< 1 Kings 6 >

1 And so it came to pass, in the four hundred and eightieth year, by the coming forth of the sons of Israel out of the land of Egypt, in the fourth year (in the month of Zif, the same, being the second month) of the reign of Solomon over Israel, that he began to build the house unto Yahweh.
Kwa hiyo Sulemani akaanza kulijenga hekalu. Hii ilikuwa mwaka wa 480 baada ya wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Sulemani huko Israeli, katika mwezi wa Ziv, ambao ndio mwezi wa pili.
2 Now, the house which King Solomon built unto Yahweh, was sixty cubits in length, and twenty in breadth, —and thirty cubits in height.
Hekalu ambalo mfalme Sulemani alimjengea BWANA lilikuwa na urefu wa mita 27, na upana wa mita 9, na kimo cha mita 13. 5.
3 And, the porch in front of the temple of the house, was twenty cubits in length, according to the breadth of the house, —ten cubits in breadth, in front of the house.
Na ukumbi uliokuwa mbele ya hekalu ulikuwa na urefu wa mita 9 na upana wa mita 4. 5 sawa na upana wa sehemu kuu ya hekalu.
4 And he made to the house windows, with closed bars.
Lile hekalu alilitengenezea madirisha ambayo fremu zake kwa nje yalifanya yaonekane membamba kuliko ile sehemu ya ndani.
5 And he built—by the wall of the house—a gallery, round about, against the walls of the house, round about, both to the temple, and to the shrine, —and he made side chambers round about.
Na ukuta wa nyumba aliuzungushia vyumba kuzunguka pande zake, kushikamana na vyumba vya nje na vya ndani ya hekalu. Akajenga vyumba katika pande zote.
6 The, lowest gallery, was five cubits broad, and, the middle, six cubits broad, and, the third, seven cubits broad, —for he put, ledges, against the house round about, on the outer side, so as not to make fastenings in the walls of the house.
Kile chumba cha chini kilikuwa na upana wa mita 2. 3, kile cha kati kilikuwa na upana wa mita 2. 8. na kile cha tatu kilikuwa na upana wa mita 3. 2. upande wa nje akaupunguza ukuta wa nyumba pande zote, ili boriti zisishikamane ukutani mwa nyumba.
7 Now, the house, when it was in building, with whole quarry-stones, was built, —neither hammer, nor axe, nor any tools of iron, was heard in the house, when it was in building.
Hekalu lilijengwa kwa mawe yaliyokuwa yamechongwa chimboni. Hakuna nyundo, wala shoka au chombo chochote cha chuma kilisikika wakati hekalu lilipokuwa likjengwa.
8 The entrance of the lowest story, was on the right side of the house, —and, by winding stairs, went they up unto the middle [story], and, out of the middle, into, the third.
Upande wa kusini wa hekalu kulikuwa na lango la chini, ambalo mtu hupanda kwa madaraja mpaka juu kwenye chumba cha kati, na kutoka chumba cha kati hadi chumba cha tatu.
9 So he built the house, and finished it, —and ceiled the house with planks and beams of cedar;
Kwa hiyo Sulemani akalijenga hekalu mpaka akalimaliza, akalifunika hekalu kwa boriti na mbao za mwerezi.
10 and built the gallery against all the house, five cubits in height, —and so fastened the house, with timber of cedar.
Akajenga vyumba vya pembeni mwa hekalu, kila upande mita 2. 3 kwenda juu. Navyo vikaunganishwa na hekalu kwa mbao za mierezi.
11 Then came the word of Yahweh unto Solomon, saying:
Neno la BWANA likamjia Sulemani, likisema,
12 Concerning this house, which thou art building, If thou wilt walk in my statutes, and, my regulations, wilt practise, and so observe all my commandments, by walking in them, Then will I establish my word with thee, which I spake unto David thy father;
“Kuhusu hili hekalu ambalo unajenga, kama utatatembea katika maagizo yangu na kuhukumu kwa haki, na kutunza amri zangu na kuishi kwa hizo, ndipo ntakapozithibitisha ahadi zangu na wewe ambazo niliziahidi kwa baba yako Daudi.
