< 1 Kings 2 >

1 And, when the days of David drew near that he must die, he charged Solomon his son, saying: —
Siku zilipokaribia za Daudi kufa, akampa mwanawe Solomoni agizo.
2 I, am going the way of all the earth, —thou must be strong, therefore, and show thyself a man;
Akasema, “Mimi ninakaribia kwenda njia ya dunia yote. Hivyo uwe hodari, jionyeshe kuwa mwanaume,
3 and keep the observances of Yahweh thy God, by walking in his ways, by keeping his statutes, his commandments, and his regulations and his testimonies, as written in the law of Moses, —to the end thou mayest prosper in all that thou doest, and whithersoever thou turnest thyself;
shika lile Bwana Mungu wako analokuagiza: Enenda katika njia zake, ushike maagizo na amri zake, sheria zake na kanuni zake, kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, ili upate kustawi katika yote ufanyayo na popote uendako,
4 to the end that Yahweh may establish his word which he spake concerning me, saying, If thy sons will take heed to their way, by walking before me, in truth, with all their heart, and with all their soul, (then, said he) there shall not be cut off to thee a man, from off the throne of Israel.
ili kwamba Bwana aweze kunitimizia ahadi yake: ‘Kama wazao wako wakiangalia sana wanavyoishi, na kama wakienenda kwa uaminifu mbele zangu kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote, kamwe hutakosa kuwa na mtu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.’
5 Moreover also, thou, knowest what Joab son of Zeruiah did to me, how he dealt with two generals of the armies of Israel—with Abner son of Ner, and with Amasa son of Jether—both of whom he slew, shedding the blood of war in peace, —and putting the blood of war upon his girdle that was on his loins, and upon his sandals, that were on his feet.
“Sasa wewe mwenyewe unafahamu lile Yoabu mwana wa Seruya alilonitendea, lile alilofanya kwa majemadari wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri mwana wa Neri, na Amasa mwana wa Yetheri. Aliwaua, akimwaga damu yao wakati wa amani kama vile ni kwenye vita, tena akaipaka damu ile kwenye mkanda uliokuwa kiunoni mwake na viatu alivyovaa miguuni mwake.
6 Thou, therefore, must do according to thy wisdom, —but will not let his grey hair go down in peace, to hades. (Sheol h7585)
Shughulika naye kwa kadiri ya hekima yako, lakini usiache kichwa chake chenye mvi kishukie kaburi kwa amani. (Sheol h7585)
7 But, with the sons of Barzillai the Gileadite, thou wilt deal in lovingkindness, and they will be among them who eat at thy table, —for, so, drew they near unto me, when I fled from Absolom thy brother.
“Lakini uwaonyeshe wema wana wa Barzilai wa Gileadi na uwaruhusu wawe miongoni mwa wale walao mezani pako. Walisimama nami nilipomkimbia ndugu yako Absalomu.
8 Lo! also, there is with thee—Shimei son of Gera a Benjamite, of Behurim, well, he, it was who cursed me with a grievous curse; on the day I journeyed to Mahanaim, —but he, came down to meet me, at the Jordan, and so I sware to him by Yahweh, saying—I will not put thee to death, with the sword.
“Ukumbuke, unaye Shimei mwana wa Gera, Mbenyamini kutoka Bahurimu, ambaye alinilaani kwa laana kali siku niliyokwenda Mahanaimu. Aliposhuka kunilaki huko Yordani, nilimwapia kwa Bwana: ‘Sitakuua kwa upanga!’
9 Now, therefore do not hold him guiltless, for, a wise man, thou art, and wilt know how thou oughtest to deal with him, and wilt suffer his grey hairs to go down with blood, to hades. (Sheol h7585)
Lakini sasa, usidhani kwamba hana hatia. Wewe ni mtu wa hekima, utajua la kumtendea. Zishushe mvi zake kaburini kwa damu.” (Sheol h7585)
10 So then David slept with his fathers, —and was buried in the city of David.
Kisha Daudi akapumzika pamoja na baba zake naye akazikwa katika Mji wa Daudi.
11 Now, the days that David reigned over Israel, were forty years, —in Hebron, reigned he seven years, and, in Jerusalem, reigned he thirty and three years.
Daudi alikuwa ametawala juu ya Israeli miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.
