< 2 Kings 7 >

1 Then said Elisha—Hear ye the word of Yahweh, —Thus, saith Yahweh—About this time to-morrow, a measure of fine meal for a shekel, and two measures of barley for a shekel, in the gate of Samaria.
Elisha akasema, “Sikiliza neno la Bwana. Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
2 Then the officer on whose hand the king leaned responded to the man of God, and said, Even if Yahweh were making windows in the heavens, could this thing, come to pass? And he said—Lo! thou, art about to see it with thine own eyes, but, thereof, shalt thou not eat!
Yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake akamwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Elisha akajibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
3 Now there were, four men, lepers, at the entrance of the gate, —and they said one to another—Why are, we, sitting here until we are dead?
Basi kulikuwepo na watu wanne wenye ukoma katika ingilio la lango la mji. Wakaambiana, “Kwa nini tukae hapa mpaka tufe?
4 If we say—Let us enter into the city, Then, the famine, is in the city, and we shall die there, and, if we remain here, then shall we die. Now, therefore, let us fall away unto the camp of the Syrians, if they save us alive, we shall live, and, if they put us to death, we shall die.
Kama tukisema, ‘Tutaingia mjini,’ mjini kuna njaa, nasi tutakufa humo. Kama tukikaa hapa, tutakufa. Kwa hiyo twende kwenye kambi ya Waaramu na tujisalimishe. Kama wakituacha hai, tutaishi; kama wakituua, basi na tufe.”
5 So they rose up in the twilight, to enter into the camp of the Syrians, —and, when they entered the outskirts of the camp of the Syrians, lo! there was not there, a man.
Wakati wa giza la jioni, wakaondoka na kwenda kwenye kambi ya Waaramu. Walipofika mwanzo wa kambi, hapakuwa na mtu,
6 Now, the Lord, had caused the camp of the Syrians to hear a noise of chariots, noise of horses, a noise of a great host, —and they said one to another—Lo! the king of Israel hath hired against us—the kings of the Hittites, and the kings of the Egyptians, to come against us.
kwa kuwa Bwana alilifanya jeshi la Waaramu lisikie sauti kama ya magari ya vita, farasi na jeshi kubwa, kiasi kwamba waliambiana, “Tazama, mfalme wa Israeli ameajiri mfalme wa Wahiti na mfalme wa Wamisri kuja kutushambulia sisi!”
7 So they arose, and fled in the twilight, and left their tents, and their horses, and their asses, —the camp, just as it was, —and fled for their lives.
Kwa hiyo wakaondoka na kukimbia wakati wa giza la jioni na kuacha mahema yao, farasi wao na punda wao. Wakakimbia kuokoa maisha yao na kuacha kila kitu ndani ya kambi kama kilivyokuwa.
8 When, therefore, these lepers came in as far as the outskirts of the camp, they entered into one tent, and did eat and drink, and carried from thence silver, and gold, and raiment, and went away and hid them, —and came again, and entered into another tent, and carried from thence—and went and hid them.
Wale watu wenye ukoma walipofika mwanzoni mwa kambi, wakaingia kwenye mojawapo ya mahema. Wakala na kunywa, na kuchukua fedha, dhahabu na nguo, wakaenda kuvificha. Wakarudi na kuingia katika hema jingine, na kuchukua baadhi ya vitu kutoka ndani yake na kuvificha pia.
9 Then said they one to another—Not a right thing, are, we, doing. This day, is, a day of good tidings, and, we, are holding our peace, if we tarry until the light of the morning, there will come upon us, some misfortune, —Now, therefore, come and let us go in, and tell the household of the king.
Kisha wakaambiana, “Hili tunalolifanya sio jema. Hii ni siku ya habari njema, nasi tunakaa kimya. Kama tukisubiri mpaka mapambazuko, maafa yatatupata. Twendeni mara moja tukatoe habari hizi katika jumba la mfalme.”
10 So they came in and called unto the gate of the city, and told them, saying, We entered into the camp of the Syrians, and lo! there was not there, a man, nor sound of human being, —only horses tied, and asses tied, and their tents, just as they were!
