< 2 Kings 21 >

1 Twelve years old, was Manasseh when he began to reign, and, fifty-five years, reigned he in Jerusalem, —and the name of his mother was Hephzibah.
Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na mbili wakati alipoanza kutawala; alitawala miaka hamsini na tano katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Hefziba.
2 And he did the thing that was wicked in the eyes of Yahweh, —after the abominable practices of the nations, whom Yahweh had dispossessed from before the sons of Israel.
Alifanya maovu usoni kwa Yahwe, kama machukizo ya mataifa ambayo Yahwe aliyafukuza nje mbele ya wana wa Israeli.
3 He again built the high places, which Hezekiah his father had destroyed, —and reared altars to Baal, and made a Sacred Stem, as did Ahab, king of Israel, and bowed down to all the army of the heavens, and served them.
Kwa kupajenga tena mahala pa juu ambapo Hezekia baba yake alipaharibu, na akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali, akafanya Ashera, kama Ahabu mfalme wa Israeli alivyofanya, akasujudu kwa nyota zote za mbinguni na kuwaabudu wao.
4 And he used to build altars in the house of Yahweh, —concerning which Yahweh had said, —In Jerusalem, will I put my Name.
Manase akajenga madhabahu za kipagani kwenye nyumba ya Yahwe, ingawaje Yahwe aliamuru, “Jina langu litakuwa Yerusalemu daima.”
5 And he built altars to all the army of the heavens, —in the two courts of the house of Yahweh;
Akajenga madhabahu kwa ajili ya nyota zote za mbinguni katika behewa mbili za nyumba ya Yahwe.
6 and caused his son to pass through the fire, and practised hidden arts and used divination, and dealt with a familiar spirit and wizards, —he exceeded in doing the thing that was wicked in the eyes of Yahweh, provoking [him] to anger;
Akamuweka mtoto wake wa kiume kwenye moto; akatazama bao ushirikina na kujishuhulisha pamoja wale ambao wenye pepo wa utambuzi na wale wachawi. Akafanya maovu mengi usoni kwa Yahwe na kuchochea hasira kwa Mungu.
7 and he set the image of the Sacred Stem which he had made, —in the house, of which Yahweh had said unto David, and unto Solomon his son, In this house, and in Jerusalem which I have chosen out of all the tribes of Israel, will I put my Name, unto times age-abiding;
Sanamu ya kuchongwa ya Ashera ambayo aliitnegeneza, akaiweka kwenye nyumba ya Yahwe. Nyumba hii ndiyo ambayo Yahwe alimwambia Daudi na Sulemani mwanawe; alisema: “Ni nyumba hii na katika Yerusalemu, ambayo nimeichagua kutoka makabila yote ya Isaraeli, ambako nitaliweka jina langu milele.
8 and I will not again let the foot of Israel wander away from the soil which I gave unto their fathers. Only if they take heed to do according to all that I have commanded them, even to the extent of all the law which, my servant Moses, commanded them.
Sintofanya miguu ya Israeli kushindwa tena nje ya nchi ambayo niliwapa babu zao, kama tu watakuwa makini kutii yale yote niliyowaamuru, na kufuata sheria zote ambazo mtumishi wangu Musa aliwaamuru.”
9 But they hearkened not, —and Manasseh led them astray to do the thing that was wicked, more than the nations which Yahweh destroyed from before the sons of Israel.
Lakini watu hawakusikia, na Manase akawaongoza kufanya maovu zaidi kuliko yale ya mataifa ambayo Yahwe aliyaharibu mbele ya watu wa Israeli.
10 Yahweh therefore spake through his servants the prophets saying—
Basi Yahwe akaongea na watumishi wake manabii, akisema,
11 Because Manasseh king of Judah hath made these abominations—hath done that which is wicked, more than all which the Amorites did who were before him, and hath caused, even Judah, to sin with his manufactured gods,
Kwasababu Manase mfalme wa Yuda amefanya haya machukizo, na kutenda maovu zaidi kuliko yote waliyoyatenda Waamori ambao walikuwa mbele yake walikubali, na pia aliwafanya Yuda kuasi kwa sanamu zake,
12 therefore—Thus, saith Yahweh, God of Israel, Behold me! bringing in calamity upon Jerusalem and Judah, —that, whosoever heareth thereof, both his ears, will tingle;
kwa hiyo Yahwe, Mungu wa Israeli, akasema hivi: Tazama, nakaribia kuleta uovu juu ya Yerusalemu na Yuda ambayo kila mtu asikiapo kuhusu hilo, masikio yake yote yatang'aa.