13 and will make my habitation in the midst of the sons of Israel, —and will not forsake my people Israel.
Nitaishi kati ya watu wa Israeli nami sitawatupa.”
14 Thus Solomon built the house, and finished it;
Kwa hiyo Sulemani akalijenga hekalu mpaka akalimaliza.
15 and he built the walls of the house on the inside, with boards of cedar, from the floor of the house, unto the cross-beams of the ceiling, he overlaid it with wood, on the inside, —and he overlaid the floor of the house with boards of fir.
Kisha akajenga kuta za ndani za hekalu kwa mbao za mwerezi. Kuanzia sakafu ya hekalu hadi boriti za juu, kwa ndani akazifunika kwa miti, na akaifunika sakafu kwa mbao za miberoshi.
16 And he built twenty cubits, at the hinder part of the house, with boards of cedar, from the floor as far as the cross-beams, —and he built it within, for a shrine, even for the holy of holies;
Alijenga mita 9 ndani ya hekalu kwa mbao za miberoshi kutoka sakafuni hadi juu. Hiki ni chumba cha ndani, cha patakatifu sana.
17 but, forty cubits, was the house itself, —the same, was the temple, before the oracle.
Ule ukumbu mkuu, ulikuwa mahali pakatifu amabao ulikuwa mbele ya patakatifu sana, ulikuwa wa mita 18. hapo kulikwa na mbao za mwerezi ndani ya hekalu, zilizokuwa zimechongwa kwa sura ya vibuyu na maua yaliyochanua.
18 And, the cedar for the house within, was carved with colocynths, and with festoons of flowers, —the whole, was cedar, there was no stone to be seen.
Zote zilikuwa za mierezi kwa ndani. Hapakuonekana chochote ndani kilichokuwa kimetengenezwa kwa mawe.
19 And, the shrine in the midst of the house within, made he ready, —for placing there, the ark of the covenant of Yahweh.
Sulemani alitengeneza kile chumba cha ndani kwa lengo la kuweka sanduku la agano la BWANA.
20 And, the interior of the shrine, was twenty cubits in length, and twenty cubits in breadth, and twenty cubits in height, and he overlaid it, with pure gold, —and overlaid the altar with cedar.
Kile chumba cha ndani kilikuwa na upana wa mita 9, na kimo cha mita 9. Sulemani alizifunika kuta kwa dhabahu na madhabahu aliifunika kwa mbao za mierezi.
21 Thus then did Solomon overlay the house within, with pure gold, —and he drew chains of gold across the front of the shrine, and overlaid it with gold;
Sulemani alifunika ndani ya hekalu kwa dhahabu safi na akaweka mikufu ya dhahabu iliyopita mbele ya chumba cha ndani, na kulifunika eneo la mbele kwa dhabahu.
22 yea, all the house, overlaid he with gold, until he had made all the house into one whole, —even all the altar that was by the shrine, overlaid he with gold.
Akalisakafia kwa dhahabu eneo lote la ndani mpaka akamaliza hekalu lote. Pia akalisakafia kwa dhahabu madhahabu yote ya chumba cha ndani.
23 And he made, within the shrine, two cherubim of wild olive wood, —ten cubits in height;
Sulemani akatengeneza makerubi mawili kwa mbao za mizeituni, kila moja lilikuwa na kimo cha mita 4. 5 kwa ajili ya chumba cha ndani.
24 and, five cubits, was the one wing of the cherub, and, five cubits, the second wing of the cherub, —ten cubits, from the one end of his wings unto the other end of his wings.
Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa mita 2. 3. Kwa hiyo kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa lingine kulikuwa na umbali wa mita 4. 5. Yule
25 Ten cubits, also was the second cherub, —of one size and one shape, were the two cherubim.
kerubi mwingine naye alikuwa na bawa lenye kipimo cha mita 4. 5 Makerubi hawa walikuwa wanafanana kwa umbo na kwa vipimo.
