< Acts 24 >

1 And, after five days, came down the High-priest Ananias, with certain Elders and a certain orator Tertullus, and they informed the governor against Paul.
Baada ya siku tano, Kuhani Mkuu Anania aliwasili Kaisarea pamoja na wazee kadhaa na wakili mmoja wa sheria aitwaye Tertulo. Walimwendea yule mkuu wa mkoa wakamweleza mashtaka yao juu ya Paulo.
2 And, when he was called, Tertullus began to make accusation, saying—Seeing that, great peace, we are obtaining through thee, and that, reforms, are being brought about for this nation through thy forethought,
Paulo aliitwa na Tertulo akafungua mashtaka hivi: “Mheshimiwa Felisi, uongozi wako bora umeleta amani kubwa na marekebisho ya lazima yanafanywa kwa manufaa ya taifa letu.
3 both in all ways and in all places, are we accepting it, most excellent Felix, with all thankfulness.
Tunalipokea jambo hili kwa furaha daima na kutoa shukrani nyingi kwako kila mahali.
4 But, lest I too long detain thee, I beseech thee to hear us concisely in thy considerateness.
Lakini, bila kupoteza wakati wako zaidi, tunakusihi kwa wema wako, usikilize taarifa yetu fupi.
5 For, finding this man a pest, and moving sedition with all the Jews that are throughout the inhabited earth, a leader also of the sect of the Nazarenes, —
Tumegundua kwamba mtu huyu ni wa hatari mno. Yeye huanzisha ghasia kati ya Wayahudi kila mahali duniani na pia ni kiongozi wa kile chama cha Wanazareti.
6 who also attempted to desecrate even, the temple, whom we also seized,
Tena alijaribu kulikufuru Hekalu nasi tukamtia nguvuni. Kama ukimhoji wewe mwenyewe, utaweza kubainisha mambo haya yote tunayomshtaki kwayo.” Tulitaka kumhukumu kufuatana na Sheria yetu.
7
Lakini Lusia, mkuu wa jeshi, aliingilia kati, akamchukua kwa nguvu kutoka mikononi mwetu.
8 from whom thou shall be able, thyself, by making examination concerning all these things, to ascertain the things of which, we, are accusing him.
Kisha akaamuru washtaki wake waje mbele yako.
9 Moreover, the Jews also were joining in the attack, saying that, these things, were, so.
Nao Wayahudi waliunga mkono mashtaka hayo wakisema kwamba hayo yote yalikuwa kweli.
10 And Paul answered, when the governor had motioned him to be speaking, —Well knowing thee to have been, for many years, judge unto his nation, cheerfully, as to the things concerning myself, do I make defence;
Basi, mkuu wa mkoa alimwashiria Paulo aseme. Naye Paulo akasema, “Nafurahi kujitetea mbele yako nikijua kwamba umekuwa hakimu wa taifa hili kwa miaka mingi.
11 seeing thou art able to ascertain, that there are, not more, than twelve days, since I went up to worship in Jerusalem, —
Unaweza kujihakikishia kwamba si zaidi ya siku kumi na mbili tu zimepita tangu nilipokwenda kuabudu Yerusalemu.
12 and neither, in the temple, found they me, with any one, disputing, or causing, a halt, of the multitude, either in the synagogues or throughout the city, —
Wayahudi hawakunikuta nikijadiliana na mtu yeyote. Hawakunikuta nikichochea watu Hekaluni wala katika masunagogi yao, wala mahali pengine popote katika mji huo.
13 neither can they make good the things concerning which they are, now, accusing me.
Wala hawawezi kuthibitisha mashtaka waliyotoa juu yangu.
14 But I confess, this, unto thee, —That, according to the Way which they call a Sect, so, I am rendering divine service unto my father’s God, believing in all the things which, throughout the law, and those which, in the prophets, are written:
Ninachokubali mbele yako ni hiki: Mimi ninamwabudu Mungu na wazee wetu nikiishi kufuatana na Njia ile ambayo wao wanaiita chama cha uzushi. Ninaamini mambo yote yaliyoandikwa katika vitabu vya Sheria na manabii.
