< 2 Chronicles 3 >

1 Then began Solomon, to build the house of Yahweh, in Jerusalem, in Mount Moriah, where he had appeared unto David his father, —in the place which David had prepared, in the threshing-floor of Ornan the Jebusite.
Kisha Selemani akaanza kuijenga nyumba ya Yahwe katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, ambako Yahwe alimtokea Daudi baba yake. Aliandaa sehemu ambayo Daudi aliikusudia, katika sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.
2 And he began to build, in the second month, on the second, in the fourth year of his reign.
Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
3 And, these, are the things wherein Solomon was grounded for the building of the house of God, —The length, by cubits, in the first measure, was sixty cubits, and, the breadth, twenty cubits.
Sasa hivi ndinyo vipimo vya ule msingi ambao Selemani alijenga kwa ajili ya nyumba ya Mungu. Akitumia mtindo wa vipimo vya zamani, urefu ulikuwa mikono sitini, na upana ulikuwa mikono ishirini.
4 And, the porch which was in front of the length, in front of the breadth of the house, was twenty cubits, and, the height thereof, was a hundred and twenty, —and he overlaid it, within, with pure gold.
Urefu wa ukumbi mbele ya nyumba ulikuwa mikono ishirini, ukilingana na upana wa nyumba, urefu wake kwenda juu pia ulikuwa mikono ishirini, na Selemani akaifunika sehemu ya ndani kwa dhahabu halisi.
5 And, the greater house, covered he with cypress wood, and overlaid it with fine gold, —and raised thereon palms, and wreathed garlands.
Akailitengeneza paa la ukumbi mkuu kwa miti ya miberoshi, ambayo aliifunika kwa dhahabu halisi, na ambayo aliifunika kwa miti ya mitende na minyororo.
6 And he covered the house with precious stones, for beauty, —and, the gold, was gold of Parvaim.
Akaipamba nyumba kwa vito vya thamani; dhahabu ilikuwa dhahabu kutoka Parvaimu.
7 And he covered the house, the beams, the entrance-hall, and the walls thereof and the doors thereof, with gold, —and he carved cherubim upon the walls.
Pia akazifunika boriti zake, vizingiti, kuta, na milango kwa dhahabu; akachonga makerubi juu ya kuta zake.
8 And he made the most holy house, the length whereof, was, according to the breadth of the house, twenty cubits, and, the breadth thereof, twenty cubits, —and he covered it with fine gold, to [the number of] six hundred talents;
Akaijenga sehemu ya patakatifu pa patakatifu. Urefu wake ulilingana na upana wa nyumba, mikono ishirini, na upana wake pia ulikuwa mikono ishirini. Aliifunika kwa dhahabu halisi, thamani yake ilikuwa talanta mia sita.
9 and, the weight of the nails, amounted to fifty shekels of gold, —and, the upper chambers, covered he with gold.
Uzito wa misumari ulikuwa shekeli hamsini za dhahabu. Alizifunika sehemu za juu kwa dhahabu.
10 And he made, in the most holy house, two cherubim, of carved work, —and covered them with gold.
Akachonga makerubi wawili kwa ajili ya sehemu za patakatifu pa patakatifu, wahunzi wakayafunika kwa dhahabu. (Maandishi ya kale yanasema: makerubi wawili waliochongwa kwenye mbao).
11 And, as for the wings of the cherubim, the length of them, was twenty cubits, —the one wing, by the cubit was five, reaching to the wall of the house, and, the other wing, five cubits, reaching to the wing of the other cherub;
Mabawa ya makerubi yalikuwa na urefu wa mikono ishirini yote kwa pamoja; bawa la kerubi mmoja lilikuwa na urefu wa mikono mitano, lilifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa jingine lilikuwa na urefu wa mikono mitano pia.
12 and, the wing of the other cherub, was five cubits, reaching to the wall of the house, —and, the other wing, was five cubits, cleaving to the wing of the other cherub:
Bawa la kerubi mwingine lilikuwa mikono mitano, likifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa lake jingine lilikuwa mikono mitano pia, likigusana na bawa la kerubi wa kwanza.
13 the wings of these cherubim, outspread, were twenty cubits, —and, they themselves, were standing upon their feet, and, their faces, were inward.
Mabawa ya makerubi hawa yalienea jumla ya mikono mitano. Makerubi yalisimama kwa miguu yake, na nyuso zake zikiuelekea ukumbi mkuu.
14 And he made a vail, of blue and purple, and crimson and byssus cloth, —and raised thereon cherubim.
Akatengeneza pazia la samawati, dhambarau, na sufu nyekundu, na kitani safi, na akachora makerubi juu yake.
15 And he made, for the front of the house, two pillars, thirty five cubits in length, —and, the capital which was upon the top of each, was five cubits.
Selemani pia akatengeneza nguzo mbili, kila moja ikiwa na urefu wa mikono thelathini na tano kwenda juu, kwa maana mbele ya nyumba; taji ambazo zilikuwa juu ya nguzo zilikuwa na urefu wa mikono mitano kwenda juu.
16 And he made wreathen chains in the shrine, and put them upon the top of the pillars, —and he made one hundred pomegranates, and put them in the chains,
Akatengeneza minyororo kwa ajili ya nguzo na akaiweka juu yake, pia akatengeneza maakomamanga mia moja na akayaunganisha kwenye minyororo.
17 And he reared up the pillars in front of the temple, one, on the right, and, one, on the left, —and called the name of that on the right hand, Jachin, and the name of that on the left, Boaz.
Akazisimamisha nguzo mbele ya hekalu, mkono wa kulia, na nyingine mkono wa kushoto; akaiita nguzo ya kulia Yakini, na nguzo ya kushoto akaiita Boazi.

< 2 Chronicles 3 >