< 1 John 3 >

1 Behold, what manner of love, the Father hath bestowed upon us—that, children of God, we should be called, —and such we are! Therefore, the world understandeth us not, because it understood not him.
Oneni basi, jinsi Baba alivyotupenda mno hata tunaitwa watoto wa Mungu! Na kweli, ndivyo tulivyo. Ndiyo maana ulimwengu haututambui sisi, kwani haumjui Mungu.
2 Beloved! now, are we, children of God; and, not yet, hath it been made manifest, what we shall be, —We know that, if it should be made manifest, like unto him, shall we be, because we shall see him, just as he is.
Wapenzi wangu, sisi ni watoto wa Mungu sasa, lakini bado haijaonekana wazi jinsi tutakavyokuwa. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwani tutamwona vile alivyo.
3 And, whosoever hath this hope on him, is purifying himself, just as, He, is pure.
Basi, kila mtu aliye na tumaini hili katika Kristo, hujiweka safi kama vile Kristo alivyo safi kabisa.
4 Whosoever is committing sin, lawlessness also, is committing, and, sin, is, lawlessness;
Kila mtu atendaye dhambi anavunja sheria ya Mungu, maana dhambi ni uvunjaji wa sheria.
5 And ye know, that, He, was made manifest—in order that, our sins, he should take away, and, sin, in him, is there none.
Mnajua kwamba Kristo alikuja kuziondoa dhambi zetu, na kwamba kwake hamna dhambi yoyote.
6 Whosoever, in him, doth abide, is not sinning: whosoever is sinning, hath not seen him, and doth not understand him.
Basi, kila aishiye katika muungano na Kristo hatendi dhambi; lakini kila mtu atendaye dhambi hakupata kamwe kumwona, wala kumjua Kristo.
7 Dear children! Let, no one, lead you astray! He that is doing righteousness, is, righteous, just as, He, is righteous:
Basi, watoto wangu, msikubali kupotoshwa na mtu yeyote. Mtu atendaye matendo maadilifu ni mwadilifu kama vile Kristo alivyo mwadilifu kabisa.
8 He that is committing sin, is, of the adversary, because, from the beginning, the adversary is sinning. To this end, was the Son of God made manifest, in order that he might undo the works of the adversary.
Lakini atendaye dhambi ni wa Ibilisi, maana Ibilisi ametenda dhambi tangu mwanzo. Lakini Mwana wa Mungu alikuja duniani kuiharibu kazi ya Ibilisi.
9 Whosoever hath been born of God, is not committing, sin, because, a seed of him, within him, abideth; and he cannot be committing sin, because, of God, hath he been born.
Kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, maana anayo hali ya kimungu ndani yake; hawezi kutenda dhambi kwa sababu yeye ni mtoto wa Mungu.
10 Herein, are, manifest, the children of God, and the children of the adversary: Whoever is not doing righteousness, is not of God, nor yet he that is not loving his brother.
Lakini yeyote asiyetenda mambo maadilifu, au asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi.
11 Because, this, is the message which ye have heard from the beginning—that we should be loving one another, —
Na, ujumbe mliousikia tangu mwanzo ndio huu: Tunapaswa kupendana!
12 Not just as, Cain, was, of the wicked one, and slew his brother! And, for what cause, slew he him? Because, his works, were, wicked, whereas, those of his brother, were, righteous.
Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimuua ndugu yake. Na, kwa nini alimuua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu, lakini yale ya ndugu yake yalikuwa mema!
13 Be not marveling, brethren, if, the world, is hating you:
Basi, ndugu zangu, msishangae kama ulimwengu unawachukia ninyi.
14 We, know, that we have passed over out of death into life, because we love the brethren: he that loveth not, abideth in death.
Sisi tunajua kwamba tumekwisha pita kutoka katika kifo na kuingia katika uzima kwa sababu tunawapenda ndugu zetu. Mtu asiye na upendo hubaki katika kifo.
15 Whosoever is hating his brother, is, a murderer; and ye know that, no murderer, hath life age-during, within him abiding. (aiōnios g166)
Kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji; nanyi mnajua kwamba muuaji yeyote yule hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios g166)
16 Hereby, have we come to understand love: in that, He, for us, his life laid down; and, we, ought, for the brethren, our lives to lay down.
Sisi tumepata kujua upendo ni nini, kwani Kristo aliyatoa maisha yake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu.
17 But, whoso hath this world’s goods, and beholdeth his brother having, need, and shutteth up his tender affections from him, how, is, the love of God, abiding in him?
Basi, mtu akiwa na mali za hapa duniani, halafu akamwona ndugu yake ana shida, lakini akawa na moyo mgumu bila kumwonea huruma, anawezaje kusema kwamba anampenda Mungu?
18 Dear children! Let us not be loving in word, nor yet with the tongue, but in deed and truth.
Watoto wangu, upendo wetu usiwe maneno matupu, bali uwe upendo wa kweli na wa vitendo.
19 Hereby, shall we get to know, that, of the truth, we are, and, before him, shall persuade our heart;
Hivyo ndivyo tuwezavyo kuwa na hakika kwamba sisi ni watu wa ukweli; na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu.
20 Because, if our own heart condemn us, greater, is God, than our heart, and perceiveth all things.
Kwa maana, hata kama dhamiri yetu yatuhukumu, twajua kwamba Mungu ni mkuu zaidi kuliko dhamiri, na kwamba yeye ajua kila kitu.
21 Beloved! if our heart be not condemning us, boldness, have we, towards God;
Wapenzi wangu, kama dhamiri yetu haina lawama juu yetu, basi, twaweza kuwa na uthabiti mbele ya Mungu,
22 And, whatsoever we are asking, we are receiving from him, because, his commandments, are we keeping, and, the things that are pleasing before him, are we doing.
na twaweza kupokea kwake chochote tunachoomba, maana tunazitii amri zake na kufanya yale yanayompendeza.
23 And, this, is his commandment, —that we should believe in the name of his Son Jesus Christ, and be loving one another—just as he gave a commandment unto us.
Na, amri yake ndiyo hii: Kumwamini Mwanae Kristo, na kupendana kama alivyotuamuru.
24 And, he that keepeth his commandments, in him, abideth, and, he, in him. And, hereby, perceive we, that he abideth in us, by reason of the Spirit which, unto us, he hath given.
Anayezitii amri za Mungu anaishi katika muungano na Mungu na Mungu anaishi katika muungano naye. Kwa njia ya Roho ambaye Mungu ametujalia, sisi twajua kwamba Mungu anaishi katika muungano nasi.

< 1 John 3 >