15 Having, hope, towards God, which, even these themselves, do entertain—that, a resurrection, there shall certainly be, both of righteous and of unrighteous:
Mimi namtumainia Mungu, na wao wanalo tumaini hilo, kwamba watu, wema na wabaya, watafufuka.
16 herein, even I, myself, am studying to have, an unoffending conscience, towards God and men, continually.
Kwa hiyo ninajitahidi daima kuwa na dhamiri njema mbele ya Mungu na mbele ya watu.
17 Now, after many years, intending to do, alms, unto my nation, I arrived, —also [to present] offerings; among which they found me, purified in the temple, not with a multitude, nor with tumult;
“Baada ya kukaa mbali kwa miaka kadhaa, nilirudi Yerusalemu ili kuwapelekea wananchi wenzangu msaada na kutoa dhabihu.
18 but certain Jews from Asia [caused it], —
Wakati nilipokuwa nikifanya hayo ndipo waliponikuta Hekaluni, nilipokuwa nimekwisha fanya ile ibada ya kujitakasa. Hakukuwako kundi la watu wala ghasia.
19 who ought, before thee, to have presented themselves, and to have been laying accusation, if, anything, they might have had against me: —
Lakini kulikuwa na Wayahudi wengine kutoka mkoa wa Asia; hao ndio wangepaswa kuwa hapa mbele yako na kutoa mashtaka yao kama wana chochote cha kusema dhidi yangu.
20 Or, let, these themselves, say what wrong they found, when I stood before the High-council, —
Au, waache hawa walio hapa waseme kosa waliloliona kwangu wakati niliposimama mbele ya Baraza lao kuu,
21 unless concerning this one voice, wherewith I cried aloud among them, as I stood—Concerning the raising of the dead, am, I, to be judged, this day, by you.
isipokuwa tu maneno haya niliyosema niliposimama mbele yao: Mnanihukumu leo hii kwa sababu ya kushikilia kwamba wafu watafufuliwa!”
22 And Felix deferred them, having more exact knowledge concerning the Way, —saying—As soon as, Lysias the captain, hath come down, I will give judgment as to your affairs, —
Hapo, Felisi, ambaye mwenyewe alikuwa anaifahamu hiyo Njia vizuri, aliahirisha kesi hiyo. Akawaambia, “Nitatoa hukumu juu ya kesi hiyo wakati Luisa, mkuu wa jeshi, atakapokuja hapa.”
23 giving orders unto the centurion, that he should be kept, and have a measure of liberty, and to be hindering, none, of his own from waiting upon him.
Kisha akamwamuru yule jemadari amweke Paulo kizuizini, lakini awe na uhuru kiasi, na rafiki zake wasizuiwe kumpatia mahitaji yake.
24 And, after certain days, Felix having arrived, with Drusilla his own wife, who was, a Jewess, he sent for Paul, and heard him concerning the faith, respecting Christ Jesus.
Baada ya siku chache, Felisi alifika pamoja na mkewe Drusila ambaye alikuwa Myahudi. Aliamuru Paulo aletwe, akamsikiliza akiongea juu ya kumwamini Yesu Kristo.
25 And, as he was reasoning of righteousness, and self-control, and the judgment to come, Felix, becoming greatly afraid, answered—For the present, be going thy way, and, when I find an opportunity, I will send for thee, —
Lakini wakati Paulo alipoanza kuongea juu ya uadilifu, juu ya kuwa na kiasi na juu ya siku ya hukumu inayokuja, Felisi aliogopa, akasema, “Kwa sasa unaweza kwenda; nitakuita tena nitakapopata nafasi.”
26 at the same time, also hoping that, money, would be given him by Paul; wherefore also, the more frequently sending for him, he used to converse with him.
Wakati huohuo alikuwa anatumaini kwamba Paulo angempa fedha. Kwa sababu hii alimwita Paulo mara kwa mara na kuzungumza naye.
27 When, however, two years, were completed, Felix, was succeeded, by Porcius Festus, and Felix, wishing to gain favour with the Jews, left Paul bound.
Baada ya miaka miwili, Porkio Festo alichukua nafasi ya Felisi, akawa mkuu wa Mkoa. Kwa kuwa alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi, Felisi alimwacha Paulo kizuizini.

< Acts 24 >