< 1 Chronicles 15 >

1 And he made him houses, in the city of David, —and prepared a place for the ark of God, and pitched for it a tent.
Daudi akajingea nyumba zake katika mji wa Daudi. Akaanda sehemu kwa ajili ya sanduku la Mungu na hema lake.
2 Then, said David, None must carry the ark of God, save the Levites, —for, of them, did Yahweh make choice, to bear the ark of Yahweh, and to attend it, unto times age-abiding.
Kisha Daudi akasema, “Walawi pekee ndio watabeba sanduku la Mungu, kwa kuwa walichaguliwa na Yahweh kubeba sanduku la Yahweh, na kumtumikia milele.”
3 So David convoked all Israel, unto Jerusalem, —to bring up the ark of Yahweh, unto the place thereof, which he had prepared for it.
Kisha Daudi akakusanya Israeli yote Yerusalemu, kuleta sanduku la Yahweh sehemu aliyo iandaa.
4 And David gathered together the sons of Aaron, and the Levites:
Daudi akakusanya uzao wa Aruni na Walawi pamoja.
5 Of the sons of Kohath, Uriel the chief, and his brethren, one hundred and twenty;
Kutoka uzao wa Kohathi, palikuwa na Urieli kiongozi na ndugu zake, wanaume 120.
6 of the sons of Merari, Asaiah the chief, and his brethren, two hundred and twenty;
Kutoka uzao wa Merari, palikuwa na Asaia kiongozi na ndugu zake, wanaume 220.
7 of the sons of Gershom, Joel the chief, and his brethren, one hundred and thirty;
Kutoka uzao wa Gerishomu, palikuwa na Yoeli kiongozi na ndugu zake, wanaume 130.
8 of the sons of Elizaphan, Shemaiah the chief, and his brethren, two hundred;
Kutoka uzao wa Elizafani, palikuwa na Shemaia kiongozi na ndugu zake, wanaume 200.
9 of the sons of Hebron, Eliel the chief, and his brethren, eighty;
Kutoka uzao wa Hebroni, palikuwa na Elieli kiongozi na ndugu zake, wanaume themanini.
10 of the son of Uzziel, Amminadab the chief, and his brethren, a hundred and twelve.
Kutoka uzao wa Uzieli, palikuwa na Aminadabu kiongozi na ndugu zake, wanaume 112.
11 Then called David, for Zadok and for Abiathar, the priests, —and for the Levites, for Uriel, Asaiah and Joel, Shemaiah and Eliel, and Amminadab;
Daudi akaagiza Zadoki kuitwa na Abiathari kuhuani, na Walawi Urieli, Asaia, Yoeli, Shemaia, Elieli, na Aminadabu.
12 and said unto them, Ye, are the chiefs of the fathers of the Levites, —Hallow yourselves, ye and your brethren, so shall ye bring up the ark of Yahweh—God of Israel, into [the place] I have prepared for it.
Akasema, “Nyinyi ni viongozi wa familia za Kilawi. Jiwekeni wakfu, nyie na ndugu zenu, ilikwamba mlete sanduku la Yahweh, Mungu wa Israeli, kwenye sehemu niliyo iandaa.
13 Because, at the first, ye, did not [bring it], Yahweh our God brake forth against us, because we sought him not in the appointed way.
Mara ya kwanza hamkubeba. Ndio maana Yahweh Mungu wetu akawa na hasira kwetu, kwa kuwa hatuku mtafuta wala kutii amri yake.”
14 So the priests and the Levites hallowed themselves, —to bring up the ark of Yahweh, God of Israel.
Hivyo makuhani na Walawi waka jiweka wakfu iliwaweze kuleta sanduku la Yahweh, Mungu wa Israeli.
15 And the sons of the Levites bare the ark of God, just as Moses commanded, according to the word of Yahweh, —on their shoulder, with the staves upon them.
Walawi wakabeba sanduku la Mungu katika mabega yao na nguzo, kama Musa alivyo amuru-kwa kufuata sheria zilizo tolewa na Yahweh.
16 And David spake to the chiefs of the Levites, to station their brethren the singers, with instruments of song, harps and lyres, and cymbals, —sounding aloud at the lifting up of the voice, for joy.
Daudi akazungumza na viongozi wa Walawi kuwapangia ndugu zao kuwa wana muziki wenye vyombo vya muziki, vyombo vya uzi, vinubi na upatu, kwa kupiga kwa sauti na furaha wakipaza sauti zao.
