< 2 Samuel 8 >

1 And it came to pass, after this, that David smote the Philistines, and subdued them, —and David took the bridle of the metropolis, out of the hand of the Philistines.
Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
2 And he smote Moab, and measured them with the line casting, them down to the ground, and be measured with two lines to put to death, and with one full line to keep alive, —so the Moabites became David’s, as servants, bringing gifts.
Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
3 And David smote Hadadezer son of Rehob, king of Zobah, —when he went to lay his hand on the River Euphrates.
Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
4 And David captured from him, a thousand and seven hundred horsemen, and twenty thousand footmen, —and David destroyed all the chariots, but reserved of them, a hundred chariots.
Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
5 And, when the Syrians of Damascus came to help Hadadezer, king of Zobah, David smote of the Syrians, twenty-two thousand men.
Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
6 Then David put garrisons in Syria of Damascus, and the Syrians became David’s, as servants bringing gifts, —and so Yahweh gave victory unto David, whithersoever he went.
Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
7 And David took the shields of gold which had come to the servants of Hadadezer, —and brought them to Jerusalem;
Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
8 also, from Betah and from Berothai, cities of Hadadezer, did King David take bronze, exceeding much.
Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
9 And, when Tou king of Hamath heard that David had smitten all the forces of Hadadezer,
Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
10 then Tou sent Hadoram his son unto King David, to ask after his welfare, and to bless him, because he had fought against Hadadezer and had smitten him, for Hadadezer had had wars with Tou, —and, in his hand, were vessels of silver, and vessels of gold, and vessels of bronze.
akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
11 Them also, did King David hallow unto Yahweh, —with the silver and the gold which he had hallowed from all the nations which he had subdued:
Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
12 from Syria, and from Moab, and from the sons of Ammon, and from the Philistines, and from Amalek, —and from the spoil of Hadadezer son of Rehob, king of Zobah.
yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
13 And David made a name, when he returned from his smiting of the Syrians in the valley of salt, —eighteen thousand.
Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
14 And he put, in Edom, garrisons, throughout all Edom, put be garrisons, and so it was that all Edom became servants unto David, —and Yahweh gave victory unto David, whithersoever he went.
Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
15 And David reigned over all Israel, —and so it was that David used to execute justice and righteousness for all his people;
Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
16 and, Joab, son of Zeruiah, was over the army, —and, Jehoshaphat, son of Ahilud, was remembrancer.
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
17 And, Zadok, son of Ahitub, and Abimelech, son of Abiathar, were priests, —and, Seraiah, was scribe;
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
18 and, Benaiah, son of Jehoiadah, was over the Cherethites and the Pelethites, —and, the sons of David, became, chief rulers.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.

< 2 Samuel 8 >