< 1 Timothy 1 >

1 Paul, an apostle of Christ Jesus—by injunction of God our Saviour and Christ Jesus our hope, —
Mimi Paulo, mtume wa Yesu Kristo kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na Yesu Kristo tumaini letu,
2 unto Timothy, my true child in faith: favour, mercy, peace, from God our Father, and Christ Jesus our Lord.
nakuandikia Timotheo mwanangu halisi katika imani. Nakutakia neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Kristo Yesu Bwana wetu.
3 Even as I exhorted thee to remain in Ephesus, when I was journeying into Macedonia, that thou mightest charge some—
Napenda ukae huko Efeso, kama nilivyokuomba nilipokuwa ninakwenda Makedonia. Wako watu fulani huko wanaofundisha mafundisho ya uongo. Wakomeshe watu hao.
4 Not to be teaching otherwise, nor yet to be giving heed to stories and endless genealogies, —the which, bring, arguings, rather than that stewardship of God which is with faith; —
Waambie waachane na zile hadithi tupu na orodha ndefu za mababu, ambazo huleta tu ubishi, wala haviwajengi watu katika mpango ujulikanao kwa imani.
5 Now, the end of the charge, is love—out of a pure heart, and a good conscience, and faith unfeigned, —
Shabaha ya amri hii ni kuhimiza mapendo yatokayo katika moyo safi, dhamiri njema, na imani ya kweli.
6 Which some, missing, have turned them aside unto idle talk,
Watu wengine wamepotoka na kugeukia majadiliano yasiyo na maana.
7 Desiring to be law-teachers, —not understanding, either what they say or whereof they confidently affirm.
Wanapenda kuwa walimu wa Sheria, lakini hawaelewi maneno yao wenyewe au mambo wanayosisitiza.
8 Now we know that, excellent, is the law, if one put it to a lawful use: —
Twajua kwamba Sheria ni njema, kama ikitumiwa ipasavyo.
9 Knowing this—that, to a righteous man, law, doth not apply, but to the lawless and insubordinate, ungodly and sinful, irreligious and profane, smiters of fathers and smiters of mothers, murderers,
Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba sheria haziwekwi kwa ajili ya watu wema, bali kwa ajili ya wahalifu na wasiotii, wasiomcha Mungu na wenye dhambi, watu wasio na dini na wa kidunia. Watu wanaowaua baba na mama zao, au wauaji wowote wale;
10 fornicators, sodomites, man-stealers, liars, false- swearers, —and, if anything else, unto the healthful teaching, is opposed; —
sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wafiraji, wanaowaiba watu, waongo, na wanaoapa uongo au wanaofanya chochote ambacho ni kinyume cha mafundisho ya kweli.
11 According to the glad-message of the glory of the happy God, with which entrusted am, I.
Mafundisho hayo hupatikana katika Habari Njema ambayo mimi nimekabidhiwa niihubiri, Habari Njema ya Mungu mtukufu na mwenye heri.
12 Grateful, am I unto him that empowered me, Christ Jesus our Lord, in that, faithful, he accounted me, putting me into ministry, —
Namshukuru Bwana wetu Yesu Kristo aliyenipa nguvu kwa ajili ya kazi yangu. Namshukuru kwa kuniona mimi kuwa ni mwaminifu, akaniteua nimtumikie,
13 Though, formerly, a defamer, and persecutor, and insulter; nevertheless mercy was shown me, because, without knowledge, I acted, in unbelief:
ingawa pale awali mimi nilimtukana na kumtesa na kumdhulumu. Lakini Mungu alinionea huruma, kwa sababu sikuwa na imani bado, na hivyo sikujua nilichokuwa ninafanya.
14 Yet exceeding abundant was the favour of our Lord, with faith and love which are in Christ Jesus.
Lakini Bwana wetu alinijalia neema yake kwa wingi, akanipa imani na upendo katika kuungana na Kristo Yesu.
15 Faithful, the saying! and, of all acceptance, worthy, —that, Christ Jesus, came into the world, sinners, to save: of whom, the chief, am, I;—
Usemi huu ni wa kuaminika, na tena unafaa kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wenye dhambi. Nami ni mkosefu zaidi kuliko hao wote,
16 Nevertheless, on this account, was mercy shewn me, —that, in me, the chief, Christ Jesus might shew forth his entire longsuffering, for an ensample of them about to believe on him unto life age-abiding. (aiōnios g166)
lakini Mungu alinionea huruma, ili Kristo aonyeshe uvumilivu wake wote kwangu mimi, kama mfano kwa wale wote ambao baadaye watamwamini na kupokea uzima wa milele. (aiōnios g166)
17 Now, unto the King of the ages, —incorruptible, invisible, alone God, be honour and glory, unto the ages of ages, Amen! (aiōn g165)
Kwake yeye aliye Mfalme wa milele na asiyekufa, yeye aliye Mungu pekee—kwake viwe heshima na utukufu milele na milele! Amina. (aiōn g165)
18 This charge, I commit unto thee, child Timothy, According to the prophecies, running before on thee, in order that thou mightest war, with them, the noble warfare.
Mwanangu Timotheo, nakukabidhi amri hii kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Yatumie maneno hayo yawe silaha yako katika kupigana vita vizuri,
19 Holding faith and a good conscience, —which some, thrusting from them, concerning their faith, have made shipwreck: —
na ushike imani yako na dhamiri njema. Watu wengine hawakusikiliza dhamiri zao na hivyo wakaiharibu imani yao.
20 Of whom are Hymenaeus and Alexander; whom I have delivered unto Satan, that they may be taught by discipline not to be defaming.
Miongoni mwao ni Humenayo na Aleksanda ambao nimewakabidhi kwa Shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.

< 1 Timothy 1 >