< 2 Chronicles 21 >

1 And Jehoshaphat slept with his fathers, and was buried with his fathers, in the city of David, —and Jehoram his son reigned in his steed.
Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
2 Now, he, had brethren, sons of Jehoshaphat—Azariah and Jehiel and Zechariah and Azariah, and Michael and Shephatiah, —all these, were sons of Jehoshaphat king of Israel,
Ndugu zake Yehoramu, wana wa Yehoshafati walikuwa: Azaria, Yehieli, Zekaria, Azaria, Mikaeli na Shefatia. Hawa wote walikuwa wana wa Yehoshafati mfalme wa Israeli
3 and their father gave them large presents—of silver and of gold and of precious things, with cities of defence, in Judah, —but, the kingdom, gave he unto Jehoram, for, he, was the firstborn.
Baba yao alikuwa amewapa zawadi nyingi za fedha na dhahabu na vitu vya thamani, pamoja na miji yenye ngome huko Yuda, bali ufalme akampa Yehoramu kwa sababu alikuwa mwanawe mzaliwa wa kwanza.
4 But, when Jehoram had arisen over the kingdom of his father, he strengthened himself, and slew all his brethren, with the sword, —moreover also some of the rulers of Israel.
Baada ya Yehoramu kujiimarisha katika ufalme wa baba yake, akawaua kwa upanga ndugu zake wote pamoja na baadhi ya wakuu wa Israeli.
5 Thirty-two years old, was Jehoram when he began to reign, —and, eight years, reigned he in Jerusalem.
Yehoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane.
6 And he walked in the way of the kings of Israel, like as did the house of Ahab, for, the daughter of Ahab, had he, to wife, —so he wrought wickedness, in the eyes of Yahweh.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana.
7 Howbeit Yahweh was not willing to destroy the house of David, because of the covenant which he had solemnised, unto David, —and as he had promised to give unto him a lamp, and unto his sons, all the days.
Hata hivyo, kwa sababu ya Agano ambalo Bwana alikuwa amefanya na Daudi, Bwana hakuwa radhi kuangamiza nyumba ya Daudi. Mungu alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili yake na wazao wake milele.
8 In his days, revolted the Edomites, from under the hand of Judah, —and set over themselves a king.
Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe.
9 So Jehoram passed over, with his captains, and all his chariot, with him, -and it came to pass that he rose up by night, and smote the Edomites that were round about unto him, and the chariot-captains.
Basi Yehoramu akaenda huko pamoja na maafisa wake na magari yake ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu.
10 So Edom revolted from under the hand of Judah—unto this day. Then, must Libnah needs revolt at the same time, from under his hand, —because he had forsaken Yahweh, the God of his fathers.
Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo kwa sababu Yehoramu alikuwa amemwacha Bwana, Mungu wa baba zake.
11 He too, made high places among the mountains of Judah, —and caused the inhabitants of Jerusalem to be unchaste, and seduced Judah.
Alikuwa pia ametengeneza mahali pa juu pa kuabudia miungu katika vilima vya Yuda na akawa amewasababisha watu wa Yerusalemu kufanya uzinzi na akawa amewapotosha watu wa Yuda.
12 Then came there unto him, a writing, from Elijah the prophet, saying, —Thus, saith Yahweh, God of David thy father, Because thou hast not walked in the ways of Jehoshaphat thy father, nor in the ways of Asa, king of Judah;
Yehoramu akapokea barua kutoka kwa nabii Eliya iliyosema: “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Daudi baba yako, asemalo: ‘Hukuenenda katika njia za Yehoshafati baba yako au za Asa mfalme wa Yuda.
13 but hast walked in the way of the kings of Israel, and hast caused Judah and the inhabitants of Jerusalem to be unchaste, after the unchastities of the house of Ahab, —moreover also, thine own brethren of the house of thy father who were better than thou, hast thou slain,
Lakini umeenenda katika njia za wafalme wa Israeli, nawe umewaongoza Yuda na watu wa Yerusalemu kuzini, kama vile nyumba ya Ahabu ilivyofanya. Pia umewaua ndugu zako mwenyewe, watu wa nyumbani mwa baba yako, watu waliokuwa bora kuliko wewe.
14 lo! Yahweh, is about to plague, with a great plague, thy people, -and thy children and thy wives, and all thy possessions;
Hivyo basi Bwana yu karibu kuwapiga watu wako, wanao, wake zako na kila kitu kilicho chako, kwa pigo zito.
15 also, thyself, with sore diseases, with disease of thy bowels, -until thy bowels shall fall out, by reason of the disease, in a year added to a year.
Wewe mwenyewe utaugua sana kwa ugonjwa wa tumbo kwa muda mrefu, hadi ugonjwa utakaposababisha matumbo yako kutoka nje.’”
16 And Yahweh stirred up against Jehoram the spirit of the Philistines, and the Arabians, who were under the direction of the Ethiopians;
Bwana akaamsha chuki ya Wafilisti na ya Waarabu walioishi karibu na Wakushi dhidi ya Yehoramu.
17 and they came up against Judah, and forced their way into it, and carried off all the possessions that were found belonging to the house of the king, moreover also his sons and his wives, —so that there was left him never a son, save only Jehoahaz the youngest of his sons.
Wakaishambulia Yuda, wakaivamia na kuchukua mali zote zilizopatikana katika jumba la mfalme pamoja na wanawe na wake zake. Hakubakiziwa mwana yeyote isipokuwa Ahazia aliyekuwa mdogo wa wote.
18 And, after all this, Yahweh plagued him in his bowels with an incurable disease.
Baada ya mambo haya yote, Bwana akampiga Yehoramu kwa ugonjwa usioponyeka wa matumbo.
19 And it came to pass, in a year beyond a year, even when the end of the days of two years had passed, that his bowels fell out by reason of his disease, so that he died, of, malignant disease, —and his people made him no burning, like the burning of his fathers.
Ikawa baada ya muda, mwisho wa mwaka wa pili, matumbo yake yakatoka nje kwa sababu ya ugonjwa, naye akafa katika maumivu makali sana. Watu wake hawakuwasha moto kwa heshima yake, kama walivyokuwa wamewafanyia baba zake.
20 Thirty-two years old, was he when he began to reign, and, eight years, reigned he in Jerusalem, —and went his way—unregretted, and, though they buried him in the city of David, yet, not in the sepulchres of the kings.
Yehoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipokuwa mfalme, naye akatawala huko Yerusalemu miaka minane. Akafa, bila kusikitikiwa na mtu yeyote, naye akazikwa katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.

< 2 Chronicles 21 >