12 But, when, Solomon, took his seat upon the throne of David his father, then was the kingdom firmly established.
Kwa hiyo Solomoni akaketi katika kiti cha ufalme cha baba yake Daudi, nao utawala wake ukaimarika sana.
13 And Adonijah son of Haggith came in unto Bath-sheba, mother of Solomon: And she said—Peaceably, comest thou? And he said—Peaceably.
Basi Adoniya, mwana wa Hagithi, akaenda kwa Bathsheba, mama yake Solomoni. Bathsheba akamuuliza, “Je, umekuja kwa amani?” Akajibu, “Ndiyo, kwa amani.”
14 Then said he—I have somewhat to say unto thee. And she said—Say on.
Kisha akaongeza, “Ninalo jambo la kukuambia.” Akajibu, “Waweza kulisema.”
15 And he said—Thou, knowest that, mine, was the kingdom, and, on me, had all Israel set their faces, that I should become king, —howbeit the kingdom, hath turned about, and become my brother’s, for, from Yahweh, became it, his.
Akasema, “Kama unavyojua, ufalme ulikuwa wangu. Israeli wote waliniangalia mimi kama mfalme wao. Lakini mambo yalibadilika, ufalme umekwenda kwa ndugu yangu, kwa maana umemjia kutoka kwa Bwana.
16 Now, therefore, one request, have I to ask of thee, do not turn away my face.
Sasa ninalo ombi moja ninalokuomba. Usinikatalie.” Bathsheba akasema, “Waweza kuliomba.”
17 And she said unto him—Say on. And he said—Speak, I pray thee, unto Solomon the king, for he will not turn away thy face, —that he give me Abishag the Shunammite, to wife.
Kwa hiyo akaendelea kusema, “Tafadhali mwombe Mfalme Solomoni, anipatie Abishagi, Mshunami, awe mke wangu; hatakukatalia wewe.”
18 And Bath-sheba said: Good! I myself, will speak for thee, unto the king.
Bathsheba akamjibu, “Vema sana, nitazungumza na mfalme kwa ajili yako.”
19 So Bath-sheba went in unto King Solomon, to speak to him for Adonijah, —and the king rose up to meet her, and bowed himself down to her, and sat down upon his throne, and caused a throne to be set for the mother of the king, and she sat on his right hand.
Bathsheba alipokwenda kwa Mfalme Solomoni kuzungumza naye kwa ajili ya Adoniya, mfalme alisimama kumlaki mama yake, akamwinamia na kuketi kwenye kiti chake cha ufalme. Akaamuru kiti cha ufalme kuletwa kwa ajili ya mama yake mfalme, naye akaketi mkono wake wa kuume.
20 Then said she—One small request, am I asking of thee, do not turn away my face. And the king said to her—Ask on, my mother, for I will not turn away thy face.
Bathsheba akamwambia mfalme, “Ninalo ombi moja dogo la kukuomba; usinikatalie.” Mfalme akajibu, “Omba, mama yangu; sitakukatalia.”
21 And she said, Let Abishag the Shunammite be given to Adonijah thy brother, to wife.
Akasema, “Mruhusu Abishagi, Mshunami, aolewe na ndugu yako Adoniya.”
22 Then answered King Solomon, and said to his mother—Wherefore, then, art thou asking Abishag the Shunammite, for Adonijah? ask, then, for him the kingdom, because he is mine elder brother, —even for him, and for Abiathar the priest, and for Joab, son of Zeruiah.
Mfalme Solomoni akamjibu mama yake, “Kwa nini uombe Abishagi, Mshunami, kwa ajili ya Adoniya? Ungeweza pia kuomba ufalme kwa ajili yake, kwani yeye ni ndugu yangu mkubwa: naam, kwa ajili yake, na kwa kuhani Abiathari na Yoabu mwana wa Seruya!”
23 Then swore King Solomon by Yahweh, saying, —So, let God do to me, and, so, let him add, if, at the cost of his life, Adonijah hath not spoken this word.
Mfalme Solomoni akaapa kwa Bwana, akasema: “Mungu na aniulie mbali, tena bila huruma, ikiwa Adoniya hatalipa kwa uhai wake kwa ajili ya ombi hili!
24 Now, therefore, by the life of Yahweh, who hath established me, and seated me upon the throne of David my father, and who hath made for me a household, as he had spoken, surely, to-day, shall Adonijah be put to death!
