< Psalms 45 >

1 For the Chief Musician; set to Shoshannim; [a Psalm] of the sons of Korah. Maschil. A Song of loves. My heart overfloweth with a goodly matter: I speak the things which I have made touching the king: my tongue is the pen of a ready writer.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
2 Thou art fairer than the children of men; grace is poured into thy lips: therefore God hath blessed thee for ever.
Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Gird thy sword upon thy thigh, O mighty one, thy glory and thy majesty.
Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
4 And in thy majesty ride on prosperously, because of truth and meekness [and] righteousness: and thy right hand shall teach thee terrible things.
Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
5 Thine arrows are sharp; the peoples fall under thee; [they are] in the heart of the king’s enemies.
Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
6 Thy throne, O God, is for ever and ever: a sceptre of equity is the sceptre of thy kingdom.
Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
7 Thou hast loved righteousness, and hated wickedness: therefore God, thy God, hath anointed thee with the oil of gladness above thy fellows.
Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
8 All thy garments [smell of] myrrh, and aloes, [and] cassia; out of ivory palaces stringed instruments have made thee glad.
Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
9 Kings’ daughters are among thy honourable women: at thy right hand doth stand the queen in gold of Ophir.
Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
10 Hearken, O daughter, and consider, and incline thine ear; forget also thine own people, and thy father’s house;
Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11 So shall the king desire thy beauty: for he is thy Lord; and worship thou him.
Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
12 And the daughter of Tyre [shall be there] with a gift; even the rich among the people shall entreat thy favour.
Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
13 The king’s daughter within [the palace] is all glorious: her clothing is inwrought with gold.
Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
14 She shall be led unto the king in broidered work: the virgins her companions that follow her shall be brought unto thee.
Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
15 With gladness and rejoicing shall they be led: they shall enter into the king’s palace.
Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
16 Instead of thy fathers shall be thy children, whom thou shalt make princes in all the earth.
Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
17 I will make thy name to be remembered in all generations: therefore shall the peoples give thee thanks for ever and ever.
Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.

< Psalms 45 >