< Psalms 113 >

1 Praise ye the LORD. Praise, O ye servants of the LORD, praise the name of the LORD.
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 Blessed be the name of the LORD from this time forth and for evermore.
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 From the rising of the sun unto the going down of the same the LORD’S name is to be praised.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 The LORD is high above all nations, and his glory above the heavens.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 Who is like unto the LORD our God, that hath his seat on high,
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 That humbleth himself to behold [the things that are] in heaven and in the earth?
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 He raiseth up the poor out of the dust, and lifteth up the needy from the dunghill;
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 That he may set him with princes, even with the princes of his people.
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 He maketh the barren woman to keep house, [and to be] a joyful mother of children. Praise ye the LORD.
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< Psalms 113 >