< 2 Kings 3 >

1 Now, Jehoram son of Ahab, began to reign over Israel, in Samaria, in the eighteenth year of Jehoshaphat, king of Judah, —and he reigned twelve years.
Basi katika mwaka wa kumi na nane wa Yehoshefati mfalme wa Yuda, Yoramu mwana wa Ahabu alianza kutawala juu ta Israeli katika Samaria; alitawala miaka kumi na miwili.
2 And he did the thing that was wicked in the eyes of Yahweh, only, not like his father, nor like his mother, —but he put away the pillars of Baal which, his father, had made;
Alifanya yaliyo maovo usoni kwa Yahwe, lakini si kama baba yake na mama yake; kwa kuwa aliiondoa ile nguzo ya mungu wa Baali ambayo baba yake aliitengeneza.
3 nevertheless, unto the sins of Jeroboam son of Nebat which he caused Israel to commit, he did cleave, —he turned not away therefrom
Hata hivyo alishikilia dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli kufanya dhambi; wala hakuziacha mbali nao.
4 Now, Mesha king of Moab, was a sheep-master, —and used to render to the king of Israel, the wool of hundred thousand fat sheep, and of a hundred thousand rams.
Basi Mesha mfalme wa Moabu alifuga kondoo. Alikuwa akimpatia mfalme wa Israeli kondoo 100, 000 na manyoya ya kondoo dume 100, 000.
5 And it came to pass, when Ahab died, that the king of Moab revolted against the king of Israel.
Ila baada ya Ahabu kufa, yule mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli.
6 So King Jehoram went forth, on that day, out of Samaria, and numbered all Israel.
Hivyo Mfalme Joramu alikaondoka Samaria katika muda huo kuwahamasisha Waisraeli wote kwa ajili ya vita.
7 And he departed, and sent unto Jehoshaphat king of Judah, saying—The king of Moab, hath revolted against me, wilt thou go with me against Moab to battle? And he said—I will go up, I am as thou art, my people are as thy people, my horses as thy horses.
Akatuma mjumbe kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda, akisema, “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je mtakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?” Yehoshafati akajibu, “Nitaenda. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
8 And he said—Which way, then, shall we go up? And he said—The way of the wilderness of Edom.
Ndipo akasema, “Tutawashambulia kwa njia gani?” Yehoshafati akajibu, “Kwa njia ya jangwa la Edemu.
9 Then departed the king of Israel, and the king of Judah, and the king of Edom, and went round, a journey of seven days, —and there was no water for the host, nor for the cattle that went with them.
Hivyo huyo mfalme wa Israeli, Yuda, na Edomu wakazunguka kwa mda wa siku saba. Hapakuwa na maji kwa ajili ya jeshi lao, wala kwa farasi au wanyama.
10 Then said the king of Israel—Alas! for Yahweh hath called these three kings, to deliver them into the hand of Moab.
Basi mfalme wa Israeli akasema, “Hii ni nini? Yahwe amewaita wafalme watatu ili kutekwa mikononi mwa Moabu?”
11 So Jehoshaphat said—Is there not, here, a prophet of Yahweh, that we may enquire of Yahweh, from him? Then answered one of the servants of the king of Israel, and said, Here, is Elisha son of Shaphat, who poured water on the hands of Elijah.
Lakini Yehoshafati akasema, “je hakuna nabii wa Yahwe, ambaye tunaweza kufanya shauri kuhusu Yahwe kupitia yeye?” Mtumishi mmoja wa wafalme wa Israeli akajibu na kusema, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa, ambaye alikuwa akimimina maji kwenye mikono ya Eliya.”
12 Then said Jehoshaphat, The word of Yahweh, is with him. So the king of Israel, and Jehoshaphat, and the king of Edom, went down unto him.
Yehoshafati akasema, “Neno la Yahwe liko pamoja nami.” Hivyo mfalme wa Israeli, Yehoshaphati, na mfalme wa Edomu wakashuka chini kwenda kwake.
13 And Elisha said unto the king of Israel—What have I and thou in common? get thee unto the prophets of thy father, and unto the prophets of thy mother. But the king of Israel said to him—Nay! for Yahweh hath called together these three kings, to deliver them into the hand of Moab.
Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nifanye nini kwa ajili yako? Nenda kwa manabii wa baba na mama yako.” Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia, “Hapana, kwa sababu Yahwe amewaita hawa wafalme watatu pamoja ili kuruhusu jeshi la Moabu liwateke.”
14 Then said Elisha—By the life of Yahweh of hosts, before whom I stand, were it not that, the countenance of Jehoshaphat king of Judah, I would lift up, I would neither look at thee, nor see thee.
Elisha akajibu, “Kama Yawhe wa majeshi aishivo, ambaye nimesimama mbele zake, hakika kama nisingemheshimu uwepo wa Yehoshafati mfalme wa Yeda, Nisingevuta usikivu kwako, au hata kukutazama.