13 And I will stretch over Jerusalem, the line of Samaria, and the plummet of the house of Ahab, —and will wipe out Jerusalem, as one wipeth out a dish, wiping it and turning it upside down;
Nitanyoosha juu ya Yerusalemu kipimo kilichotumika dhidi ya Samaria, na kuangusha msatari utakaotumika dhidi ya nyumba ya Ahabu; Nitaifuta Yerusalemu safi, kama kufuta sahani, kuifuta na kuifunika juu chini.
14 And will abandon the remnant of mine inheritance, and deliver them into the hand of their enemies, —and they shall become a prey and a plunder, to all their enemies:
Nitawatupa masalia ya urithi wangu na kuwaweka mikononi mwa maadui zao. Watakuwa nyara na mateka kwa maadui zao wote,
15 Because they have done the thing that is wicked in mine eyes, and have become such as to provoke me to anger, —from the day when their fathers came forth out of Egypt, even until this day.
kwa sababu wamefanya yaliyo maovu usoni kwangu, na kunichochea hasira, tangu siku babu zao walipotoka Misri, hadi leo.”
16 Moreover also, innocent blood, did Manasseh shed in great abundance, till he had filled Jerusalem, from one end to the other, besides his committing the sins which he caused, Judah, to commit, in doing the thing that was wicked in the eyes of Yahweh.
Aidha, Manase akazimwaga damu nyingi za wasio na hatia, hadi alipoijaza Yerusalemu kutoka upande huu kwenda mwingine kwa kifo. Hii ilikuwa ni kuongeza kwenye dhambi ambayo aliifanya Yuda kuasi, wakati walipofanya uovu mbele za Yahwe.
17 Now, the rest of the story of Manasseh, and all that he did, and his sin that he committed, are, they, not written in the book of the Chronicles of the Kings of Judah?
Kama kwa mambo mengine yamhusuyo Manase, yote aliyoyafanya, na dhambi ambayo aliyoifanya, je haya hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio cha wafalme wa Yuda?
18 And Manasseh slept with his fathers, and was buried in the garden of his own house, in the garden of Uzza, —and, Amon his son, reigned, in his stead.
Manase akalala pamoja na babu zake na alizikwa kwenye bustani ya nyumba yake, katika bustani ya Uza. Amoni mwanawe akawa mfalme katika sehemu yake.
19 Twenty-two years old, was Amon when he began to reign, and, two years, reigned he in Jerusalem, —and, his mother’s name, was Meshullemeth daughter of Haruz, of Jotbah.
Amoni alikuwa na miaka kumi na mbili alipoanza kutawala; alitawala miaka miwili katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Meshlemethi; alikuwa binti wa Haruzi wa Yotba.
20 And he did the thing that was wicked in the eyes of Yahweh, —as did Manasseh his father;
Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe, kama manase baba yake alivyofanya.
21 yea he walked in all the way wherein, his father, had walked, —and served the manufactured gods that, his father, had served, and bowed down to them;
Amoni alifuata njia zote ambazo baba yake alizotembelea na kuabudu sanamu ambazo baba yake aliziabudu, na kuzisujudia.
22 and forsook Yahweh the God of his fathers, —and walked not in the way of Yahweh.
Akajitenga na Yahwe, Mungu wa baba zake, na hakutembea katika njia ya Yahwe.
23 And the servants of Amon, conspired against him, —and slew the king in his own house.
Watumishi wa Amoni wakafanya njama dhidi yake na kumuua mfalme kwenye nyumba yake mwenyewe.
24 Then the people of the land smote all who had conspired against King Amon, —and the people of the land made, Josiah his son, king, in his stead.
Lakini watu wa nchi wakawaua watu wote waliofanya njama dhidi ya mfalme Amoni, na wakamfanya Yosia mtoto wake kuwa mfalme katika sehemu yake.
25 Now, the rest of the story of Amon, what he did, is, it, not written in the book of the Chronicles of the Kings of Judah?
Kama ilivyo kwa mambo mengine yamhusuyo Amoni yale aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
26 And he was buried in his grave, in the garden of Uzza, —and, Josiah his son, reigned, in his stead.
Watu wakamzika kwenye kaburi lake katika bustani ya Uza, na Yosia mwanawe akawa mfalme katika sehemu yake.

< 2 Kings 21 >