, but also in the coming one, (aiōn g165)
Huko, Kristo anatawala juu ya kila tawala, mamlaka, enzi na ukuu; anatawala juu ya kila cheo kiwezacho kutajwa katika ulimwengu huu na katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
22 And did put, all things, in subjection beneath his feet. And gave him to be head over all things unto the assembly,
Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamkabidhi kwa kanisa akiwa mkuu wa vitu vyote.
23 Which, indeed, is his body, the fulness of him who, the all things in all, is for himself filling up.
Kanisa ni mwili wa Kristo, na ukamilifu wake yeye anayekamilisha vitu vyote kila mahali.

< Ephesians 1 >