Hivyo wakaenda mjini na kuwaita walinzi wa langoni, wakawaambia, “Tulikwenda katika kambi ya Waaramu lakini hapakuwepo na mtu huko, hata sauti ya mtu yeyote, ila farasi na punda waliofungwa na mahema yaliyoachwa kama yalivyokuwa.”
11 And the watchers of the gate called and told it to the household of the king, within.
Walinzi wa langoni wakatangaza habari ile kwa sauti kuu, na taarifa hii ikatolewa ndani ya jumba la mfalme.
12 Then arose the king by night, and said unto his servants, Let me tell you, I pray you, what the Syrians have done to us, —they knew that we were, famished, so they have gone forth out of the camp, to hide in the field, saying, When they come forth out of the city, then shall we take them alive, and, into the city, will we enter.
Mfalme akaamka usiku na kuwaambia maafisa wake, “Nitawaambia kile Waaramu walichotufanyia. Wanajua kwamba tuna njaa, hivyo wameacha kambi yao ili kujificha mashambani, wakifikiri, ‘Kwa hakika watatoka nje ya mji, nasi tutawakamata wakiwa hai na kuingia ndani ya mji.’”
13 Then responded one of his servants, and said—Let there be taken, I pray thee, five of the horses that remain, which have been left therein, there they are, according to all the multitude of Israel who have been left therein, there they are, according to all the multitude of Israel, who have been consumed, —and let us send and see!
Mmoja wa maafisa wake akajibu, “Waamuru watu wachache wakawachukue farasi watano kati ya wale waliobaki katika mji. Hatima yao itakuwa kama ya Waisraeli wote walio hapa. Watakuwa tu kama Waisraeli hawa ambao wanangoja kifo. Hivyo tuwatumeni wajue kumetendeka nini.”
14 So they took two chariots and horses, —and the king sent after the host of the Syrians, saying, Go and see!
Ndipo wakachagua magari mawili ya vita pamoja na farasi wake, naye mfalme akawatuma wafuatilie jeshi la Waaramu. Akawaamuru waendeshaji akisema, “Nendeni mkaone ni nini kilichotokea.”
15 And they followed them as far as the Jordan, and lo! all the way, was full of garments, and utensils, which the Syrians had cast away in their fright, —and the messengers returned, and told the king.
Wakawafuatia hadi Yordani, nao wakakuta barabara yote ikiwa imetapakaa nguo na vyombo vya Waaramu walivyokuwa wamevitupa walipokuwa wanatoroka. Basi wale wajumbe wakarudi na kutoa taarifa kwa mfalme.
16 Then went the people forth and spoiled the camp of the Syrians, —and so there came to be—a measure of fine meal for a shekel, and two measures of barley for a shekel, according to the word of Yahweh.
Kisha watu wakatoka na kuteka nyara kambi ya Waaramu. Kwa hiyo kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
17 Now, the king, had set the officer on whose hand he leaned, in charge over the gate, and the people trode upon him in the gate, that he died, —as spake the man of God, who said it when the messenger came down to him.
Basi mfalme alikuwa amemweka yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake awe msimamizi wa lango. Nao watu wakamkanyaga walipoingia langoni, naye akafa, kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa ametangulia kusema wakati mfalme alipofika nyumbani kwake.
18 Yea it came to pass, as the man of God had spoken unto the messenger, saying, —Two measures of barley for a shekel, and a measure of fine meal for a shekel, shall there be about this time to-morrow, in the gate of Samaria:
Ikatokea kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia mfalme: “Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
19 And when the officer responded to the man of God, and said, Lo! then, if Yahweh were making windows in the heavens, could it be according to this word? And he said, —Lo! thou art about to see it with thine own eyes, but, thereof, shalt thou not eat.
Yule afisa alikuwa amemwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Naye yule mtu wa Mungu alikuwa amemjibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
20 Yea it fell out to him, thus, —and the people trode upon him in the gate, that he died.
Ndivyo hasa ilivyotokea kwake, kwa kuwa watu walimkanyaga langoni, naye akafa.

< 2 Kings 7 >