< 2 Chronicles 18 >

1 And it came to pass, when Jehoshaphat had riches and honour, in abundance, that he contracted, by marriage, affinity with Ahab.
Basi, Yehoshafati alikuwa na mali nyingi sana na heshima. Naye akafanya urafiki na Ahabu kwa mwanawe kumwoa binti wa Ahabu.
2 So he went down, at the end of some years, unto Ahab, to Samaria, Ahab therefore sacrificed for him, sheep and oxen, in abundance, also for the people whom he had with him, -and then persuaded him to go up against Ramoth-gilead.
Baada ya miaka kadhaa akashuka kumtembelea Ahabu huko Samaria. Ahabu akachinja ngʼombe na kondoo wengi kwa ajili yake na watu aliokuwa amefuatana nao. Kisha Ahabu akamshawishi Yehoshafati kukwea pamoja naye ili kuishambulia Ramoth-Gileadi.
3 For Ahab king of Israel said unto Jehoshaphat king of Judah, Wilt thou go up with me to Ramoth-gilead? And he said unto him—So am I, even as thou, and, like thy people, are my people, and, with thee, in the war.
Ahabu mfalme wa Israeli akamuuliza Yehoshafati mfalme wa Yuda, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako. Tutakuwa pamoja nawe vitani.”
4 Then said Jehoshaphat, unto the king of Israel, —Seek, I pray thee, some time to-day, the word of Yahweh.
Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
5 So the king of Israel gathered together the prophets, four hundred men, and said unto them, Shall we go up against Ramoth-gilead to battle, or shall I forbear? And they said—Go up, and may God deliver it into the hand of the king!
Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda kwa kuwa Mungu ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
6 Then said Jehoshaphat, Is there not here a prophet of Yahweh, besides, —that we may seek, from him?
Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
7 Then said the king of Israel unto Jehoshaphat—There is yet one man, by whom to seek Yahweh, but, I, hate him, for he is never prophesying, concerning me, anything good—but—all his days—evil, the same, is Micaiah, son of Imla. Then said Jehoshaphat, Let not the king say, so!
Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
8 And the king of Israel called for a certain officer, —and said, Haste, Micaiah son of Imla!
Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
9 Now, the king of Israel, and Jehoshaphat king of Judah, were sitting, each upon his throne, clothed in robes, and they were sitting in an open space, at the entrance of the gate of Samaria, —and, all the prophets, were prophesying before them.
Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
10 Then did Zedekiah son of Chenaanah make him horns of iron, —and said—Thus, saith Yahweh, With these, shalt thou push Syria, until they are consumed.
Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
11 And, all the prophets, were prophesying, so, saying, -Go up to Ramoth-gilead, and prosper, and Yahweh will deliver [it] into the hand of the king.
Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho, wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
12 And, the messenger who went to call Micaiah, spake unto him, saying, Lo! the words of the prophets, with one mouth, are good for the king, —be thy word then, I pray thee, like one of theirs, so wilt thou speak good.
Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
13 Then said Micaiah, —By the life of Yahweh, whatsoever my God shall say, that, must I speak.
Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
14 Now, when he came unto the king, the king said unto him, Micah, shall we go against Ramoth-gilead to battle, or shall I forbear? And he said, Go ye up and prosper, and may they be delivered into your hand.
Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa watatiwa mkononi mwako.”
15 Then the king said unto him, How many times, must, I, be putting thee on oath, —that thou speak unto me nothing but the truth in the name of Yahweh?
Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
16 So he said, I saw all Israel, scattered upon the mountains, like sheep that have no shepherd, -and Yahweh said, No masters, have these! let them return every man unto his own house, in peace.
Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
17 Then said the king of Israel, unto Jehoshaphat, —Said I not unto thee, He wilt not prophesy concerning me anything good, but evil?
Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu bali mabaya tu?”
18 Then said he, Therefore, hear ye the word of Yahweh, —I saw Yahweh, sitting upon his throne, and, all the host of the heavens, standing, on his right hand and his left.
Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama upande wa kulia na wa kushoto.
19 Then said Yahweh, Who will persuade Ahab king of Israel, that he may go up and fall in Ramoth-gilead? And one spake, saying after this manner, and another, saying after that manner.
Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu, mfalme wa Israeli, ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
20 Then came there forth a spirit and stood before Yahweh, and said, I, will persuade him. And Yahweh said unto him, Wherewith?
Mwishoni, roho akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’ “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’
21 And he said, I will go forth and become a spirit of falsehood, in the mouth of all his prophets. And he said—Thou mayest persuade, moreover also, thou shalt prevail, go forth, and do, so.
“Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
22 Now, therefore, lo! Yahweh hath suffered a spirit of falsehood to be put into the mouth of these thy prophets, —but, Yahweh, hath spoken concerning thee—evil.
“Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
23 Then drew near Zedekiah son of Chenaanah, and smote Micaiah upon the cheek, —and said, Which then is the way the spirit of Yahweh passed from me, to speak with thee?
Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
24 Then said Micaiah, Lo! thou shalt see, on that day when thou shalt enter into a chamber within a chamber, to hide thyself.
Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
25 Then said the king of Israel, Take ye Micaiah, and carry him back unto Amon ruler of the city, and unto Joash son of the king;
Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
26 and ye shall say, Thus, saith the king, Put ye this one into the prison, —and feed him with the bread of oppression, and with the water of oppression, until I return in peace.
Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
27 Then said Micaiah, If thou do, at all return, in peace, Yahweh hath not spoken by me. And he said, Hear! ye peoples, all!
Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
28 Then went up the king of Israel, and Jehoshaphat king of Judah, against Ramothgilead.
Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
29 And the king of Israel said unto Jehoshaphat, [I am about] to disguise myself, and enter into the battle, but, thou, put on thy robes. So the king of Israel disguised himself, and entered into the battle.
Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
30 Now, the king of Syria, had commanded the captains of chariots which he had, saying, Ye shall not fight, with small [or] with great, —save with the king of Israel, alone.
Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
31 So it came to pass, when the chariot-captains saw Jehoshaphat, that, they, said, The king of Israel, it is. And they compassed him about, to fight, —but Jehoshaphat made outcry, and, Yahweh, helped him, yea God allured them away from him.
Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati, wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele, naye Bwana akamsaidia. Mungu akawaondoa kwake,
32 And so it came to pass, when the chariot-captains saw that it was not the king of Israel, that they turned back from pursuing him;
wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli nao wakaacha kumfuatilia.
33 but, a certain man, drawing a bow in his innocence, smote the king of Israel between the shoulder-joints and the coat of mail, —wherefore he said to the charioteer, Turn thy hand, and convey me out of the host, for I am sore wounded.
Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma, mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
34 But the battle increased on that day, and, the king of Israel, was propping himself up in the chariot before the Syrians, until evening, -and died at the time of the going in of the sun.
Vita vikaendelea mchana kutwa, naye mfalme wa Israeli akajitegemeza ndani ya gari lake kuwaelekea Waaramu hadi jioni. Basi jioni yake akafa.

< 2 Chronicles 18 >