26 The height of the one cherub, was ten cubits, —and, so, of the second cherub.
Kimo cha kerubi mmoja kilikuwa mita 4. 5 na yule wa pili alikuwa hivyo hivyo.
27 And he placed the cherubim in the midst of the inner house, and the cherubim stretched forth their wings, —so that the wing of the one touched the [one] wall, and the wing of the other cherub, was touching the other wall, —and, their wings in the midst of the house, were touching, wing to wing.
Sulemani aliwaweka hao kerubi kwenye chumba cha patakatifu sana. Bawa moja la kerubi lilikuwa limeenea kiasi kwamba bawa moja liligusa ukuta huu na bawa la yule wa pili nalo liligusa ukuta wa upande mwingine. Hayo mabawa yalikuwa yanakutana katikati ya chumba cha patakatifu sana.
28 And he overlaid the cherubim with gold.
Sulemani aliwafunika hao kerubi kwa dhahabu.
29 And, all the walls of the house round about, carved he with figures of cherubim, and palm-trees, and festoons of flowers, —within and without.
Akazinakshi kuta zote kwa sura za makerubi, miti ya mitende, na maua yaliyochanua, kwa vyumba vya nje na vya ndani.
30 Even the floor of the house, overlaid he with gold, —within and without.
Sulemani akalisakafia hekalu kwa dhahabu, kwa vyumba vyote vya ndani na vya nje.
31 And, the entrance of the shrine, made he with doors, of wild olive-wood, the pillars and posts being a fifth.
Sulemani akatengeneza milango ya mbao za mizeituni kwenye lango la kuingia ndani. Aliweka vizingiti na miimo kwenye pande tano.
32 The two doors, also were of olive-wood, and he carved upon them carvings of cherubim, and palm-trees, and festoons of flowers, and overlaid them with gold, —yea he spread out, over the cherubim and over the palm-trees, the gold.
Kwa hiyo akatengeneza na milango miwili ya mizeituni, na akainakshi kwa makerubi, na mitende, na maua yaliyochanua. Akasakafia kwa dhahabu na akatandaza dhahabu kwenye makerubi na kwenye mitende.
33 So, also, made he for the entrance of the temple, with posts of wild olive-wood, —a fourth part.
Kwa njia hii, akalitengenezea hekalu miimo miwili ya mbao za mizeituni yenye pande nne
34 And, the two doors, were of fir wood, —the two leaves of the one door, were folding, and, the two leaves of the other door, were folding.
na milango miwili ya mbao za mierezi. Zile mbao mbili za mlango mmoja zilikuwa zikijikunja na mbao mbili za mlango wa pili nazo zilikuwa zikijikunja pia.
35 And he carved cherubim, and palm-trees, and festoons of flowers, and overlaid them with gold, smoothed out on the carved work.
Akazinakshi kwa makerubi, mitende, na maua yaliyochanua, na pia akazisakafia kwa dhahabu juu ya zile nakshi.
36 And he built the inner court, with three rows of hewn stone, —and a row of beams of cedar.
Akalijengs Korido la ndani kwa safu tatu za mawe ya kuchongwa na safu moja ya mhimili wa mierezi.
37 In the fourth year, was laid the foundation of the house of Yahweh, —in the month Zif;
Msingi wa hekalu ulijengwa katika mwaka wa nne, wa mwezi wa Ziv.
38 and, in the eleventh year, in the month Bul—the same, is the eighth month, was the house finished, as to all the particulars thereof, and as to all the appointments thereof, —so then he built it in seven years.
Mwaka wa kumi na moja mwezi wa Buli, ambao ndio mwezi wa nane, sehemu zote za hekalu zilimalizika na sharti zake zote. Sulemani alilijenga hekalu kwa miaka saba.

< 1 Kings 6 >