< Song of Solomon 3 >

1 By night on my bed I sought him whom my soul loveth: I sought him, but I found him not.
Usiku kucha kwenye kitanda changu nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye; nilimtafuta, lakini sikumpata.
2 [I said], I will rise now, and go about the city, in the streets and in the broad ways, I will seek him whom my soul loveth: I sought him, but I found him not.
Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini, katika barabara zake na viwanja; nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye. Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.
3 The watchmen that go about the city found me: [to whom I said], Saw ye him whom my soul loveth?
Walinzi walinikuta walipokuwa wakizunguka mji. Nikawauliza, “Je, mmemwona yule moyo wangu umpendaye?”
4 It was but a little that I passed from them, when I found him whom my soul loveth: I held him, and would not let him go, until I had brought him into my mother’s house, and into the chamber of her that conceived me.
Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita nilimpata yule moyo wangu umpendaye. Nilimshika na sikumwachia aende mpaka nilipomleta katika nyumba ya mama yangu, katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.
5 I adjure you, O daughters of Jerusalem, by the roes, and by the hinds of the field, that ye stir not up, nor awaken love, until it please.
Binti za Yerusalemu, ninawaagiza kwa paa na kwa ayala wa shambani: Msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe.
6 Who is this that cometh up out of the wilderness like pillars of smoke, perfumed with myrrh and frankincense, with all powders of the merchant?
Ni nani huyu anayekuja kutoka jangwani kama nguzo ya moshi, anayenukia manemane na uvumba iliyotengenezwa kwa vikolezo vyote vya mfanyabiashara?
7 Behold, it is the litter of Solomon; threescore mighty men are about it, of the mighty men of Israel.
Tazama! Ni gari la Solomoni lisindikizwalo na mashujaa sitini, walio wakuu sana wa Israeli,
8 They all handle the sword, [and] are expert in war: every man hath his sword upon his thigh, because of fear in the night.
wote wamevaa panga, wote wazoefu katika vita, kila mmoja na upanga wake pajani, wamejiandaa kwa ajili ya hofu za usiku.
9 King Solomon made himself a palanquin of the wood of Lebanon.
Mfalme Solomoni alijitengenezea gari; alilitengeneza kwa mbao kutoka Lebanoni.
10 He made the pillars thereof of silver, the bottom thereof of gold, the seat of it of purple, the midst thereof being paved with love, from the daughters of Jerusalem.
Nguzo zake alizitengeneza kwa fedha, kitako chake kwa dhahabu. Kiti chake kilipambwa kwa zambarau, gari lake likanakshiwa njumu kwa upendo na binti za Yerusalemu.
11 Go forth, O ye daughters of Zion, and behold king Solomon, with the crown wherewith his mother hath crowned him in the day of his espousals, and in the day of the gladness of his heart.
Tokeni nje, ninyi binti za Sayuni, mkamtazame Mfalme Solomoni akiwa amevaa taji, taji ambalo mama yake alimvika siku ya arusi yake, siku ambayo moyo wake ulishangilia.

< Song of Solomon 3 >