15 But, now, bring me one that can touch the strings. For it used to be, when the player touched the strings, then would, the hand of Yahweh, be upon him.
Lakini sasa niletee mwanamuziki.” Ndipo alipokuja mpiga muziki alipocheza, mkono wa Yahwe ukaja juu ya Elisha.
16 Then said he, Thus, saith Yahweh, Make, in this torrent-bed, pits, pits!
Akasema, “'Yahwe asema hivi, 'Fanya hili bonde la mto mkavu lijae mahandaki.'
17 For, thus, saith Yahweh—Ye shall not see wind, and ye shall not see rain, yet, that torrent-bed, shall be filled with water, —And ye shall drink, ye, and your cattle, and your beasts;
Kwa kuwa Yahwe asema hivi, 'Hutaona upepo, wala hamtaona mvua, bali hili bonde la mto litajaa maji, na mtakunywa, ninyi na mifugo yenu na wanyama wenu wote.'
18 And, this being a small thing in the eyes of Yahweh, he will deliver Moab into your hand;
Hiki ni kitu rahisi usoni mwa Yahwe. Pia atawapa ushindi juu ya hao Wamoabu.
19 And ye shall smite every strong city, and every choice city, and, every goodly tree, shall ye fell, and, all fountains water, shall ye close up, —and, every goodly heritage, shall ye mar with stones.
Mtaiteka kila ngome ya mji na kila mji mzuri, kukata kila mti mzuri, kusimamisha chemichemi zote za maji, na kuharibu kila sehemu nzuri ya nchi na miamba.”
20 And it came to pass, in the morning, when the offering ascended, that lo! waters, were coming in from the way of Edom, —and the land was filled with the water.
Hivyo asubuhi karibia na mda wa kutoa sadaka ya kuteketeza, yakaja maji kutoka uelekeo wa Edomu; nchi ikajaa maji.
21 Now, all Moab, had heard that the kings had come up to fight against them, —so they came together, from all who could gird on a girdle and upwards, and took their stand at the border.
Ndipo wakati Wamoabu wote waliposikia kwamba wafalme wamekuja kupigana dhidi yao, walikusanyika pamoja, wote waliotakiwa kubeba silaha, na wakasimama mpakani.
22 And, when they rose early in the morning, the sun, shone forth upon the waters, —and so the Moabites beheld over against them, the waters, red as blood.
Walitembea asubuhi na mapema na jua likang'aa kwenye maji. Wakati Wamoabu walipoyaona yale maji yaliyowaelekea, yanaonekana mekundu kama damu.
23 They said therefore—Blood, —this! Destroyed! The kings have destroyed each other! Yea they have smitten every man his neighbour, —Now, then, to the spoil, O Moab!
Wakatamka kwa hasira, “Hii ni damu! Yamkini hao wafalme wameharibiwa, na wameuna wao kwa wao! Sasa basi, Moabu, ngoja tuende tukawateke nyara!”
24 And, when they came into the camp of Israel, Israel arose and smote Moab, and they fled from before them, —so they entered thereinto, yea still farther entered Moab;
Wakati walipokuja kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakawashtukiza na kuwashambulia Wamoabi, ambao walikimbia mbele yao. Hilo jeshi la Israeli waliwakimbiza hao Wamoabu hadi kwao wakiwaua.
25 And, the cities, they pulled down, and, on every goodly heritage, they cast every man his stone, and filled it, and, all fountains of waters, they closed up, and, every goodly tree, they felled, and, though they left the stones thereof in Kir-haraseth, yet the slingers surrounded and smote it.
Waliiharibu miji, na kila aina ya amani ya nchi kila mtu alirusha jiwe mpaka ulipojaa. Walizuia kila chemichemi ya maji na kukata chini miti mizuri yote. Kir-haresethi tu ndiyo ilichwa na mawe yake. Lakini hao maaskari wakawashambulia na makombeo wakiwazunguka na kuishambulia.
26 And, when the king of Moab saw that, the battle, prevailed against him, he took with him seven hundred men that drew swords, to break through against the king of Edom, but they could not.
Ndipo Mfalme Mesha wa Moabu alipoona kwamba ameshindwa, alichukua watu hodari wa upanga mia saba pamoja naye kwenda kwa mfalme wa Edomu, lakini walishindwa.
27 So he took his firstborn son who was to have reigned in his stead, and offered him up as an ascending-sacrifice upon the wall. And so it came to pass that there was great indignation against Israel. And they brake up from against him, and returned to their own land.
Ndipo akamchukua mtoto wake wa kwanza, ambaye angetawala baada ya yeye, na akamuudhi kwa kumtoa kama sadaka ya kuteketezwa juu ya ukuta. Hivyo, kulikuwa na hasira kubwa dhidi ya Israeli, na hao Waisraeli, na Jeshi la Israeli likamuacha mfalme Mesha na kurudi kwenye nchi yao.

< 2 Kings 3 >