< 1 Chronicles 24 >

1 Now, the sons of Aaron, had their courses, —the sons of Aaron, Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar;
Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 but Nadab and Abihu, died, before their father, and sons, had they none, —but Eleazar and Ithamar became priests;
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
3 and David apportioned to them courses, both to Zadok of the sons of Eleazar, and to Ahimelech of the sons of Ithamar, —by their appointed place in their service.
Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
4 But the sons of Eleazar were found to be more numerous, by the chiefs of their able men, than were the sons of Ithamar, so they divided them, —the sons of Eleazar, had chiefs, of the ancestral house, sixteen, whereas, the sons of Ithamar, had of their ancestral house, eight.
Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
5 They divided them, therefore, by [casting] lots, these with those, —for there were princes of the sanctuary, and princes of God, from among the sons of Eleazar, and among the sons of Ithamar.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
6 And Shemaiah son of Nethanel the scribe from among the Levites, wrote them down, before the king and the rulers and Zadok the priest, and Ahimelech son of Abiathar, and the ancestral chiefs, pertaining to the priests and to the Levites, —one ancestral house, was taken for Eleazar, and, was equally taken, for Ithamar.
Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
7 So then the first lot came forth for Jehoiarib, for Jedaiah, the second;
Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
8 for Harim, the third, for Seorim, the fourth;
ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
9 for Malchijah, the fifth, for Mijamin, the sixth;
ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
10 for Hakkoz, the seventh, for Abijah, the eighth;
ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
11 for Jeshua, the ninth, for Shecaniah, the tenth;
ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
12 for Eliashib, the eleventh, for Jakim, the twelfth;
ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
13 for Huppah, the thirteenth, for Jeshebeab, the fourteenth;
ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
14 for Bilgah, the fifteenth, for Immer, the sixteenth;
ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
15 for Hezir, the seventeenth, for Happizzez, the eighteenth;
ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
16 for Pethahiah, the nineteenth, for Jehezkel, the twentieth;
ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
17 for Jachin, the twenty-first, for Gamul, the twenty-second;
ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
18 for Delaiah, the twenty-third, for Maaziah, the twenty-fourth.
ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
19 These, were their appointed places for their service, for entering the house of Yahweh, according to the regulation of them, by the hand of Aaron their father, —just as Yahweh God of Israel, commanded him.
Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
20 Now, as for the sons of Levi who remained, of the sons of Amram, Shubael, of the sons of Shubael, Jehdeiah.
Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
21 Of Rehabiah, of the sons of Rehabiah, the chief Isshiah;
Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
22 of the Izharites, Shelomoth, —of the sons of Shelomoth, Jahath;
Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
23 and, the sons [of Hebron], Jeriah, —Amariah, the second, Jehaziel, the third, Jekameam, the fourth;
Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
24 the sons of Uzziel, Micah, of the sons of Micah, Shamir;
Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
25 the brother of Micah, Isshiah, of the sons of Isshiah, Zechariah.
Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
26 The sons of Merari, Mahli and Mushi, —the sons of Jaaziah, Beno;
Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
27 the sons of Merari, of Jaaziah, Beno, and Shoham and Zaccur and Ibri:
Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
28 of Mahli, Eleazar, who had no sons;
Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
29 of Kish—the sons of Kish, Jerameel;
Wana wa Kishi: Yerameli
30 and, the sons of Mushi, Mahli and Eder and Jerimoth. These, were the sons of the Levites, belonging to their ancestral house.
wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
31 Moreover, they also, cast lots along with their brethren the sons of Aaron, before David the king and Zadok and Ahimelech, and the ancestral chiefs, pertaining to the priests and to the Levites, the ancestral chief along with his younger brethren.
Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.

< 1 Chronicles 24 >