17 So the Levites caused to stand, Heman son of Joel, and, of his brethren, Asaph, son of Berechiah, —and, of the sons of Merari their brethren, Ethan, son of Kushaiah;
Hivyo Walawi wakamchagua Hemani mwana wa Yoeli na mmoja wa kaka zake, Asafu mwana wa Berekia. Pia walimchagua ndugu wa uzao wa Merari na Ethani mwana wa Kushaia.
18 and, with them, their brethren of the second degree, —Zechariah, Ben, and Jaaziel, and Shemiramoth, and Jehiel and Unni, Eliab, and Benaiah, and Maaseiah, and Mattithiah, and Eliphelehu, and Mickneiah, and Obed-edom and Jeiel, the door-keepers.
Pamoja nao walikuwa ndugu wa daraja la pili: Zekarai, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaia, Maasaeia, Matithia, Elifelehu, Mikineaia, Obedi Edomu, na Yeieli, mlinzi wa lango.
19 And, the singers, Heman, Asaph and Ethan, with cymbals of bronze, were to sound aloud;
Wanamuziki Hemani, Asafu, na Ethani walichaguliwa kupiga upatu wa shaba.
20 and Zechariah, and Aziel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Unni, and Eliab, and Maaseiah and Benaiah, —with harps, over the trebles;
Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni Eliabu, Maaseia, na Benaia walicheza vyombo vya uzi.
21 and Mattithiah, Eliphelehu, and Mikneiah, and Obed-edom, and Jeiel and Azaziah, —with lyres over the bass, to take the lead.
Matithia, Elifelehu, Mikineia, Obedi Edomu, Yeieli, na Azazia waliongoza njia na vinubi.
22 And, Chenaniah the leader of the Levites, in the service, used to give instructions in the service, because skilful was he.
Kenania, kiongozi wa Walawi, aliongoza uimbaji sababu alikuwa mwalimu wa muziki.
23 And, Berechiah and Elkanah, were door-keepers to the ark.
Berekia na Elikana walikuwa walinzi wa sanduku.
24 And, Shebaniah, and Joshaphat, and Nethanel, and Amasai, and Zechariah, and Benaiah, and Eliezer, the priests, were blowing with the trumpets, before the ark of God, —and, Obed-edom and Jehiah, were door-keepers, to the ark.
Shebania, Yoshafati, Nethanieli, Amasai, Zekaria, Benaia, na Eliezeri, makuhani, walikuwa wa kupuliza matarumbeta mbele ya sanduku la Mungu. Obedi Edomu na Yehia walikuwa walinzi wa sanduku.
25 Thus, it was, David and the elders of Israel, and the rulers of thousands, who were going, to bring up the ark of the covenant of Yahweh, out of the house of Obed-edom, with joy.
Hivyo Daudi, wazee wa Israeli, na wakuu wa maelfu wakaenda kuchukua sanduku la agano la Yahweh kutoka nyumba ya Obedi Edomu kwa shangwe.
26 And so it was that, when God helped the Levites, who were bearing the ark of the covenant of Yahweh, they sacrificed seven bullocks and seven rams.
Wakati Mungu alipo wasaidia Walawi kubeba sanduku la agano la Yahweh, walitoa ng'ombe saba na mbuzi
27 Now, David, was wrapped about with a robe of byssus, with all the Levites who were bearing the ark, and the singers, and Chenaniah the leader of the service rendered by the singers, —but, upon David, was an ephod of white linen.
Daudi alivishwa joho safi la maridadi, pamoja na Walawi walio beba sanduku, waimbaji, na Kenania, kiongozi wa nyimbo na waimbaji. Daudi alivaa juu ya joho lake naivera.
28 So, all Israel, were bringing up the ark of the covenant of Yahweh, with shouting, and with sound of the horn, and with trumpets, and with cymbals, —sounding aloud, with harps, and lyres.
Hivyo Israeli yote wakaleta sanduku la agano la Yahweh na kelele za shangwe, na sauti za tarumbeta, ngoma za saani, na vyombo vya uzi na vinubi.
29 And so it was that, when the ark of the covenant of Yahweh came in as far as the city of David, —and Michal daughter of Saul looked forth through the window, and saw King David, dancing and playing, that she despised him in her heart.
Lakini sanduku la Yahweh lilivyokuja kwa mji wa Daudi, Mikali binti wa Sauli, alitazama nje ya dirisha, Akamuona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea. Kisha akamdharau moyoni mwake.

< 1 Chronicles 15 >