Basi sasa, hakika kama Bwana aishivyo, yeye ambaye ameniimarisha salama kwenye kiti cha ufalme cha Daudi baba yangu, naye amenipa ufalme wa kudumu kama alivyoahidi, Adoniya atauawa leo!”
25 So King Solomon sent by the hand of Benaiah son of Jehoiada, —and he fell upon him, that he died.
Hivyo Mfalme Solomoni akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada, naye akampiga Adoniya akafa.
26 Also, unto Abiathar the priest, said the king—To Anathoth, get thee unto thine own fields, for, death-doomed, thou art, —but, this day, will I not put thee to death, because thou didst bear the ark of My Lord, Yahweh, before David my father, and because thou wast afflicted in all wherein my father was afflicted.
Mfalme akamwambia kuhani Abiathari, “Nenda huko Anathothi katika mashamba yako. Wewe unastahili kufa, lakini sitakuua sasa, kwa sababu ulilichukua Sanduku la Bwana Mwenyezi mbele ya Daudi baba yangu na ulishiriki taabu zote za baba yangu.”
27 So Solomon thrust out Abiathar from being priest unto Yahweh, —to fulfil the word of Yahweh which he spake concerning the household of Eli, in Shiloh.
Hivyo Solomoni akamwondoa Abiathari kwenye ukuhani wa Bwana, akilitimiza neno la Bwana alilokuwa amenena huko Shilo kuhusu nyumba ya Eli.
28 And, the report, came unto Joab, for, Joab, had inclined after Adonijah, although, after Solomon, he had not inclined, —so then Joab fled into the Tent of Yahweh, and laid hold of the horns of the altar.
Habari zilipomfikia Yoabu, ambaye alikuwa amefanya shauri baya na Adoniya, lakini sio na Absalomu, alikimbilia kwenye hema la Bwana na kushika pembe za madhabahu.
29 And it was told King Solomon—Joab hath fled into the Tent of Yahweh, and, there he is, beside the altar. So Solomon sent Benaiah son of Jehoiada, saying—Go fall upon him!
Mfalme Solomoni akaambiwa kuwa Yoabu amekimbilia kwenye hema la Bwana naye alikuwa kando ya madhabahu. Basi Solomoni akamwagiza Benaya mwana wa Yehoyada: “Nenda ukamuue!”
30 And Benaiah came into the Tent of Yahweh, and said unto him—Thus, saith the king, Come forth! And he said—Nay! but, here, will I die! So Benaiah brought the king word again, saying, Thus, spake Joab, and, thus, he answered me.
Ndipo Benaya akaingia kwenye hema la Bwana na kumwambia Yoabu, “Mfalme anasema, ‘Toka nje!’” Lakini akajibu, “La! Nitafia hapa hapa.” Benaya akamwarifu mfalme, “Hivi ndivyo Yoabu alivyonijibu.”
31 And the king said to him—Do as he hath spoken, fall, then, upon him, and bury him, —and so put away the innocent blood, which Joab shed, from off me, and from off the house of my father;
Kisha mfalme akamwamuru Benaya, “Fanya kama asemavyo. Muue na kumzika, ili uniondolee mimi na nyumba ya baba yangu dhambi ya damu isiyokuwa na hatia ile Yoabu aliyoimwaga.
32 thus will Yahweh bring back his blood upon his own head, in that he fell upon two men more righteous and better than he, and slew them with the sword, my father David not knowing it, —even Abner son of Ner, general of the army of Israel, and Amasa son of Jether, general of the army of Judah;
Bwana atamlipiza kwa ajili ya damu aliyoimwaga, kwa sababu pasipo Daudi baba yangu kujua, aliwashambulia watu wawili na kuwaua kwa upanga. Wote wawili, Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Israeli, na Amasa mwana wa Yetheri, jemadari wa jeshi la Yuda, walikuwa watu wazuri na wanyofu kuliko yeye.
33 thus shall their blood come back upon the head of Joab, and upon the head of his seed unto times age-abiding, —but, David and his seed, and his house, and his throne, shall have peace, unto times age-abiding, from Yahweh.
Hatia ya damu yao na iwe juu ya kichwa cha Yoabu na wazao wake milele. Lakini kwa Daudi na uzao wake, nyumba yake na kiti chake cha ufalme, iwepo amani ya Bwana milele.”
34 So Benaiah son of Jehoiada went up, and fell upon him, and put him to death, —and he was buried in his own house, in the wilderness.
