< Psalms 108 >

1 A Song, a Psalm Of David. My heart is fixed, O God; I will sing, yea, I will sing praises, even with my glory.
Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2 Awake, psaltery and harp: I myself will awake right early.
Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
3 I will give thanks unto thee, O LORD, among the peoples: and I will sing praises unto thee among the nations.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
4 For thy mercy is great above the heavens, and thy truth [reacheth] unto the skies.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
5 Be thou exalted, O God, above the heavens: and thy glory above all the earth.
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 That thy beloved may be delivered, save with thy right hand, and answer us.
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
7 God hath spoken in his holiness; I will exult: I will divide Shechem, and mete out the valley of Succoth.
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
8 Gilead is mine; Manasseh is mine; Ephraim also is the defence of mine head; Judah is my sceptre.
Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
9 Moab is my washpot; upon Edom will I cast my shoe: over Philistia will I shout.
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
10 Who will bring me into the fenced city? who hath led me unto Edom?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
11 Hast not thou cast us off, O God? and thou goest not forth, O God, with our hosts.
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
12 Give us help against the adversary: for vain is the help of man.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
13 Through God we shall do valiantly: for he it is that shall tread down our adversaries.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.

< Psalms 108 >