< Deuteronomy 27 >

1 And Moses with the elders of Israel commanded the people saying, —Observe all the commandment which I am commanding you to-day.
Mose na wazee wa Israeli wakawaagiza watu: “Yashikeni maagizo haya yote ninayowaagiza leo.
2 So then it shall be in the day when ye shall pass over the Jordan, into the land which Yahweh thy God is giving unto thee, —that thou shalt rear thee up great stones, and plaster them with plaster;
Mtakapokuwa mmevuka Mto Yordani na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, msimamishe mawe makubwa na mkayatie lipu.
3 and shalt write upon them all the words of this law, when thou shalt pass over, —to the end that thou mayest enter upon the land which Yahweh thy God is giving unto thee a land flowing with milk and honey, as Yahweh the God of thy fathers hath spoken unto thee.
Andikeni juu yake maneno yote ya sheria hii wakati mtakapokuwa mmevuka na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, nchi itiririkayo maziwa na asali, kama vile Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi.
4 So then it shall be when ye shall pass over the Jordan, that ye shall rear up these stones which I am commanding you to-day in Mount Ebal, —and thou shalt plaster them with plaster.
Mtakapokuwa mmevuka Yordani, simamisheni mawe haya juu ya Mlima Ebali, kama ninavyowaagiza leo, mkayatie lipu.
5 And thou shalt build there an altar unto Yahweh thy God, —an altar of stones, thou shalt not wield thereupon any tool of iron.
Huko mjengeeni Bwana Mungu wenu madhabahu, madhabahu ya mawe. Msitumie kifaa chochote cha chuma juu yake.
6 Of whole stones, shalt thou build the altar of Yahweh thy God, —then shalt thou cause to go up thereon ascending-sacrifices, unto Yahweh thy God;
Jengeni madhabahu ya Bwana Mungu wenu kwa mawe ya shambani, na mtoe sadaka za kuteketezwa juu yake kwa Bwana Mungu wenu.
7 and thou shalt sacrifice peace-offerings and shalt eat there, —and rejoice before Yahweh thy God.
Toeni sadaka za amani juu yake, mkizila na kufurahia mbele za Bwana Mungu wenu.
8 And thou shalt write upon the stones all the words of this law doing it plainly and well.
Nanyi mtaandika maneno yote ya sheria hii kwa wazi sana juu ya mawe haya ambayo mmesimamisha.”
9 And Moses and the priests the Levites spake unto all Israel saying, —Keep silence and hear O Israel, This day, hast thou been made a people unto Yahweh thy God.
Kisha Mose na makuhani, ambao ni Walawi, wakawaambia Israeli wote, “Nyamaza ee Israeli, sikiliza! Sasa umekuwa taifa la Bwana Mungu wako.
10 Thou shalt therefore hearken unto the voice of Yahweh thy God, —and do his commandments and his statutes, which I am commanding thee to-day.
Mtii Bwana Mungu wako, na kufuata amri zake na maagizo ninayokupa leo.”
11 And Moses commanded the people on that day, saying:
Siku ile ile Mose akawaagiza watu:
12 These, shall stand to bless the people upon Mount Gerizim, when ye have passed over the Jordan, —Simeon and Levi and Judah, and Issachar and Joseph and Benjamin;
Mtakapovuka Mto Yordani, makabila haya yatasimama juu ya Mlima Gerizimu kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benyamini.
13 and, these, shall stand by the curse in Mount Ebal, —Reuben Gad and Asher, and Zebulun Dan and Naphtali.
Makabila haya yatasimama juu ya Mlima Ebali kwa kutamka laana: Reubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani na Naftali.
14 Then shall the Levites respond and say unto every man of Israel with voice uplifted: —
Nao Walawi watawasomea watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
15 Cursed, be the man that maketh an image—cut or molten—an abomination unto Yahweh the work of the hands of the craftsman and putteth it in a secret place. And all the people shall respond and say—Amen.
“Alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga au mwenye kusubu sanamu, kitu ambacho ni chukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi stadi, na kuisimamisha kwa siri.”
16 Cursed, be he that holdeth in light esteem his father or his mother. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu amdharauye baba yake na mama yake.”
17 Cursed, be he that moveth back the boundary of his neighbour. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”
18 Cursed, be he that causeth the blind to wander in the way. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”
19 Cursed, be he that perverteth the right of the sojourner, the fatherless, or the widow. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu apotoshaye haki ya mgeni, yatima au mjane.”
20 Cursed, be he that lieth with his father’s wife, because he hath turned aside his father’s coverlet. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mke wa baba yake, kwa maana anadharau malazi ya baba yake.”
21 Cursed, be he that lieth with any beast. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mnyama yeyote.”
22 Cursed, be he that lieth with his sister, daughter of his father or daughter of his mother. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake.”
23 Cursed, be he that lieth with his mother-in-law. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mama mkwe wake.”
24 Cursed, be he that smiteth his neighbour secretly. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu amuuaye jirani yake kwa siri.”
25 Cursed, be he that taketh a bribe to shed innocent blood. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu apokeaye rushwa ili kumuua mtu asiye na hatia.”
26 Cursed, be he that establisheth not the words of this law to do them. And all the people shall say—Amen.
“Alaaniwe mtu yule ambaye hatashikilia maneno ya sheria hii kwa kuyatekeleza.”

< Deuteronomy 27 >