< 2 Chronicles 17 >

1 And Jehoshaphat his son reigned in his stead, —and strengthened himself against Israel;
Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake na akajiimarisha dhidi ya Israeli.
2 and put forces in all the fortified cities of Judah, —and set garrisons in the land of Judah, and in the cities of Ephraim, which Asa his father had captured.
Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka.
3 And it came to pass, that, Yahweh, was with Jehoshaphat, —because he walked in the first ways of David his father, and sought not unto the Baalim;
Bwana Mungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake ya mwanzoni alienenda katika njia za Daudi baba yake. Hakutafuta Mabaali
4 for, unto the God of his father, he sought, and, in his commandments, he walked, —and not according to the doing of Israel.
bali alimtafuta Mungu wa baba yake na kuzifuata amri zake badala ya kufuata desturi za watu wa Israeli.
5 Therefore did Yahweh establish the kingdom in his hand, and all Judah gave a present unto Jehoshaphat, —and he came to have riches and honour, in abundance.
Kwa hiyo Bwana akauimarisha ufalme chini ya uongozi wake, nao Yuda wote wakamletea Yehoshafati zawadi, hivyo akawa na utajiri mwingi na heshima.
6 And his heart was encouraged, in the ways of Yahweh, —and he, yet further, took away the high places and the Sacred Stems, out of Judah.
Moyo wake ukawa hodari katika njia za Bwana na zaidi ya yote, akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na nguzo za Maashera katika Yuda.
7 And, in the third year of his reign, he sent to his rulers, even to Ben-hail and to Obadiah and to Zechariah, and to Nethanel, and to Micaiah, —that they were to teach throughout the cities of Judah;
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa akatuma maafisa wake ambao ni: Ben-Haili, Obadia, Zekaria, Nethaneli na Mikaya ili kufundisha katika miji ya Yuda.
8 and, with them, Levites, Shemaiah and Nethaniah and Zebadiah and Asahel and Shemiramoth and Jehonathan, and Adonijah and Tobijah and Tob-adonijah, Levites, —and, with them, Elishama and Jehoram, priests;
Pamoja nao walikuwepo Walawi fulani nao ni: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, Tob-Adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
9 and they taught throughout Judah, and, with them, was the book of the law of Yahweh, —so they went round throughout all the cities of Judah, and taught the people.
Wakafundisha Yuda yote, wakiwa wamechukua Kitabu cha Sheria ya Bwana wakazunguka miji yote ya Yuda na kufundisha watu.
10 And it came to pass, that, the dread of Yahweh, was upon all the kingdoms of the countries, that were round about Judah, —and they warred not against Jehoshaphat.
Hofu ya Bwana ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda, hivyo hawakufanya vita na Yehoshafati.
11 And, from among the Philistines, were they bringing in unto Jehoshaphat a present, and silver as tribute, —even the Arabians, were bringing in unto him flocks, seven thousand seven hundred rams, and seven thousand seven hundred he-goats.
Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi na fedha kama ushuru, nao Waarabu wakamletea mifugo: kondoo dume 7,700 na mbuzi 7,700.
12 And so it came to pass that, Jehoshaphat, went on waxing surpassingly great, —and he built, throughout Judah, fortresses and cities for store;
Yehoshafati akaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi, akajenga ngome na miji ya hazina katika Yuda
13 and, much business, had he, throughout the cities of Judah, —but, the men of war, the heroes of valour, were in Jerusalem.
na akawa na wingi mkubwa wa vitu katika miji ya Yuda. Pia aliweka askari wa vita wenye uzoefu huko Yerusalemu.
14 And, these, are the numbers of them, by their ancestral house, —To Judah, pertained rulers of thousands, Adnah the chief, and, with him, mighty men of valour, three hundred thousand;
Wakaandikishwa katika jamaa zao kama ifuatavyo: Kutoka Yuda, majemadari wa vikosi vya elfu: Jemadari Adna akiwa na askari wa vita 300,000;
15 and, under his direction, was Jehohanan the chief, —and, with him, two hundred and eighty thousand;
aliyefuata ni jemadari Yehohanani, akiwa na askari 280,000 walio tayari kwa vita;
16 and, under his direction, Amasiah son of Zichri, who willingly offered himself unto Yahweh, —and, with him, two hundred thousand heroes of valour.
aliyefuata ni Amasia mwana wa Zikri, ambaye alijitolea kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiwa na askari 200,000.
17 And, out of Benjamin, a hero of valour, Eliada, —and, with him, armed with bow and buckler, two hundred thousand;
Kutoka Benyamini: Eliada, askari shujaa akiwa na watu 200,000 wenye silaha za nyuta na ngao;
18 and, under his direction, Jehozabad, —and, with him, a hundred and eighty thousand, equipped for war.
aliyefuata ni Yehozabadi, akiwa na askari 180,000 wenye silaha za vita.
19 These, were they who were waiting upon the king, —besides those whom the king placed in the fortified cities, throughout all Judah.
Hawa ndio waliomtumikia mfalme, mbali na wale mfalme aliweka katika miji yenye ngome huko Yuda yote.

< 2 Chronicles 17 >