Basi Benaya mwana wa Yehoyada akakwea, akampiga na kumuua Yoabu, naye akazikwa katika nchi yake mwenyewe katika jangwa.
35 And the king put Benaiah son of Jehoiada, in his stead, over the army, —and, Zadok the priest, did the king put in the stead of Abiathar.
Mfalme akamweka Benaya mwana wa Yehoyada juu ya jeshi kwenye nafasi ya Yoabu na kumweka kuhani Sadoki badala ya Abiathari.
36 And the king sent, and called for Shimei, and said to him—Build thee a house, in Jerusalem, so shalt thou dwell there, —and shalt not go forth from thence, hither or thither;
Kisha mfalme akatuma ujumbe kwa Shimei na kumwambia, “Ujijengee nyumba huko Yerusalemu uishi huko, lakini usiende mahali pengine popote.
37 but it shall be that, on the day thou goest forth, and passest over the Kidron ravine, know, that thou shalt, die, —thy blood, shall be, upon thine own head.
Siku utakayoondoka kuvuka Bonde la Kidroni, uwe na hakika utakufa; damu yako itakuwa juu ya kichwa chako mwenyewe.”
38 And Shimei said to the king—Good, is the word, as my lord the king hath spoken, so, will thy servant do. And Shimei dwelt in Jerusalem many days.
Shimei akamjibu mfalme, “Ulilolisema ni jema. Mtumishi wako atatenda kama bwana wangu mfalme alivyosema.” Naye Shimei akakaa Yerusalemu kwa muda mrefu.
39 But it came to pass, at the end of three years, that two of the servants of Shimei fled unto Achish son of Maachah king of Gath, —and they told Shimei, saying—Lo! thy servants are in Gath.
Lakini baada ya miaka mitatu, watumwa wawili wa Shimei wakatoroka kwenda kwa Akishi mwana wa Maaka, mfalme wa Gathi, naye Shimei akaambiwa, “Watumwa wako wako Gathi.”
40 So Shimei arose, and saddled his ass, and went to Gath, unto Achish, to seek his servants—and Shimei went and brought in his servants, from Gath.
Kwa ajili ya hili, Shimei akatandika punda wake, akaenda kwa Akishi huko Gathi kuwatafuta watumwa wake. Basi Shimei akaondoka na kuwarudisha watumwa wake kutoka Gathi.
41 And it was told Solomon—Shimei hath been out of Jerusalem to Gath, and returned.
Solomoni alipoambiwa kuwa Shimei ametoka Yerusalemu na kwenda Gathi na amekwisha kurudi,
42 Then sent the king and called for Shimei, and said unto him—Did I not put thee on oath by Yahweh, and adjure thee, saying—On the day thou goest forth and takest thy journey hither or thither, know, that thou shalt, die. Then saidst thou unto me—Good, is the word I have heard.
mfalme akamwita Shimei na kumwambia, “Je, sikukuapiza kwa Bwana na kukuonya kuwa, ‘Siku utakayoondoka kwenda mahali pengine popote, uwe na hakika utakufa?’ Wakati ule uliniambia, ‘Ulilolisema ni jema. Nitatii!’
43 Why then, hast thou not kept the oath of Yahweh, —and the charge which I laid upon thee?
Kwa nini basi hukutunza kiapo chako kwa Bwana na kutii amri niliyokupa?”
44 Then said the king unto Shimei—Thou, knowest all the wickedness which thy heart is privy to, which thou didst unto David my father, —therefore shall Yahweh bring back thy wickedness, upon thine own head.
Pia mfalme akamwambia Shimei, “Unajua katika moyo wako makosa uliyomtendea baba yangu Daudi. Sasa Bwana atakulipiza kwa ajili ya mabaya yako uliyotenda.
45 But, King Solomon, shall be blessed, —and, the throne of David, shall be established before Yahweh, unto times age-abiding.
Lakini Mfalme Solomoni atabarikiwa, na kiti cha ufalme cha Daudi kitakuwa imara mbele za Bwana milele.”
46 So the king charged Benaiah son of Jehoiada, and he went out and fell upon him, that he died, —and, the kingdom, was established in the hand of Solomon.
Kisha mfalme akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada, naye akatoka nje, akampiga Shimei na kumuua. Sasa ufalme ukawa umeimarika kikamilifu mikononi mwa Solomoni.

< 1 Kings 2 >