< Acts 24 >

1 And, after five days, came down the High-priest Ananias, with certain Elders and a certain orator Tertullus, and they informed the governor against Paul.
Baada ya siku tano, Anania kuhani mkuu, baadhi ya wazee na msemaji mmoja aitwaye Tertulo, wakaenda pale. Watu hawa wameleta mashtaka dhidi ya Paulo kwa gavana.
2 And, when he was called, Tertullus began to make accusation, saying—Seeing that, great peace, we are obtaining through thee, and that, reforms, are being brought about for this nation through thy forethought,
Paulo alipo simama mbele ya gavana, Tertulo akaanza kumshitaki na kusema kwa gavana, “kwa sababu yako tuna amani kuu; na kwa maono yako yanaleta mageuzi mazuri katika taifa letu;
3 both in all ways and in all places, are we accepting it, most excellent Felix, with all thankfulness.
basi kwa shukurani yote tunapokea kila kitu ukifanyacho, Wasalam mheshimiwa Feliki.
4 But, lest I too long detain thee, I beseech thee to hear us concisely in thy considerateness.
Lakini nisikuchoshe zaidi, nakusihi unisikilize maneno machache kwa fadhili zako.
5 For, finding this man a pest, and moving sedition with all the Jews that are throughout the inhabited earth, a leader also of the sect of the Nazarenes, —
Kwa maana tumempata mtu huyu mkorofi, na anasababisha Wayahudi wote kuasi duniani. Tena ni kiongozi wa madhehebu ya Wanazorayo. (Zingatia: Sehemu ya maneno ya mstari huu 24: 6
6 who also attempted to desecrate even, the temple, whom we also seized,
Na tena alijaribu kulitia hekalu unajisi hivyo tukamkamata., haumo kwenye nakala bora za kale). (Zingatia: Mstari huu
7
Lisiasi, afisa, alikuja na akamchukua kwa nguvu mikononi mwetu., haumo kwenye nakala bora za maandiko ya kale).
8 from whom thou shall be able, thyself, by making examination concerning all these things, to ascertain the things of which, we, are accusing him.
Ukimwuliza Paulo kuhusu mambo haya, hata utaweza kujifunza ni kitu gani tumemshtakia.”
9 Moreover, the Jews also were joining in the attack, saying that, these things, were, so.
Wayahudi nao wakamshtaki Paulo, wakisema kwamba haya mambo yalikuwa kweli.
10 And Paul answered, when the governor had motioned him to be speaking, —Well knowing thee to have been, for many years, judge unto his nation, cheerfully, as to the things concerning myself, do I make defence;
Liwali alipompungia mkono ili Paulo aongee, Paulo alijibu, “Ninajua ya kwamba kwa miaka mingi umekua mwamuzi wa taifa hili, na nina furaha kujieleza mwenyewe kwako.
11 seeing thou art able to ascertain, that there are, not more, than twelve days, since I went up to worship in Jerusalem, —
Waweza kuhakikisha kuwa hazijapita siku zaidi ya kumi na mbili tangu nilipopanda kwenda kuabudu Yerusalemu.
12 and neither, in the temple, found they me, with any one, disputing, or causing, a halt, of the multitude, either in the synagogues or throughout the city, —
Na waliponikuta katika hekalu, sikubishana na mtu yeyote, na sikufanya fujo katika mkutano, wala katika masinagogi wala ndani ya mji;
13 neither can they make good the things concerning which they are, now, accusing me.
na wala hawawezi kuhakikisha kwako mashitaka wanayoyashitaki dhidi yangu.
14 But I confess, this, unto thee, —That, according to the Way which they call a Sect, so, I am rendering divine service unto my father’s God, believing in all the things which, throughout the law, and those which, in the prophets, are written:
Ila nakiri hili kwako, ya kwamba kwa njia ile ambayo wanaiita dhehebu, kwa njia iyo hiyo ninamtumikia Mungu wa baba zetu. Mimi ni mwaminifu kwa yote yaliyoko kwenye sheria na maandiko ya manabii.
