< Psalms 30 >

1 A Psalm; a Song at the Dedication of the House; [a Psalm] of David. I will extol thee, O LORD; for thou hast raised me up, and hast not made my foes to rejoice over me.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 O LORD my God, I cried unto thee, and thou hast healed me.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 O LORD, thou hast brought up my soul from Sheol: thou hast kept me alive, that I should not go down to the pit. (Sheol h7585)
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
4 Sing praise unto the LORD, O ye saints of his, and give thanks to his holy name.
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 For his anger is but for a moment; in his favour is life: weeping may tarry for the night, but joy [cometh] in the morning.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 As for me, I said in my prosperity, I shall never be moved.
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 Thou, LORD, of thy favour hadst made my mountain to stand strong: thou didst hide thy face; I was troubled.
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 I cried to thee, O LORD; and unto the LORD I made supplication:
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 What profit is there in my blood, when I go down to the pit? Shall the dust praise thee? shall it declare thy truth?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Hear, O LORD, and have mercy upon me: LORD, be thou my helper.
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Thou hast turned for me my mourning into dancing; thou hast loosed my sackcloth, and girded me with gladness:
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 To the end that [my] glory may sing praise to thee, and not be silent. O LORD my God, I will give thanks unto thee for ever.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.

< Psalms 30 >