< 2 Chronicles 13 >

1 In the eighteenth year of King Jeroboam, began Abijah to reign over Judah:
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
2 three years, reigned he in Jerusalem, and, the name of his mother, was Maacah, daughter of Uriel of Gibeah, —and there was, war, between Abijah and Jeroboam.
naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea. Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
3 And Abijah began the war with a force of heroes of war, four hundred thousand chosen men, —and, Jeroboam, set in array against him to battle, with eight hundred thousand chosen men, heroes of valour.
Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.
4 And Abijah stood up upon Mount Zemaraim, which is in the hill country of Ephraim, —and said, Hear me, O Jeroboam and all Israel!
Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi!
5 Is it not yours to know, that, Yahweh God of Israel gave the kingdom to David, over Israel, unto times age-abiding, —to him and to his sons, by a covenant of salt?
Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi?
6 Yet hath Jeroboam son of Nebat, servant of Solomon son of David, risen up, —and rebelled against his lord.
Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake.
7 And there are gathered unto him vain men, sons of the Abandoned One, who emboldened themselves against Rehoboam son of Solomon, -when, Rehoboam, was young and tender of heart, and had not strengthened himself to meet them.
Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.
8 Now, therefore, ye, are thinking to strengthen yourselves against the kingdom of Yahweh, in the hand of the sons of David, —and, ye, are a great multitude, and, with you, are calves of gold, which Jeroboam hath made you for gods.
“Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu.
9 Have ye not driven out the priests of Yahweh, the sons of Aaron, and the Levites, —and made for yourselves priests like the peoples of the countries? Whosoever cometh to install himself with a young bullock, and seven rams, then becometh he a priest unto the, no-gods.
Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.
10 But, as for us, Yahweh, is our God, and we have not forsaken him, —and, the priests who are waiting upon Yahweh, are sons of Aaron, with Levites in the work;
“Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia.
11 and they are making a perfume unto Yahweh, with ascending-sacrifices morning by morning, and evening by evening and an incense of sweet spices, and are putting in order bread upon the pure table, and the lampstand of gold with the lamps thereof, for lighting up evening by evening, for, observant, are we of the charge of Yahweh our God, —whereas, ye, have forsaken him.
Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu.
12 And lo! with us as Head, is God himself, and his priests, and the trumpets of alarm, to sound an alarm against you, —O sons of Israel! do not fight against Yahweh God of your fathers, for ye shall not prosper.
Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”
13 But, Jeroboam, sent round an ambush, to come up from behind them, —so they were before Judah and, the ambush, did come up from behind them.
Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma.
14 And, when Judah turned and lo! as for them, the battle was before and behind, then made they outcry unto Yahweh, —and, the priests, kept on blowing with the trumpets.
Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao,
15 Then the men of Judah gave a shout, —and it came to pass, when the men of Judah shouted, then, God himself, smote Jeroboam and all Israel, before Abijah and Judah.
nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda.
16 And the sons of Israel fled from before Judah, —and God delivered them into their hand.
Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao.
17 And Abijah and his people smote among them with a great smiting, —and there fell down slain, of Israel, five hundred thousand chosen men.
Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli.
18 Thus were the sons of Israel subdued at that time, —and the sons of Judah prevailed, because they leaned upon Yahweh the God of their fathers.
Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
19 And Abijah pursued after Jeroboam, and captured from him, cities, even Bethel, with the villages thereof, and Jeshanah, with the villages thereof, —and Ephron, with the villages thereof;
Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo.
20 neither was Jeroboam strong any more, in the days of Abijah, —and Yahweh smote him that he died.
Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.
21 And Abijah strengthened himself, and took him, fourteen wives, —and begat twenty-two sons, and sixteen daughters.
Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.
22 And, the rest of the story of Abijah, both his ways and his words, —are written, in the commentary of the prophet Iddo.
Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.

< 2 Chronicles 13 >