< Psalms 48 >

1 A Song; a Psalm of the sons of Korah. Great is the LORD, and highly to be praised, in the city of our God, in his holy mountain.
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 Beautiful in elevation, the joy of the whole earth, is mount Zion, [on] the sides of the north, the city of the great King.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 God hath made himself known in her palaces for a refuge.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 For, lo, the kings assembled themselves, they passed by together.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 They saw it, then were they amazed; they were dismayed, they hasted away.
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Trembling took hold of them there; pain, as of a woman in travail.
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 With the east wind thou breakest the ships of Tarshish.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 As we have heard, so have we seen in the city of the LORD of hosts, in the city of our God: God will establish it for ever. (Selah)
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 We have thought on thy lovingkindness, O God, in the midst of thy temple.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 As is thy name, O God, so is thy praise unto the ends of the earth: thy right hand is full of righteousness.
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 Let mount Zion be glad, let the daughters of Judah rejoice, because of thy judgments.
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Walk about Zion, and go round about her: tell the towers thereof.
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 Mark ye welt her bulwarks, consider her palaces; that ye may tell it to the generation following.
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 For this God is our God for ever and ever: he will be our guide [even] unto death.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.

< Psalms 48 >