< Psalms 56 >

1 For the Chief Musician; set to Jonath elem rehokim. [A Psalm] of David: Michtam: when the Philistines took him in Gath. Be merciful unto me, O God; for man would swallow me up: all the day long he fighting oppresseth me.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
2 Mine enemies would swallow me up all the day long: for they be many that fight proudly against me.
Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
3 What time I am afraid, I will put my trust in thee.
Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
4 In God I will praise his word: in God have I put my trust, I will not be afraid; what can flesh do unto me?
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
5 All the day long they wrest my words: all their thoughts are against me for evil.
Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
6 They gather themselves together, they hide themselves, they mark my steps, even as they have waited for my soul.
Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
7 Shall they escape by iniquity? in anger cast down the peoples, O God.
Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
8 Thou tellest my wanderings: put thou my tears into thy bottle; are they not in thy book?
Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
9 Then shall mine enemies turn back in the day that I call: this I know, that God is for me.
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10 In God will I praise [his] word: in the LORD will I praise [his] word.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11 In God have I put my trust, I will not be afraid; what can man do unto me?
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
12 Thy vows are upon me, O God: I will render thank offerings unto thee.
Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
13 For thou hast delivered my soul from death: [hast thou] not [delivered] my feet from falling? that I may walk before God in the light of the living.
Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.

< Psalms 56 >