< Psalms 96 >

1 O SING unto the LORD a new song: sing unto the LORD, all the earth.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
2 Sing unto the LORD, bless his name; shew forth his salvation from day to day.
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 Declare his glory among the nations, his marvelous works among all the peoples.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 For great is the LORD, and highly to be praised: he is to be feared above all gods.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 For all the gods of the peoples are idols: but the LORD made the heavens.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 Honour and majesty are before him: strength and beauty are in his sanctuary.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
7 Give unto the LORD, ye kindreds of the peoples, give unto the LORD glory and strength.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 Give unto the LORD the glory due unto his name: bring an offering, and come into his courts.
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 O worship the LORD in the beauty of holiness: tremble before him, all the earth.
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
10 Say among the nations, The LORD reigneth: the world also is stablished that it cannot be moved: he shall judge the peoples with equity.
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 Let the heavens be glad, and let the earth rejoice; let the sea roar, and the fulness thereof;
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 Let the field exult, and all that is therein; then shall all the trees of the wood sing for joy;
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 Before the LORD, for he cometh; for he cometh to judge the earth: he shall judge the world with righteousness, and the peoples with his truth.
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.

< Psalms 96 >