15 Having, hope, towards God, which, even these themselves, do entertain—that, a resurrection, there shall certainly be, both of righteous and of unrighteous:
Nina ujasiri ule ule kwa Mungu ambao hata hao nao wanaungojea, kuja kwa ufufuo wa wafu, kwa wote wenye haki na wasio na haki pia;
16 herein, even I, myself, am studying to have, an unoffending conscience, towards God and men, continually.
na kwa hili, ninafanya kazi ili niwe na dhamira isiyo na hatia mbele za Mungu na mbele ya watu kupitia mambo yote.
17 Now, after many years, intending to do, alms, unto my nation, I arrived, —also [to present] offerings; among which they found me, purified in the temple, not with a multitude, nor with tumult;
Sasa Baada ya miaka mingi nimekuja kuleta msaada kwa taifa langu na zawadi ya fedha.
18 but certain Jews from Asia [caused it], —
Nilipofanya hivi, Wayahudi fulani wa Asia wakanikuta ndani ya sherehe ya utakaso ndani ya hekalu, bila kundi la watu wala ghasia.
19 who ought, before thee, to have presented themselves, and to have been laying accusation, if, anything, they might have had against me: —
Watu hawa ambao imewapasa kuwapo mbele yako sasa hivi na waseme kile walichonacho juu yangu kama wana neno lo lote.
20 Or, let, these themselves, say what wrong they found, when I stood before the High-council, —
Au watu hawa wenyewe na waseme ni kosa gani waliloliona kwangu niliposimama mbele za baraza la kiyahudi;
21 unless concerning this one voice, wherewith I cried aloud among them, as I stood—Concerning the raising of the dead, am, I, to be judged, this day, by you.
isipokuwa kwa ajili ya kitu kimoja nilichokisema kwa sauti niliposimama katikati yao, ' ni kwa sababu ya ufufuo wa wafu ninyi mnanihukumu.”'
22 And Felix deferred them, having more exact knowledge concerning the Way, —saying—As soon as, Lysias the captain, hath come down, I will give judgment as to your affairs, —
Feliki alikuwa ametaarifiwa vizuri kuhusu njia, na akauahirisha mkutano. Akasema, “Lisia jemedari atakapokuja chini kutoka Yerusalemu nitatoa maamuzi dhidi ya mashitaka yenu.”
23 giving orders unto the centurion, that he should be kept, and have a measure of liberty, and to be hindering, none, of his own from waiting upon him.
Ndipo akamwamuru akida amlinde Paulo, ila awe na nafasi na hata asiwepo mtu wakuwakataza marafiki zake wasimsaidie wala wasimtembelee.
24 And, after certain days, Felix having arrived, with Drusilla his own wife, who was, a Jewess, he sent for Paul, and heard him concerning the faith, respecting Christ Jesus.
Baada ya siku kadhaa, Feliki akarudi na Drusila mkewe aliyekuwa Myahudi, akatuma kumwita Paulo na akasikiliza toka kwake habari za imani ndani ya Kristo Yesu.
25 And, as he was reasoning of righteousness, and self-control, and the judgment to come, Felix, becoming greatly afraid, answered—For the present, be going thy way, and, when I find an opportunity, I will send for thee, —
Ila Paulo alipokuwa akijadiliana naye kuhusu haki, kuwa na kiasi na hukumu itakayokuja, Feliki akapata hofu akajibu, “nenda mbali kwa sasa, ila nikipata muda tena, nitakuita.”
26 at the same time, also hoping that, money, would be given him by Paul; wherefore also, the more frequently sending for him, he used to converse with him.
Muda uo huo, alitegemea kwamba Paulo atampa fedha kwa hiyo alimwita mara nyingi akaongea naye.
27 When, however, two years, were completed, Felix, was succeeded, by Porcius Festus, and Felix, wishing to gain favour with the Jews, left Paul bound.
Ila miaka miwili ilipopita, Porkio Festo akawa Liwali baada ya Feliki, ila Feliki alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi, hivyo akamwacha Paulo chini ya uangalizi.

< Acts 24 >