< 1 Kings 15 >

1 Now, in the eighteenth year of King Jeroboam son of Nebat, began Abijah to reign over Judah.
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
2 Three years, reigned he in Jerusalem, —and, the name of his mother, was Maachah, daughter of Abishalom.
naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
3 And he walked in all the sins of his father which he had done before him, —and his heart was not blameless with Yahweh his God, like the heart of David his father.
Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
4 But, for the sake of David, did Yahweh his God give him a lamp, in Jerusalem, —by raising up a son of his after him, and by suffering Jerusalem to stand;
Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
5 because David did that which was right in the eyes of Yahweh, —and turned not aside from anything that he commanded him, all the days of his life, save only in the matter of Uriah the Hittite.
Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
6 And there was, war, between Rehoboam and Jeroboam, all the days of his life.
Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
7 Now, the rest of the story of Abijah and all that he did, are, they, not written in the book of Chronicles of the Kings of Judah? And there was, war, between Abijah and Jeroboam.
Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
8 So then Abijah slept with his fathers, and they buried him in the city of David, —and, Asa his son, reigned, in his stead.
Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
9 Now, in the twentieth year of Jeroboam king of Israel, began Asa to reign as king of Judah;
Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
10 and, forty-one years, reigned he in Jerusalem, —and, the name of his mother, was Maachah, daughter of Abishalom.
naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
11 And Asa did that which was right in the eyes of Yahweh, —like David his father;
Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
12 and he put away the male devotees out of the land, —and removed all the idols that his fathers had made.
Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
13 Moreover also, even Maachah his mother, he removed from being queen, because she had made a monstrous thing to the Sacred Stem, —and Asa cut down her monstrous thing and burned it in the Kidron ravine.
Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
14 But, the high places, removed he not, —nevertheless, the heart of Asa, was blameless with Yahweh, all his days.
Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
15 And he brought in the hallowed things of his father, and his own hallowed things, into the house of Yahweh, —silver and gold, and vessels.
Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
16 And there was, war, between Asa and Baasha king of Israel, all their days.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
17 And Baasha king of Israel came up against Judah, and built Ramah, —so as not to suffer any one to come out or go in unto Asa king of Judah.
Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
18 So Asa took all the silver and the gold, that were left in the treasuries of the house of Yahweh, and the treasures of the house of the king, and delivered them into the hand of his servants, —and King Asa sent them unto Ben-hadad, son of Tabrimmon, son of Hezion, king of Syria, who dwelt in Damascus, saying:
Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
19 [Let there be a] covenant between me and thee, [as] between my father and thy father: Lo! I have sent thee a gift, silver and gold, Come break thy covenant with Baasha, king of Israel, that he may go up from against me.
“Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
20 So Ben-hadad hearkened unto King Asa, and sent the generals of the forces which he had, against the cities of Israel, and smote Iyyohn [Ijon], and Dan, and Abel-beth-maacah, —and all Chinneroth, against all the land of Naphtali.
Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
21 And it came to pass, when Baasha heard thereof, he left off building Ramah, —and returned to Tirzah.
Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
22 And, King Asa, published it unto all Judah, none was exempted, so they carried away the stones of Ramah, and the beams thereof, wherewith Baasha had built, —and King Asa built therewith Geba of Benjamin, and Mizpah.
Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
23 Now, the rest of all the story of Asa, and all his might, and all that he did and the cities which he built, are, they, not written in the book of the Chronicles of the Kings of Judah? Howbeit, in the time of his old age, he was diseased in his feet.
Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
24 So then Asa slept with his fathers, and was buried with his fathers, in the city of David his father, —and, Jehoshaphat his son, reigned, in his stead.
Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Now, Nadab son of Jeroboam, began to reign over Israel, in the second year of Asa king of Judah, —and he reigned over Israel, two years.
Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
26 And he did the thing that was wicked in the eyes of Yahweh, —and walked in the way of his father, and in his sin, wherewith he caused, Israel, to sin.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
27 And Baasha son of Ahijah, of the house of Issachar, conspired against him, and Baasha smote him in Gibbethon, which belonged to the Philistines, —Nadab and all Israel being in siege against Gibbethon.
Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
28 And Baasha slew him, in the third year of Asa king of Judah, —and reigned in his stead.
Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
29 And it came to pass, when he became king, that he smote all the house of Jeroboam, he left not remaining any breathing thing pertaining to Jeroboam, until he had destroyed him, —according to the word of Yahweh, which he spake by the hand of his servant Ahijah the Shilonite:
Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
30 for the sins of Jeroboam which he committed, and which he caused, Israel, to commit, —by his provocation wherewith he provoked to anger Yahweh God of Israel.
kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
31 Now, the rest of the story of Nadab, and all that he did, are, they, not written in the book of the Chronicles of the kings of Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
32 And there was, war, between Asa and Baasha king of Israel, all their days.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
33 In the third year of Asa king of Judah, began Baasha, son of Ahijah, to reign over all Israel, in Tirzah, [and he reigned] twenty-four years.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
34 And he did that which was wicked in the eyes of Yahweh, —and walked in the way of Jeroboam, and in his sin wherewith he caused, Israel, to sin.
Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.

< 1 Kings 15 >