< Psalms 31 >

1 For the Chief Musician. A Psalm of David. In thee, O LORD, do I put my trust; let me never be ashamed: deliver me in thy righteousness.
Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
2 Bow down thine ear unto me; deliver me speedily: be thou to me a strong rock, an house of defence to save me.
Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
3 For thou art my rock and my fortress; therefore for thy name’s sake lead me and guide me.
Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
4 Pluck me out of the net that they have laid privily for me; for thou art my strong hold.
Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
5 Into thine hand I commend my spirit: thou hast redeemed me, O LORD, thou God of truth.
Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
6 I hate them that regard lying vanities: but I trust in the LORD.
Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
7 I will be glad and rejoice in thy mercy: for thou hast seen my affliction; thou hast known my soul in adversities:
Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
8 And thou hast not shut me up into the hand of the enemy; thou hast set my feet in a large place.
Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
9 Have mercy upon me, O LORD, for I am in distress: mine eye wasteth away with grief, [yea], my soul and my body.
Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
10 For my life is spent with sorrow, and my years with sighing: my strength faileth because of mine iniquity, and my bones are wasted away.
Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
11 Because of all mine adversaries I am become a reproach, yea, unto my neighbours exceedingly, and a fear to mine acquaintance: they that did see me without fled from me.
Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
12 I am forgotten as a dead man out of mind: I am like a broken vessel.
Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
13 For I have heard the defaming of many, terror on every side: while they took counsel together against me, they devised to take away my life.
Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
14 But I trusted in thee, O LORD: I said, Thou art my God.
Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
15 My times are in thy hand: deliver me from the hand of mine enemies, and from them that persecute me.
Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
16 Make thy face to shine upon thy servant: save me in thy lovingkindness.
Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
17 Let me not he ashamed, O LORD; for I have called upon thee: let the wicked be ashamed, let them be silent in Sheol. (Sheol h7585)
Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
18 Let the lying lips be dumb; which speak against the righteous insolently, with pride and contempt.
Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
19 Oh how great is thy goodness, which thou hast laid up for them that fear thee, which thou hast wrought for them that put their trust in thee, before the sons of men!
Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
20 In the covert of thy presence shalt thou hide them from the plottings of man: thou shalt keep them secretly in a pavilion from the strife of tongues.
Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
21 Blessed be the LORD: for he hath shewed me his marvelous lovingkindness in a strong city.
Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
22 As for me, I said in my haste, I am cut off from before thine eyes: nevertheless thou heardest the voice of my supplications when I cried unto thee.
Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
23 O love the LORD, all ye his saints: the LORD preserveth the faithful, and plentifully rewardeth the proud doer.
Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
24 Be strong, and let your heart take courage, all ye that hope in the LORD.
Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.

< Psalms 31 >